Najuta kutupa pesa yangu VETA

Najuta kutupa pesa yangu VETA

Desierto

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2019
Posts
850
Reaction score
2,964
Kabla sijaenda niliomba ushauri kwanza wengine wakaniambia niende maana mafundi wa mtaani wengi ni wachoyo kukupa siri zote za kazi, na wengine wakaniambia nisiende maana hiyo pesa ya ada robo tu unapata fundi anakufundisha vizuri tu.

Llakini nikaona ni bora tu niende veta ila nilichokikuta huko ndugu yangu sikushauri na wewe uende.

Nilienda kusomea ufundi simu hardwire na softwire lakini mpaka namaliza sijui hata kutoa port ya kuchajishia simu, nimekuja kujifunzia huku mtaani na nimejua.

Kule ni kwenda tu kujua majina ya component na matatizo ya simu
Ni veta za serikali lakini.
 
Pole kijana, hujatoka bure huko veta kuna maisha umejifunza.
 
Ni upotezaji mkubwa sana wa muda kwenda veta.

huwa wanatoka weupe. yaani hakuna wanachokijua. zaidi utaambiwa tu hiki kinaitwa hivi hiki kinaitwa vile.
 
Kabla sijaenda niliomba ushauri kwanza wengine wakaniambia niende maana mafundi wa mtaani wengi ni wachoyo kukupa siri zote za kazi, na wengine wakaniambia nisiende maana hiyo pesa ya ada robo tu unapata fundi anakufundisha vizuri tu, lakini nikaona ni bora tu niende veta ila nilichokikuta huko ndugu yangu sikushauri na wewe uende,
Nilienda kusomea ufundi simu hardwire na softwire lakini mpaka namaliza sijui hata kutoa port ya kuchajishia simu, nimekuja kujifunzia huku mtaani na nimejua
Kule ni kwenda tu kujua majina ya component na matatizo ya simu
Ni veta za serikali lakini
 
nilimuita mjomba wangu alie somea veta miaka mitatu aje kiniwekea belt kwenye gari.chaajabu alishindwa licha yakuja namatilio yake.nikaenda gereji kuomba fundi anisaidie nikapewa kakijana kadogotu hakakuchukua hata dakika mbili tayari kamesha weka.mjomba nilimuuliza maswali kibao nikagundua hajui chochote
 
Sijaona upungufu wa VETA mpaka sasa... kwamba wanafundisha theory? Yes wanafundisha theory, ila ambacho ungetakiwa kufanya ni kuingia kitaa kupata uzoefu sambamba na elimu ya theory... na ndivo elimu ya bongo inatakiwa iwe..

Theory plus practical, kama practical hawatoi VETA kwa mapungufu yao, wewe inatakiwa ujiongeze ukaitafute practical kitaani
 
Elimu ya bongo kikubwa kupata cheti..just imagine unasoma diploma ya hydogeology ila ukienda kuchukua bachelor husomi kipya yaleyale unayarudia
 
Elimu ya bongo kikubwa kupata cheti..just imagine unasoma diploma ya hydogeology ila ukienda kuchukua bachelor husomi kipya yaleyale unayarudia
Kwamba mwanafunzi wa diploma hiyo course akiingia UE ya hiyo Course mambo fresh?
Au ni practical point of view?
 
Back
Top Bottom