Najuta kumuonea huruma na kutembea nae

Wanaume tumeumbwa mateso ee kuangaika : pole sana mkuu pambana kiume usikate tamaa mkuu.
 
Hi wana bodi,
Nipo na mawazo na majuto kwa kutembea na mtalaka wangu,
Mtalaka wangu tumeachana miaka minne iliyo pita, kinachoniuma kwa hii miaka minne ya kuachana nae kanisumbua sana kuanzia bakwata, ustawi wa jamii mpaka mahamakani ,huku kote akidai matunzo ya mtoto.
Anachotaka yeye ni mahakama impe %ya kipato changu badala ya mimi ninavyo mtumia.
Sasa kufuatana fuatana nimejikuta natembea nae ili kumshawishi asinipeleke mahakamani kwani sipendi kufikishwa huko.
Sasa ameanza usumbfu kuwa amenasa na alikuwa anataka sana mtoto wa nyongeza azae na mimi, na anasema Mungu amejibu dua yake kwani alikuwa ana ombea niwe baba wa watoto wake tena. Sasa kwa hii miaka minne shubiri niliyoipata kwake nimeichoka lakini mwezangu hajali kama mimi sasa Nina maisha mapya anachodai mimba hii tutailea wote tukiwa nyumba moja.
Naomba ushauri ,hivi kuna waganga wa kutoa mimba rimoteness.?
*Kutoa mimba hapo mie siafiki mkuu samahani sana!
 
Hongera zake huyo mwanamke angalau watoto wake watakuwa na baba mmoja sio kila mtoto na babaake
 
Huruma imekuponza. Na kwenye kesi ya huyu mtoto wa pili utamuonea huruma tena utapata wa 3. Hongera in advance.
 
Huruma imekuponza. Na kwenye kesi ya huyu mtoto wa pili utamuonea huruma tena utapata wa 3. Hongera in advance.
shida sana,kuwa nae lakini mapenzi ni kitu cha utata sana duniani.sijui imekuaje nikalala nae tena.
 
Haaaaaa ukachovya Tena..,.tena na tena....Lea wanao
Siogopi kulea,shida ni aina ya mama anaelea watoto wangu na ulimwengu huu wa sasa.
plus Wivu niue,wenye malipizo ya visasi,na kukomoana na kubagua watu kwa dini zao.na kutaka muda wote tujitenge na majirani,marafiki,ndugu,na jamii inizungukayo(alikuwa mke)
 
Unaogopa mahakamani bila wewe ni mwaume wa dar
mahakamani niliambiwa wanakata 10/ ya gloss salary ,pesa ambazo ni nyingi sana ma balance yangu ingebaki kiducbu sana kutokana na mikopo niliyonayo.
 
Baba waza kiutu uzima.
Nani alikuambia matapishi huliwa?
Nyie ndiyo mnaosababisha kesi za talaka ziwe ngumu sana kuhitimishwa mahamani.
Hivi mkienda mahakamani kuendeleza kesi yenu ya talaka wakati mmebebeshana mimba, hiyo mahakama inaweza kufikia maamuzi gani?
'Sitaki nataka' yako haistahili kuomba ushauri wowote, kwa sababu wewe ni mtu dhaifu sana usiyekuwa na msimamo wa maamuzi yako.
Na huenda michango hii uisomayo jf, waweza kwenda nayo kwa x-mtalaka wako na kumuangukia aisome!
 
Hi wana bodi,

Nipo na mawazo na majuto kwa kutembea na mtalaka wangu, mtalaka wangu tumeachana miaka minne iliyo pita, kinachoniuma kwa hii miaka minne ya kuachana nae kanisumbua sana kuanzia BAKWATA, Ustawi wa Jamii mpaka mahamakani, huku kote akidai matunzo ya mtoto.

Anachotaka yeye ni mahakama impe %ya kipato changu badala ya mimi ninavyo mtumia. Sasa kufuatana fuatana nimejikuta natembea nae ili kumshawishi asinipeleke mahakamani kwani sipendi kufikishwa huko.

Sasa ameanza usumbfu kuwa amenasa na alikuwa anataka sana mtoto wa nyongeza azae na mimi, na anasema Mungu amejibu dua yake kwani alikuwa ana ombea niwe baba wa watoto wake tena.

Sasa kwa hii miaka minne shubiri niliyoipata kwake nimeichoka lakini mwezangu hajali kama mimi sasa nina maisha mapya anachodai mimba hii tutailea wote tukiwa nyumba moja.

Naomba ushauri, hivi kuna waganga wa kutoa mimba rimoteness.?
Hehehe!!!!rimoteless(ndiyo nini mkuu)
 
Ndio ishatokea,Mishauri jinsi ya kumtoa mapema ,kuhusu kondom,sisi tunapanga yetu Mungu nae hupanga yake.
aisee ni kweli kujisahau kupo na kunagharimu....suala hapa la kutoa mimba na kuwe na mwafaka ya wote wawili na ilivyo sasa ni kwamba yeye anataka mrudiane na hii mimba ndio tiketi inayompa nguvu
sasa siku zote ni vyema kusimamia unchokiamini na kama unaona hakuna maisha ya doa ya kuongeza mtoto nae basi ni vyema ukakaa nae ukamwabia bila kutafuna maneno msimamo wako ni huu..
pia je wewe ushashuhudia kipimo kuhakiki uwepo wa hio mimba..
Ili ajue upo serious mwambia upo tayari sasa kwenda hata Bakwata na kwingine kupata suluhisho la matunzo n.k
otherwise all the best Mkuu
 
Back
Top Bottom