Najuta kulipandia........

Udereva si tatizo, e ndugu yangu sikia
Fungua na masikio, hoja hujaipatia
Sio waja mbio mbio, dereva wanidhania
Mbona nilisha eleza, udereva nimefuzu

Mabovu wayatetea, njiani kusafiria
vipi tatuelezea, safari kikudodea
Ni mabaya mazoea, vundo kuukodolea
Mbona nilisha eleza, udereva nimefuzu


sindano mwana wa ganzi

Yakuonea wataka ligi,na kikombe kuchua.
Sio kama siiwezi,hilo kaa ukijua.
Nataka kui maizi,kindaki ndaki kujua.
Sasa nakupa mji,hoja kunifumbilia.
 
Hakuna ligi yoyote, ewe matuka sikia
Na fani ni yetu sote, huoni twafurahia
vipi unipe kikombe, na mji watoa pia
Hoja ni kutofikishwa, kama nilivyodhamiria

Utaonaje furaha, gari yakuzimikia
Mimi kwangu ni karaha, wepesi sitasikia
Kweli hata ukihaha, injini imejifia
Hoja ni kutofikishwa, kama nilivyodhamiria

sindano mwana wa ganzi

Yakuonea wataka ligi,na kikombe kuchua.
Sio kama siiwezi,hilo kaa ukijua.
Nataka kui maizi,kindaki ndaki kujua.
Sasa nakupa mji,hoja kunifumbilia.
 
Gari hili si la kwangu, ndugu ninakuambia
Liliona toka tangu, nikataka jipandia
Na wala si la mafungu, kweli ninakuapia
Lipi sasa nitapanda, mengi mechakachuliwa

Kupanda la pili si hoja, ubora ndo zingatio
Mengi ya sasa viroja, kufika ndo kusudio
Sitaki safari moja, nizugishwe na vilio
Lipi sasa nitapanda, mengi mechakachuliwa

kwa nje yanavutia, machoni tatamania
Mikono ukishatia, ndani kujichunguzia
Tashindwa kuaminia, tafiti utanambia
Lipi sasa nitapanda, mengi mechakachuliwa


sindano mwana wa ganzi

Gari linalotembea,
Linaloingizwa gia,
Usukani shikilia,
Safari yaendelea.

Safari utaifika, piga konde moyo wako.

Kishaingia garini,
Uendapo safarini,
Siangalie nyumani,
Safari iko mbeleni.

Gari likisha tumika, Siyo limekongoroka.

Ya nyuma kuyawazia,
Moyo wajiumizia,
Wala hitosaidia,
Safari yakungojea

Magari yalotumika, Bado yapo safarini.

Garini kishaingia,
Nyuma acha angalia,
Safari itaishia,
Nyumani kutakukwaza.

Safari iko mbeleni, siyo nyuma utokako.

Gari kijinyakulia,
Safari hakikishia,
Gari sevisi fanyia,
Safari itanogea.

Gari yake ni sevisi, Na siyo uzuri sura.
 
Safari mwendo mrefu, pwani mpaka arusha
kwa gari la hitilafu, ndugu tachemsha
Njia zitifutifu, kifika mehatisha
Kwa gia ya namba moja, je kweli utafika

Kiweka gia ya pili, gari lakugomea
vipi hili takabili, safari kuisogeza
Au ndo utakatili, lingine kujizolea
kwa gia ya namba moja, je kweli tutafika


sindano mwana wa ganzi


Gari linalotembea,
Linaloingizwa gia,
Usukani shikilia,
Safari yaendelea.

Safari utaifika, piga konde moyo wako.

Kishaingia garini,
Uendapo safarini,
Siangalie nyumani,
Safari iko mbeleni.

Gari likisha tumika, Siyo limekongoroka.

Ya nyuma kuyawazia,
Moyo wajiumizia,
Wala hitosaidia,
Safari yakungojea

Magari yalotumika, Bado yapo safarini.

Garini kishaingia,
Nyuma acha angalia,
Safari itaishia,
Nyumani kutakukwaza.

Safari iko mbeleni, siyo nyuma utokako.

