quimby_joey
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 391
- 175
Nimefatilia kwa karibu hali inayoendelea nchini Libya kuung'oa utawala wa Col. Ghadafi, nimekosa imani kabisa na vyombo vya habari vya kimagharibi (BBC, Sky News) pamoja na kile cha wamarekani (CNN) toka watangaze waasi wa libya wanashikilia asilimia 90 ya mji wa Tripoli wamekua wakitoa taarifa zisizo na uhakika pamoja na kutuonesha live nini kinachoendelea. Hizi ni baadhi:
i. Kwamba, waasi wanashikilia 90% ya mji wa Tripoli (BBC), CNN wanasema 80%
ii. Correspondents wa BBC toka juzi wanasema waasi wameuteka mji wote na hawatorudi nyuma wala hakuna vipingamizi walivyokutana navyo usiku wa kuamkia leo wanatuambia waasi itabidi wasikae Tripoli warudi kwani hali bado si shwari mji haujatulia kutokana na majeshi ya Ghadafi kushambulia (BBC,CNN).
iii. BBC, Sky News,CCN walitoa taarifa toka juzi kuwa watoto 3 wa Col. Ghadafi wamekamatwa na wanashikiliwa na waasi, alfajiri ya leo Saif Al-Islam kajitokeza hadharani na kukanusha kukamatwa kwake na kutoa taarifa kuwa babake yuko hai na salam na kwamba bado wanaushikilia mji wa Tripoli.
Je, nini maslahi ya vyombo hivi vya habari vya wazungu katika vita ya Libya, ilihali kulipotoka taarifa kuwa Afrika Kusini wamepeleka ndege yao kutorosha Ghadafi vyombo hivyo vya habari vilikuja juu kuilamu Afrika Kusini, ni wanachokitaka hawa watu?
i. Kwamba, waasi wanashikilia 90% ya mji wa Tripoli (BBC), CNN wanasema 80%
ii. Correspondents wa BBC toka juzi wanasema waasi wameuteka mji wote na hawatorudi nyuma wala hakuna vipingamizi walivyokutana navyo usiku wa kuamkia leo wanatuambia waasi itabidi wasikae Tripoli warudi kwani hali bado si shwari mji haujatulia kutokana na majeshi ya Ghadafi kushambulia (BBC,CNN).
iii. BBC, Sky News,CCN walitoa taarifa toka juzi kuwa watoto 3 wa Col. Ghadafi wamekamatwa na wanashikiliwa na waasi, alfajiri ya leo Saif Al-Islam kajitokeza hadharani na kukanusha kukamatwa kwake na kutoa taarifa kuwa babake yuko hai na salam na kwamba bado wanaushikilia mji wa Tripoli.
Je, nini maslahi ya vyombo hivi vya habari vya wazungu katika vita ya Libya, ilihali kulipotoka taarifa kuwa Afrika Kusini wamepeleka ndege yao kutorosha Ghadafi vyombo hivyo vya habari vilikuja juu kuilamu Afrika Kusini, ni wanachokitaka hawa watu?