Naishinda vipi hii vita?

Naishinda vipi hii vita?

Habari wakuu

Hapa job kuna dada mgeni ana kama miezi miwili sasa,Na ofisi yetu ina watu wengi sana hasa wa jinsia ya kiume so tangu afike ni vita kila mmoja anataka amnase.

Sasa kwa records mpaka sasa hakuna yeyote ambae inaonekana kashafanikisha na huyu dada kihulka ni mtu mcheshi anaongea na kucheka na mtu yeyote yule.

So baada ya kuvutiwa nae pia mimi nimejitokeza kuwania saini yake na juzi alinipa namba yake ya simu na tukaanza kuchati.

Ila nlichogundua ni kuwa kashatengeneza security mindset kali sana kiasi kwamba sioni mbinu mbadala za kumpata.

Nimeona nije kwenu kambini mnipe ujuzi niwawakilishe vema hapa kilingeni maana ushindi wangu utakua ushindi wa hili jukwaa lote.

Nakaribisha mawazo na mbinu za kuweza kushinda vita kama hii.
Kwa hiyo mindset yako kuwa humwezi basi ujue ushashindwa mapema
 
Hapana najua ila hii case ndo inahitaji mbinu za ziada
Sawa, basi anza kuwa na ukaribu nae.
Pia hakikisha unafahamu nini huyo mwali anapendelea.
Onyesha kumjali, na msikilize zaidi anapo kua anaongea.
Usionyeshe tamaa na haraka ya kumkula.
Mkaribishe dinner na mitoko ya jioni.
 
Mpotezee, usichat nae, mpe salamu tu inamtosha. usiwe na shobo nae..mfanye kama sio chochote...mfanye kama mtu wa daraja la chini kwako asie na hadhi ya daraja lako. Huku kwa mbali ukichungulia hao madume wenzio wanavyopigana vikumbo kumpa tongozo.

Uzinzi ni mlango wa kufisha nguvu za asilia za mwanadamu.
Mkuu mi nimekuelewa hapo mwisho unaweza kunidadavulia kivipi kuhusu uzinz unavyomaliza nguvu.
 
Mkuu mi nimekuelewa hapo mwisho unaweza kunidadavulia kivipi kuhusu uzinz unavyomaliza nguvu.

Kuna milango miwili ya kuiteka na kuiangamiza nafsi ya mtu.(Mwanaume), Kwanza ni tumbo lake kwa kupitia chakula na pili ni kwa kiungo chake cha uzazi. Unapofanya uzinzi unafungua ulimwengu mwingine. Hapo kunakuwa na roho tofauti za uumbaji na maangamizi. Unapoingia ndani ya mwanamke unafungua ufahamu wa kiroho, kukosa misingi na maarifa ya kukuongoza utajikuta una surrender kila kilicho chako kwa huyo mwanamke, na kama haitoshi utajikuta unatoka na laana na mikosi kwa huyo mwanamke.

Kuna sex rituals watu wanavuta nyota kwa kutumia tendo hili la uzinzi. Hii ipo sana, hata ukipewa threesome kiroho safi fikiria mara mbili, ukiona kuna mshikaji anataka mfanye ku share mwanamke mmoja kwa kupenda kiroho safi yafaa ufikirie mara mbili,
 
Kwanza kuwa tofaut na hao wenzako wakat wenzako wanamtongoza kwa pupa we kuwa cool, usiongee nae mambo ya kumtaka kabisa alaf hata Kama una namba yake usichat nae mara kwa Mara yan akuone haumshobokei kama wengne,,, ila hakikisha huachi kuwasiliana nae kwa muda mref kama anaweka status WhatsApp siku moja unamsifia ila siyo kila siku,,,, baada ya muda ukishaona wale wenye shobo wameangukia pua sasa ww anza harakat taratibu sana usikurupuke,,,
Wasipoangukia pua?
 
Back
Top Bottom