Sanda Matuta
JF-Expert Member
- May 9, 2007
- 949
- 134
Ati....!!!!,nini?? Mkokoteni..!!!!!????ha ha ha ha ha ha ha!
I salute mzeeSalamu nawatumia, magwiji mlochangia,
Swali nimelipitia, majibu yanavutia,
Nami nikaazimia, ujumbe kuwapatia,
Gari siyo gari lile,
Gari ni mkokoteni!
Muda nimeutumia, swali kulifikiria,
Ndipo iliponijia, hadi nikashangilia,
Jibu nikalipatia, la fumbo alilofumbia,
Gari siyo gari lile,
Gari ni mkokoteni!
Linafanana na kia, ndivyo ametuambia,
Gharama ni rahisia, si ghali tumesikia,
Miye namkubalia, la chee kalipandia,
Gari siyo gari lile,
Gari ni mkokoteni!
La rangi ya kahawia, gari akalisifia,
Magari tunajulia, hakuna ya kahawia,
Ni mbao kazisifia, mkokoteni karukia,
Gari siyo gari lile,
Gari ni mkokoteni!
Tena akatuambia, mbele limetanukia,
Lipi liko kama kia, mbele limejiachia?
Yale ya kusukumia, kwa mbele na nyuma pia,
Gari siyo gari lile!
Gari ni mkokoteni!
Nyuma akalisifia, mbinuko unavutia,
Wallahi sijasikia, gari linabinukia,
Jinsi ninavyojulia, mkokoteni kasifia!
Gari siyo gari lile,
Gari ni mkokoteni!
Tena akalipandia, kati akajiachia,
Wapi umeshasikia, kupanda ukatandia,
Mkokoteni ukipandia, kati utatanulia!
Gari siyo gari lile,
Gari ni mkokoteni!
Gari alilopandia, kelele alisikia,
Mbele halikuhamia, kashindwa kusukumia,
Limekosa girisia, mkweche kaudandia!
Gari siyo gari lile,
Ni gari mkokoteni!
Pole ninakugaia, kwa uliyojitakia,
Gari ulilopandia, si gari nakuambia,
Tairi zilizugia, wewe ukalidandia,
Gari siyo gari lile,
Ni gari mkokoteni!
Kelele ulizosikia, mgosi anavutia,
Wewe ukafikiria, benzi umelidandia,
Nne ukajikunjia, sigara unavutia,
Gari siyo gari lile,
Ni gari mkokoteni.
Safari ikikujia, kwanza anza ulizia,
Tafiti na tafutia, kabla hujalidandia,
Ujue kama ni kia, au lori la skania,
Gari siyo gari lile,
Ni gari mkokoteni!
Beti ninaziachia, fumbo nimefumbulia,
Natumai utaachia, gari la kufikiria,
Kisha utajipangia, la ukweli kupatia,
Gari ulilodandia,
Ni gari mkokoteni!!
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
Salamu nawatumia, magwiji mlochangia,
Swali nimelipitia, majibu yanavutia,
Nami nikaazimia, ujumbe kuwapatia,
Gari siyo gari lile,
Gari ni mkokoteni!
Muda nimeutumia, swali kulifikiria,
Ndipo iliponijia, hadi nikashangilia,
Jibu nikalipatia, la fumbo alilofumbia,
Gari siyo gari lile,
Gari ni mkokoteni!
Linafanana na kia, ndivyo ametuambia,
Gharama ni rahisia, si ghali tumesikia,
Miye namkubalia, la chee kalipandia,
Gari siyo gari lile,
Gari ni mkokoteni!
La rangi ya kahawia, gari akalisifia,
Magari tunajulia, hakuna ya kahawia,
Ni mbao kazisifia, mkokoteni karukia,
Gari siyo gari lile,
Gari ni mkokoteni!
Tena akatuambia, mbele limetanukia,
Lipi liko kama kia, mbele limejiachia?
Yale ya kusukumia, kwa mbele na nyuma pia,
Gari siyo gari lile!
Gari ni mkokoteni!
Nyuma akalisifia, mbinuko unavutia,
Wallahi sijasikia, gari linabinukia,
Jinsi ninavyojulia, mkokoteni kasifia!
Gari siyo gari lile,
Gari ni mkokoteni!
Tena akalipandia, kati akajiachia,
Wapi umeshasikia, kupanda ukatandia,
Mkokoteni ukipandia, kati utatanulia!
Gari siyo gari lile,
Gari ni mkokoteni!
Gari alilopandia, kelele alisikia,
Mbele halikuhamia, kashindwa kusukumia,
Limekosa girisia, mkweche kaudandia!
Gari siyo gari lile,
Ni gari mkokoteni!
Pole ninakugaia, kwa uliyojitakia,
Gari ulilopandia, si gari nakuambia,
Tairi zilizugia, wewe ukalidandia,
Gari siyo gari lile,
Ni gari mkokoteni!
Kelele ulizosikia, mgosi anavutia,
Wewe ukafikiria, benzi umelidandia,
Nne ukajikunjia, sigara unavutia,
Gari siyo gari lile,
Ni gari mkokoteni.
Safari ikikujia, kwanza anza ulizia,
Tafiti na tafutia, kabla hujalidandia,
Ujue kama ni kia, au lori la skania,
Gari siyo gari lile,
Ni gari mkokoteni!
Beti ninaziachia, fumbo nimefumbulia,
Natumai utaachia, gari la kufikiria,
Kisha utajipangia, la ukweli kupatia,
Gari ulilodandia,
Ni gari mkokoteni!!
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
Ati....!!!!,nini?? Mkokoteni..!!!!!????ha ha ha ha ha ha ha!
JAMANI EEH,HILO SIO GARI.ETI LIMEBINUKA,DOH!HAKUNA GARI LENYE MA BEHIND MAKUBWA,HILO NI UPANDE WETU WA PILI TU.LOL:becky:
Hongera kwa mashairi mazuri,pole mwanakwetu mbona kuna gari mpya zipo zinauzwa hayo ya zamani sisi tumeyaacha