Gari kijinyakulia,
Safari hakikishia,
Gari sevisi fanyia,
Safari itanogea.

Gari yake ni sevisi, Na siyo uzuri sura.
 
Vipi niendeshe mbele, nyuma nikususie
Hii jamani kasheshe, mi nawe tufikirie
Gari zenyewe mikweche, nyuma pia tuwazie
Ninapoendesha mbele, nyuma siachi tazama

kama megongwa kwa nyuma, ni vipi utabaini
Au pengine ni chuma, kwa kati kimehaini
Na hata ukijituma, hapa safari huwini
Ninapoendesha mbele, nyuma siachi tazama

vioo tumefungiwa, pembeni kwenye magari
lengo kutotapeliwa, tuone nyuma ya hatari
sitaki uje pagawa, hebu fanya tafakari
Ninapoendesha mbele, nyuma siachi tazama

sindano mwana wa ganzi


Gari linalotembea,
Linaloingizwa gia,
Usukani shikilia,
Safari yaendelea.

Safari utaifika, piga konde moyo wako.

Kishaingia garini,
Uendapo safarini,
Siangalie nyumani,
Safari iko mbeleni.

Gari likisha tumika, Siyo limekongoroka.

Ya nyuma kuyawazia,
Moyo wajiumizia,
Wala hitosaidia,
Safari yakungojea

Magari yalotumika, Bado yapo safarini.

Garini kishaingia,
Nyuma acha angalia,
Safari itaishia,
Nyumani kutakukwaza.

Safari iko mbeleni, siyo nyuma utokako.

Gari kijinyakulia,
Safari hakikishia,
Gari sevisi fanyia,
Safari itanogea.

Gari yake ni sevisi, Na siyo uzuri sura.
 
Hakuna ligi yoyote, ewe matuka sikia
Na fani ni yetu sote, huoni twafurahia
vipi unipe kikombe, na mji watoa pia
Hoja ni kutofikishwa, kama nilivyodhamiria

Utaonaje furaha, gari yakuzimikia
Mimi kwangu ni karaha, wepesi sitasikia
Kweli hata ukihaha, injini imejifia
Hoja ni kutofikishwa, kama nilivyodhamiria

sindano mwana wa ganzi


Mwenye kuanza safari,nia kwisha jitilia.
Kufika ame hiyari,hiyo ndio kidunia.
Miguu ama gari,kufika ndio dhamira.
Hato kwama vuli,kipupwe yake masika.

Safari namna hizi,gari yako nunua.
Yenye kupendeza machoni,na kupanda pia.
Chagua rangi thamani,nyeupe au kahawia.
Mifumo kwenye injini,vyema uka somea.

Ukilimiliki gari,utajua na kutumia.
Kasi kwenye lami,na matope kudemea.
Salama na makini,safarini wa tanua.
Sio lile la kukodi,ingawa lina vutia.
 
Sanda nimekusikia, yote uliyo usia
Sawa nitakusudia, la kwangu kujipatia
Niache ya kudandia, safarini sitafika
Wapi naweza pata, la injini siyoguswa

Sitaki eti lolote, moyoni sitaridhia
Au la kwenye matope, mjini yana kadhia
Kuna yale kiokote, kinunua tajutia
Wapi naweza pata, la injini siyoguswa

Nataka liwe jipya, mashine kichungulia
Hapa nina uhakika, dunia tazungukia
Nitaondokwa mashaka, sababu nalijulia
wapi naweza pata, la injini siyoguswa

Siwezi nunua gari, iliyokwisha tumika
Na kila siku si shwari, sipana ninajitwika
Nyingi kikiri kikiri, wabaki wataabika
wapi naweza pata, la injini isoguswa

sindano mwana wa ganzi


Mwenye kuanza safari,nia kwisha jitilia.
Kufika ame hiyari,hiyo ndio kidunia.
Miguu ama gari,kufika ndio dhamira.
Hato kwama vuli,kipupwe yake masika.

Safari namna hizi,gari yako nunua.
Yenye kupendeza machoni,na kupanda pia.
Chagua rangi thamani,nyeupe au kahawia.
Mifumo kwenye injini,vyema uka somea.

