klorokwini
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 8,648
- 5,139
Kama gari si la kwako, vipi linakusumbuayou are the reason behind this, shairi lako 'from me to you' was my turning point, much respect
Vipi nipige mnada, kwa gari lisilo langu
Nilitaka tu kupanda, linifikishe mwenzangu
Kwa miguu sitakwenda, sitaki kizungu zungu
Gari hili sio langu, siwezi piga mnada
vipi ningelijulia, kama ni gari makini
Waweza nisaidia, mwenzio sikubaini
Mafuta livujishiwa, sikuiona injini
Gari hili sio langu, siwezi piga mnada
Lirejeshe litokako , spea zako chukua
Gari hilo ni kituko, halifai kutumia
Tafuta lililo lako , ila hadhari chukua
Gari zima walijua , ufunguo ukitia
Mvumo huwa murua, gia laini kuingia
Resi ukikanyagia , moshi si wa kupalia
Oili kiangalia , ni nzito ilokozea.
Chungulia na mashine, uione gasketi
Zinavujisha nyengine , eneo lake la kati
Rejieta ni chengine, ujue halichemshi
Otaneta isiwe nene, ifiti na breketi
Ingia barabarani, lijaribu kwa safari
Anza spidi ya chini, kuiepuka hatari
Likanyage thamanini, ukiliona lishwari
Uzamie mvunguni , njiani likikuadhiri
Njiani likikuadhiri, uzamie mvunguni.
Kwanza urudi safari, ukatulie nyumbani
Ila ujue tayari , hilo gari si makini
Ni vyema ukaghairi, ukalitupa jaani