Najuta kumfahamu huyu binti

Najuta kumfahamu huyu binti

kholo

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2011
Posts
413
Reaction score
76
Habari za majukumu wana jf, kwa mara ya kwanza nimejikuta nikiingia katika jukwaa hili nikiwa muhanga na majeruhi wa kufa leo au kesho kwa sababu ya mapenzi, ni miaka 2 sasa imepita toka nimfahamu huyu binti anayeninyanyasa(tukiwa shule kipindi hicho) na katika kipindi cha mwaka mmoja tuliokuwa pamoja shule tuliishi vizuri ila sii kama wapenz, nilitokea kumpenda sana ila sikuthubutu kumwambia kutokana na kuhofia kuchanganya hali ya mambo japo baadaye aligundua. Na katika kipindi cha mwaka mzima tulipoachana baada ya kumaliza shule tuliendelea kuwasiliana japo kwa mara chache ila ugonjwa wangu haukuwa umetibika bado kwan kila nilipoisikia sauti yake mapigo ya moyo wangu yaliongeza kasi lakin pia sikumwambia kuwa nampenda. Zahama ilianza baada ya kumwambia ukweli kuwa nampenda mwezi 1 uliopita, alinikubalia na akaniambia hilo alilitambua toka mwanzo, cha ajabu kwangu imekuwa mateso kwan ninapoongea naye kwenye simu najisikia burudani sana ila simu iki katika tu na aman nayo inatoweka kwangu na hakuna ninachoweza kufanya kikawa sawa hata kula inakuwa shida, namuwaza yeye tuu. Natamani kusitisha uhusiano ila nafsi yangu inanambia ni afadhali mimi nife kuliko kusitisha uhusiano, nashindwa kuelewa kuwa nampenda au namtaman. Wanajamvi plz, ushauri wenu ni muhimu sana kwangu kwan najihisi kupungua uzito kwa kuwaza. Ahsanten
 
Duh mie nikahis kakupa ngoma kumbe ishu ya infatuation tu!! Usijal ukizowea hayo makitu hyo hali itakwisha
 
cha kufanya nenda kwa wazaziw ake tangaza nia mpose, kisha oa jumla uwe naye ndani 24/7 hapo kiu yako itakuwa imeisha

Kila la heri
King'asti hebu kidooogo punguza "unoko" mshauri kijana mwenzio
 
Last edited by a moderator:
Mapenzi pasua kichwa mkuu jitahidi kuzoea tu you will be fine. Je ukigundua hauko peke yako si ndio utacollapse?
 
Duh, hakunaga mapeeenzi yale, yakugandana ni zama za kale, hayanaga ujuuuzi yale, kila mtu analilia mapenzi.! Mapenzi yana nguvu Sana, nahisi huyo mtoto ni mzuri sana!
 
Umezama umezama kwenye bahari ya huba wewe kazana tu lkn angalia dont test the depth of river with both legs anza kwanza na mguu mmoja ili iwe rahisi kujikwamua usiondoke na mafuriko
 
cha kufanya nenda kwa wazaziw ake tangaza nia mpose, kisha oa jumla uwe naye ndani 24/7 hapo kiu yako itakuwa imeisha

Kila la heri
King'asti hebu kidooogo punguza "unoko" mshauri kijana mwenzio

nahisi kumpenda sana na lengo langu ni aje awe mama watoto wangu japo lengo langu la kuoa ni after 2 years toka sasa
 
Last edited by a moderator:
Duh, hakunaga mapeeenzi yale, yakugandana ni zama za kale, hayanaga ujuuuzi yale, kila mtu analilia mapenzi.! Mapenzi yana nguvu Sana, nahisi huyo mtoto ni mzuri sana!

Hapana, sii mzuri saana kiivo ka ng'ang'ania tu mzizi wa moyo wangu. Nimewahi kuwa na mahusiano na wasichana wazur kuliko yeye lakin hawakuwahi kunipa uchiz kama anavyoniendesha huyu mwanamke
 
Huko ndio kupenda mkuu...unahisi kama butterflies tumboni wakati huo huo kama electricity mwilini....
 
Huu mwaka wako mbona utakoma nimeshtushwa na msemo wako kuwa wee unakonda ye ananenepa.
 
nahisi kumpenda sana na lengo langu ni aje awe mama watoto wangu japo lengo langu la kuoa ni after 2 years toka sasa

huo muda huo uliojiwekea na ye kauridhia maana ukishindwa kubalance hapa utamsikia hewani tu
 
Mhhhh ukishakula mchezo zaidi ya mara 5 ndo utajua unampenda au???
 
Back
Top Bottom