Naitafuta gari yangu

Naitafuta gari yangu

565099_a.jpg
hio ndio ilivyo ina tintid nyeusi kabisa

Acha ujinga wewe,picha hii gari iko chumba cha kupigia picha magari Beforward Japan. Gari yako T....AMS iweje hivi?
 
sasa unatafuta gari au unamtafuta uliyemuachia gari?

vipi mkuu!!
 
inside job labda kama bima na siwezi kufanya upuuzi huo na 4ur short information bima yangu ilikwisha
 
kuna mtu humu ndani kandika kaiona kwa macheni naenda kuingalia naitafuta kama iko pale
 
Mtu mwenyewe kajiandikisha leo, achaneni naye anatuzuga tuu
 
salaam wana jamii tafadhalini naitafuta gari yangu aina ya toyota harrier rangi ya silver namba T445AMS napatika kwenye namna hii 0716041044 au email kikoto007@gmail.com nimeshatoa ripoti polisi

mbona maelezo ya gari hili yanafanana na maelezo yaliyopo kwenye kesi ya Nyirabu v/s Ms Lyimo?!, si kesi ya kudai urudishiwe gari la uchumba iko mahakamani?! Umeamua kuja kushitaki humu JF?, funy anyway!
 
mbona maelezo ya gari hili yanafanana na maelezo yaliyopo kwenye kesi ya Nyarari v/s Ms Lyimo?!, si kesi ya kudai urudishiwe gari la uchumba iko mahakamani?! Umeamua kuja kushitaki humu JF?, funy anyway!

Nyalali au NYIRABU
 
Ni Nyirabu, asante na nimeshafanya masahihisho.

MBONA SILO LENYEWE?


MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi ya Kisutu Dar es Salaam imetengua hukumu ya kesi inayomhusu Christopher Nyirabu anayedaiwa kumhonga gari aina ya Toyota Harrier la thamani ya Sh milioni 28 mpenzi wake wa zamani Carolyn Lyimo, ili kumpa nafasi Lyimo kushiriki kwenye kesi hiyo.

Katika hukumu ya awali iliyotolewa Mei mwaka jana mahakama ilimwamuru Lyimo amrudishie Nyirabu gari alilomnunulia mwaka 2003 akitarajia wangeoana. Lakini katika uamuzi uliotolewa mwishoni mwa wiki, Hakimu Mkazi Mfawidhi Pellagia Khaday alisema ni vema hukumu hiyo ikitenguliwa kwa kuwa alisikia kuwa kesi hiyo ilisikilizwa na kutolewa hukumu wakati Lyimo akiwa nje ya nchi.

Kutokana na hali hiyo, Hakimu Khaday ameamua sasa kesi hiyo ianze kusikilizwa upya huku pande zote mbili zikishiriki na amepanga kesi hiyo isikilizwe Jumatatu ijayo. Inasemekana Lyimo na Nyirabu walikuwa ni wapenzi na waliishi pamoja kwenye nyumba ya Nyirabu kiwanja namba 54 A eneo la Msasani kati ya Aprili 2002 na Oktoba 2004 kwa ahadi na matarajio ya kuoana baadaye.

Katika kipindi walichokuwa pamoja inadaiwa Nyirabu alimlipia Lyimo ada ya mafunzo ya kompyuta yenye thamani ya Sh milioni 2.2 katika Chuo cha Teknolojia ya Mawasiliano (IIT) cha jijini na pia alimnunulia gari hilo lililokuwa na namba T 471 ADQ na kulisajili kwa jina la Lyimo.

Inadaiwa ilipofika Oktoba 22 mwaka 2004, Lyimo alighairi kuolewa na kuondoka nyumbani kwa Nyirabu bila maelezo huku akibeba vitu vyake vyote pamoja na gari bila kuonyesha nia ya kulirudisha.

Lyimo pia inadaiwa baada ya kuondoka alikwenda kuolewa na mwanamume mwingine, jambo ambalo Nyirabu anaona alikiuka makubaliano yao na ahadi aliyoitoa awali ya kuoana. Baada ya Lyimo kukataa kurudisha gari, Nyirabu alifungua kesi akidai alifedheheshwa na kuvunjwa moyo na kupata hasara baada ya ahadi yao kutotimizwa.

Ndipo Mei 25 mwaka jana Mahakama hiyo ikaamuru Nyirabu apewe gari lake baada ya kuridhika kwamba hakukuwa na ushahidi wa kutosha unaoonyesha kuwa gari hilo lilinunuliwa kama zawadi kwa Lyimo, bali kwa matumizi ya Lyimo kama mke mtarajiwa. Baada ya kupata hukumu ya mahakama, Februari 6 mwaka huu Lyimo alimwagiza wakili wake Joseph Rutabingwa kupeleka maombi maalumu mahakamani ili hukumu hiyo itenguliwe kwa kuwa hakujulishwa maendeleo ya kesi ya awali kama inavyotakiwa.
 
kuna mtu humu ndani kandika kaiona kwa macheni naenda kuingalia naitafuta kama iko pale

Angalia usije ukaibiwa zaidi. Yaani mtu akuibie gari halafu aranderande nayo kwa macheni?!!
Hii stroy yako iko too vague anyway...
 
Tuwekee picha tunaweza fananisha!! Ila kwa numba tu Itakuwa ngumu, pia Anaweza kubadilisha tu kwa kuzuga!! Sasa Umemuazima gari Hata humjui anakoishi?? You are Kidding!! Au Ilikuwa Calabash unapata moja Baridi na moto?

Information mbona vipande vipande au ndio ku-panic baada ya kupoteza gari? Maana huwa wanasema ukipoteza gari unaeza tafuta ktk mifuko ya suruali.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom