GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,738
- 109,177
Kwa yanayoendelea kwa sasa nchini Tanzania huku na hawa Wanaharakati wawili mmoja wa Upinzani na mwingine wa Serikali akina Mange Kimambi na Cyprian Musiba nahisi wamebakisha muda mchache mno wa kunifanya GENTAMYCINE niwe Taahira kabisa kutokana na wanayoaandika na kuyazungumza.
Kuna lililojificha na ' bomu ' kubwa linakuja nchini Tanzania kama hawa wote hawatasikilizwa na Wahusika kuyafanyia Kazi huku Watanzania kwa ujumla wetu tukikubali kuwa kuna mahala kama Taifa tumekosea kisha wote tuombane radhi / msamaha na tukubaliane kuanza upya kwa maslahi mapana ya Mama Tanzania yetu.
Nisiwaficheni sasa naanza ' Kuogopa ' juu ya mambo yanavyokwenda na naanza kuamini kuwa Mange Kimambi huwa yupo sahihi 100% na hata huyu Cyprian Musiba ne yupo sahihi kwa 100% kutokana na kwamba Wawili wote hawa ' taarifa ' zao zote huwa wanazitoa kule kule Makao Makuu ya ' Unyeti na Uzandiki ' nchini Tanzania hivyo hawabahatishi.
Mwenyezi Mungu nakuomba ingilia kati haraka kwani kwa dalili ninazoziona sasa kama ' Malaika ' wako pamoja na Wewe hamtoingilia kati ile Tanzania ya Hayati Baba wa Taifa Nyerere, ya Mzee Mwinyi, ya Mzee Mkapa na ya Mzee Kikwete inakwenda kupotelea kama siyo hata Kuangukia kwa Baba Dkt. Magufuli.
Leo GENTAMYCINE nina OMBI muhimu Kwenu hebu naomba Watanzania wote bila kujali tofauti zetu za Kivyama au Kidini au Kijiografia basi tushikane mikono popote pale na tuombane ' Misamaha ' kwa yote yaliyopita na naomba kila Mtu kwa Imani yake akienda ' Ibadani ' aiombee Tanzania yetu Uvumulivu, Upendo na Amani.
Narudia tena kusema ' Ninaogopa ' mno na kuna dalili fulani ya ' hatari ' naiona kwa mbali sana inakuja. Tujitafakari haraka sana!
Nawasilisha.
Kuna lililojificha na ' bomu ' kubwa linakuja nchini Tanzania kama hawa wote hawatasikilizwa na Wahusika kuyafanyia Kazi huku Watanzania kwa ujumla wetu tukikubali kuwa kuna mahala kama Taifa tumekosea kisha wote tuombane radhi / msamaha na tukubaliane kuanza upya kwa maslahi mapana ya Mama Tanzania yetu.
Nisiwaficheni sasa naanza ' Kuogopa ' juu ya mambo yanavyokwenda na naanza kuamini kuwa Mange Kimambi huwa yupo sahihi 100% na hata huyu Cyprian Musiba ne yupo sahihi kwa 100% kutokana na kwamba Wawili wote hawa ' taarifa ' zao zote huwa wanazitoa kule kule Makao Makuu ya ' Unyeti na Uzandiki ' nchini Tanzania hivyo hawabahatishi.
Mwenyezi Mungu nakuomba ingilia kati haraka kwani kwa dalili ninazoziona sasa kama ' Malaika ' wako pamoja na Wewe hamtoingilia kati ile Tanzania ya Hayati Baba wa Taifa Nyerere, ya Mzee Mwinyi, ya Mzee Mkapa na ya Mzee Kikwete inakwenda kupotelea kama siyo hata Kuangukia kwa Baba Dkt. Magufuli.
Leo GENTAMYCINE nina OMBI muhimu Kwenu hebu naomba Watanzania wote bila kujali tofauti zetu za Kivyama au Kidini au Kijiografia basi tushikane mikono popote pale na tuombane ' Misamaha ' kwa yote yaliyopita na naomba kila Mtu kwa Imani yake akienda ' Ibadani ' aiombee Tanzania yetu Uvumulivu, Upendo na Amani.
Narudia tena kusema ' Ninaogopa ' mno na kuna dalili fulani ya ' hatari ' naiona kwa mbali sana inakuja. Tujitafakari haraka sana!
Nawasilisha.