Naishi na njiwa

Naishi na njiwa

ndege JOHN

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2015
Posts
23,621
Reaction score
56,936
Nilikuwa na hamasa sana ya kuanza ufugaji wa wanyama mbalimbali kama kuku, sungura, mbwa, paka, njiwa, na bata. Kwa hiyo, kama sehemu ya mwanzo wa safari hiyo, niliamua kununua njiwa sita. Niliwaleta nyumbani kwangu nikiwa na nia ya kuwafuga kwa ajili ya urembo tu, si kwa biashara wala kwa chakula.

Hata hivyo, sikuwatengenezea mazingira rasmi ya banda au makazi yao maalum. Walikuwa wanashinda juu ya bati na kwenye dari. Mwanzoni, nilikuwa nawapa mtama kama chakula chao, lakini baada ya muda, niliachana na shughuli zote za ufugaji kwa sababu msimamizi wangu aliondoka. Nikaamua kuuza mifugo wote niliokuwa nao, isipokuwa njiwa. Kuwaondoa njiwa ilikuwa ngumu sana kwa sababu ni wepesi na walishazoea kuishi juu ya dari – kuwakamata ilikuwa haiwezekani.

Kilichonifanya niwaache ni kwa sababu hata siwapendi kwa ajili ya chakula; sijawahi kula njiwa hata mara moja. Nilikuwa tu na wazo la kuwaweka kama sehemu ya mandhari na urembo wa nyumba. Lakini tatizo kubwa lilikuja baadaye – wameendelea kuzaana. Sasa wameongezeka na kufikia karibu ishirini. Wanachafua sana mazingira ya nyumba, wanakojoa na kunya kila sehemu – ukutani, kwenye vitu – japokuwa cha kushangaza ni kwamba kinyesi chao hakitoi harufu kali. Wanachafua tu.

Nimejaribu njia mbalimbali ili wahame kama kutowapa chakula wala maji – lakini wamegoma kuhama. Nyumba yangu ipo mbali, imejitenga, kwa hiyo hawana sehemu nyingine ya kwenda. Kwa ratiba yangu ya maisha, natoka asubuhi na kurudi usiku, na naishi mwenyewe, hivo sina nafasi wala muda wa kuwashughulikia.

Nimeamua kuwaacha hivyo hivyo. Labda niwalete kama walinzi wa anga – maana hawasumbui zaidi ya uchafu tu.
 
Ukibahatika kuwakamata wawili watatu ukiwachinja hadharani wenzao wakiona au ukitafuta mchepuko umlete hapo halafu mgombane mzozane zozane hawakai watahama.

Njiwa hawapendi nyumba yenye migogoro pia hawapendi kushuhudia sehemu wanayoliwa liwa..
 
Ukiona mtu kavuka miaka 21 alafu anafuga njiwa ujue kichwani kuna nyaya zimechubuka alafu zinagusana
Mkuu mimi njiwa nilifuga utotoni kweli wakafika kama 84 wakanishinda kuwajengea mabanda hivyo walizidi kuzaliana sana. Makadirio walifika hadi 140 au zaidi. Nilikuwa siuzi labda kugawa tu.

Basi nikamaliza form 4 nikaenda pwani
Kisarawe Kwa miaka2 niliporudi sikukuta njiwa hata1 ila mabanda tu nikashasafisha kwa kuondoa kinyesi na viota vyao kisha nikaendelea na shughuli zangu siku moja walikuja njiwa3
Baada ya siku wakaenda wakarudi na njiwa wengine5 wakafika idadi ya njiwa8 hivyohivyo walizidi kuongezeka hadi idadi ikawa 22 badae wakaanza kuzaliana.

Nikatoka nyumbani tena na kwenda mahali pengine nao hawakubaki.....


Mungu ni mkubwa bana kanijaria nikawa na kwangu kuna siku naamka tu naona njia wawili wapo kwangu nikaingia ndani nikachukua karanga tena zilikuwa kwa ajiri ya lishe ya watoto nikawapa.

Kila siku wakawa wanakuja wanaondoka

Mwisho wakaja kundi kubwa kama njiwa 13 hivi.

Walienda njiwa 5 wa8 wakabaki kwenye kenchi za jiko wakalala hapo hadi siku3 ndo nikakumbuka tangu utotoni mimi na njiwa hatuachani.

Nikatengeneza mabanda mimi mwenyewe hadi sasa wapo 20 na usher na wanazaliana kwa speed sana.


Je hapo kuna shida gani kwenye kichwa chagu? Siwali siwauzii wapo tu kwa starehe zao na kuna baadhi ya njiwa wanakuja kushinda kwangu nakuondoka.

Natazamia wafike 200 kabisa. Pia nikiwa Pwani kuna mwarabu alikuwa nao njiwa wazuri kwelikweli makubwa yanavutia.
 
Back
Top Bottom