Ukilimiliki gari,utajua na kutumia.
Kasi kwenye lami,na matope kudemea.
Salama na makini,safarini wa tanua.
Sio lile la kukodi,ingawa lina vutia.
 
Polepole elezea, kipi kilicho vutia
Kwa gari silolijua,nini umekimbilia
Ulipenda ya njiani,sasa yamekutokea
Sio yote yavutia,mengine vimeo pia

Umakini wa viwango,hiyo ndiyo zingatia
Achana na maringo,hayo ndo yazuzua
Waparamia korongo,ni kwanini wajutia
Sio yote yavutia.mengine vimeo pia.

Gari zuri kwenye yadi,hilo ndilo lazuzua
Yapo mengi kwa idadi, na ndani yametulia
Nje na ndani maridadi,jinsi yanavyovutia
Sio yote yavutia.mengine vimeo pia.
 
Sanda nimekusikia, yote uliyo usia
Sawa nitakusudia, la kwangu kujipatia
Niache ya kudandia, safarini sitafika
Wapi naweza pata, la injini siyoguswa

Sitaki eti lolote, moyoni sitaridhia
Au la kwenye matope, mjini yana kadhia
Kuna yale kiokote, kinunua tajutia
Wapi naweza pata, la injini siyoguswa

Nataka liwe jipya, mashine kichungulia
Hapa nina uhakika, dunia tazungukia
Nitaondokwa mashaka, sababu nalijulia
wapi naweza pata, la injini siyoguswa

Siwezi nunua gari, iliyokwisha tumika
Na kila siku si shwari, sipana ninajitwika
Nyingi kikiri kikiri, wabaki wataabika
wapi naweza pata, la injini isoguswa

sindano mwana wa ganzi


Sindano mwana ganzi,sije leta msiba.
Ukayaleta majonzi,chozi silo tiba.
Kwa kuleta weredi,injini kuzi chunguza.
Waweza leta ufundi,wenzio kwisha chakachua.

Walikuwapo wakwezi,mabingwa wa kupalamia.
Miembe na minazi,wako juu kudandia.
Matawi yakawa telezi,ahera kwenda mapema.
Magari sio nazi,ikivunjwa unaona.

Japo kwenye yadi,utacheza patapotea.
Yapo ya toka enzi,rami yana chubua.
Jaifongo na Bedifodi,yang'aa kama Korola.
Upwa injini si kazi,dukani wenda nunua.

Waweza pata uchizi,ukweli kuja fahamu.
Kuna yale Mashangingi,bei milioni mia.
Injini ni za Bajaji,zile kutoka India.
Bora kuacha chunguzi,safari unapo ridhia.
 
Ni vipi wayasifia, magari yale ya yadi
Mbwembwe wayamiminia, kuwa ni yamaridadi
Ulaya lishatumia, na sasa hayana hadhi
Magari haya ya yadi, yalisha pandwa kitambo

Elfu kwa maelfu, maili yametembea
Huku kwetu twayasifu, mjini twagereshea
Huu kwangu ni upofu, ya yadi nayabezea
Magari haya ya yadi, yalisha pandwa kitambo

Dereva walisha kaa, ndani wakayaendesha
Yalivyo pata chakaa, kwetu wakayasogesha
Mie leo nashangaa, wengi yawahamasisha
Magari haya ya yadi, yalisha pandwa kitambo


sindano mwana wa ganzi


Polepole elezea, kipi kilicho vutia
Kwa gari silolijua,nini umekimbilia
Ulipenda ya njiani,sasa yamekutokea
Sio yote yavutia,mengine vimeo pia

Umakini wa viwango,hiyo ndiyo zingatia
Achana na maringo,hayo ndo yazuzua
Waparamia korongo,ni kwanini wajutia
Sio yote yavutia.mengine vimeo pia.

Gari zuri kwenye yadi,hilo ndilo lazuzua
Yapo mengi kwa idadi, na ndani yametulia
Nje na ndani maridadi,jinsi yanavyovutia
Sio yote yavutia.mengine vimeo pia.
 
Back
Top Bottom