VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Nina masikitiko makubwa kuhusu Kinondoni. Tangu niamke leo,hata kazini nimechelewa kwenda,nimekuwa nikilia kwa uchungu kuiona Manispaa ya Kinondoni ikirudi mikononi mwa CCM.
Sijalia kwa jinsi CCM ilivyotwaa Umeya na Unaibu Meya wa Kinondoni. Najua mchuano wa kimahakama utafuata. Nimelia kwa masikitiko kuona Kinondoni ikirejea kwenye mkwamo wa kimaendeleo.
Tangu kuanza kwa vyama vingi,Dar ilikuwa chini ya CCM,ikiwemo Kinondoni. Mambo yalifanyika kwa mazoea. Kodi ilikusanywa kwa mazoea. Miundombinu ilijengwa kwa mazoea. Mazoea yanarudi. Kulindana na kukwepana.
Walipoingia UKAWA chini ya Meya Boniface Jacob pale Kinondoni,mambo yalibadilika. Makusanyo ya kodi yaliongezeka. Bajeti za miradi na wafadhili vilinona. Hakukuwa,kwenye kukusanya kodi,na upendeleo wowote.
Kwaheri Kinondoni yenye kwenda mbele,karibu Kinondoni ya mazoea. Wapenda mteremko na kupendelewa kwa kulindwa wanashangilia. Mimi nalia!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Sijalia kwa jinsi CCM ilivyotwaa Umeya na Unaibu Meya wa Kinondoni. Najua mchuano wa kimahakama utafuata. Nimelia kwa masikitiko kuona Kinondoni ikirejea kwenye mkwamo wa kimaendeleo.
Tangu kuanza kwa vyama vingi,Dar ilikuwa chini ya CCM,ikiwemo Kinondoni. Mambo yalifanyika kwa mazoea. Kodi ilikusanywa kwa mazoea. Miundombinu ilijengwa kwa mazoea. Mazoea yanarudi. Kulindana na kukwepana.
Walipoingia UKAWA chini ya Meya Boniface Jacob pale Kinondoni,mambo yalibadilika. Makusanyo ya kodi yaliongezeka. Bajeti za miradi na wafadhili vilinona. Hakukuwa,kwenye kukusanya kodi,na upendeleo wowote.
Kwaheri Kinondoni yenye kwenda mbele,karibu Kinondoni ya mazoea. Wapenda mteremko na kupendelewa kwa kulindwa wanashangilia. Mimi nalia!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam