Naionya China, isijaribu

Naionya China, isijaribu

Akilihuru

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2022
Posts
1,522
Reaction score
3,039
Hamjambo wakuu.

Ndugu wana Jamii Forum baada ya kufuatilia kile kinachoendelea kutokea kule katika mpaka wa kisiwa cha Taiwan, kuhusu mzozo wa China na Taiwan.

Kama ningekuwa na uwezo wa kuwasiliana na uongozi wa China, basi ushauri wangu mkubwa kwao ingekuwa ni kuwaambia wasithubutu kukivamia kisiwa kile.

Ule ni mtego uliotegwa na hawa wababe wa dunia wakiongozwa na baba lao USA.

Ikumbukwe kwamba hata vita ya Ukraine na Russia ilianza hivi hivi, huku Russia ikiwa na uhakika wa kuisambaratisha Ukraine kwa muda wa siku 3 tu au ikichelewa sana ni week. Sasa kinachoendelea leo kila mtu anakiona.

Russia imekuwa ikitumia kila aina ya njia za kijeshi, rasilimali, na jeshi lake la akiba kuimaliza vita hiyo lkn inashindikana.

Leo hii Russia ishatumia kiasi kikubwa cha silaha zake, ishapoteza kiasi kikubwa cha wanajeshi wake, ishayumbisha uchumi wake na kushuka thamani kwa hela yake (na hili ndio USA na nchi zingine za NATO walilitaka) bila kufanikiwa kuiangusha Serikali ya Ukraine wala kuuteka mji mkuu.

Kile kinachoendelea sasa hivi kimetokana na uzembe wa Putin na serikali yake, sasa wanaona yamekuwa magumu kwao, zile siku 3 ikawa week, ile week ikawa mwezi, mwezi sasa imekuwa miezi.

Na kila wanavyoendelea na vita na ndio jinsi wanavyoendelea kupata hasara kwa kupoteza askari, silaha mbalimbali za kijeshi na kudhoofisha uchumi wao.

Na wamarekani wakishirikiana na ndugu zao wa West wataendelea kuijambisha Russia kwa kujifanya wanaitumia Ukraine silaha (japo nyingi ni za kichovu) ili kuichochea Russia izidi kuendeleza mashambulizi na kudhoofisha nguvu zake kwa miaka kadhaa ijayo.

Ni nani kati ya wana NATO asiejua madhara ya kuingia vitani mzimamzima. Leo hii marekani haiwezi kuthubutu kuingia vitani hata na Mexico, japo kijeshi inaweza kutumia hata jeshi lake lililo katika jimbo la California tu kuisambaratisha Mexico, lakn wanaangalia hasara ambayo inaweza kuipata katika vita hiyo.

Marekani inaweza kutuma silaha au vijana wake kadhaa wa jeshi kwenda kusaidia sehem fulan kwa ajili ya masilahi ya marekani ila haiwezi kuingia vitani moja kwa moja kama ilivyofanya Russia.

Ni mara ngapi Iran imekuwa ikiangamiza ndege zisizo na rubani za Marekani, kuzilipua meli za Marekani na pengine kuteka hata meli za washirika hao wa Marekani, lakn kamwe Marekani haikufikiria na haifikirii kuingia vitani, maana inaelewa kuwa vita kuianza ni vyepesi sana lakin kuimaliza ni vigumu.

Sasa inashangaza kuona China pamoja na kuwa na wasomi wengi pamoja na intelejensi kubwa duniani, lakin inataka kuingia mtegoni kama alivyoingia ndugu yake Russia. USA na swaiba zake wana uwezo wa kutoa msaada kwa Taiwan au Ukraine kwa miaka kumi ili mradi lengo lao litimie.
Marekani na swaiba zake sio wajinga, wanajua vizuri kile wanachokifanya.

Na majibu kuhusu uchumi wa Russia na nguvu zake za kijeshi tutayapata baadae baada ya vita kuisha. Kwa sasa bado inachochewa chochewa ili iweze kutumia hata zile silaha ambazo ingetakiwa kutumia pale inapopambana na nchi kubwa kama USA, China, India nk.
Mwisho wa siku ghala la silaha litabaki tupu.

So naionya China kama inataka kuendelea kuwa nchi ya pili kwa uchumi na ya tatu kwa nguvu za kijeshi, basi iachane na wazo la kuivamia Taiwan maana itapoteza nafasi zake zote mbili, kuanzia kwenye uchumi hadi jeshi. Vikwazo itakavyowekewa na wakubwa hao wa dunia vitakuwa sio vya dunia hii, na hapo ndipo atakapoanza kuona madhara ya kuingia vitani kichwa kichwa bila kutumia akili.
 
Taiwan inabakwa mda wowote
Screenshot_20220805-155520.jpg
 
Kuna watu wana mahaba Niue humu,wanajifariji kwamba urusi haiathiriki chochote kutokana na hii anayoiita special epereshen,hawajiulizi hata swali la kawaida tu kwamba marekani pamoja na nguvu zake zote alizonanazo, uchumi imara, silaha kibao, mbona hajawai kuingia vitani peke yake mpaka aombe kolabo ya washirika wake?? .., hakuna kitu kinafilisi uchumi kama vita!
 
Kwa upande wa Russia

1. Alivyomega Crimea sio mabeberu walifurahia, waliruhusu aimege kisha wakalaani kinafki, media zikafunguliwa kumsifia Putin ni mbabe. Asichokijua ni kwamba, walikuwa wanamjaza ili baadae aingie na Ukraine. Hatimae kajaa kweli Ukraine, anatamani kutoka ila akitazama anaona ni aibu nzito kwake.

2. Leo watu wanasifia Russia kuchukua majimbo, wanasahau kuwa mwezi wa 3 au wa 4 nchi za Magharibi zimepanga kutoa bajeti ya vita hii kwa muda wa miaka 5.

3. US akasema kuwa nia yake kule Ukraine ni kutaka Russia atumie muda mwingi ktk hii Vita. Tumesahau hii kauli ya Biden?

HITIMISHO

Russia atachukua miji na vijiji lakini baada ya muda Ukraine itavikomboa tena. Rejea Ukraine alivyoikomboa Kharkiv, Snake Island na sasa Kherson inakaribia kukombolewa.

Hii yote ni kumchosha Russia. Hata hizi kelele Ulaya wanazopiga mfumuko wa bei, kwao wanajua ni kipindi cha muda tu, tayari walishajipanga kukabiliana na Russia.

CHINA V TAIWAN.

Moja ya vitu nisivyovifikiria ni China kuingia Vitani, China ana majirani ambao akiingia Taiwan na akadhoofika kwa namna yoyote ile, basi muda huohuo India na Japan wanaweza nao wakawasha moto hapo China.

India na Japan hawa wana uwezo kabisa wa kuikalisha serikali ya China totally. Hizi nchi mbili teknolojia zao ktk silaha zao za kivita ni nzuri kuliko mchina.

Mziki wa India na Japan sio wa kitoto.
 
Kuna watu wana mahaba Niue humu,wanajifariji kwamba urusi haiathiriki chochote kutokana na hii anayoiita special epereshen,hawajiulizi hata swali la kawaida tu kwamba marekani pamoja na nguvu zake zote alizonanazo, uchumi imara, silaha kibao, mbona hajawai kuingia vitani peke yake mpaka aombe kolabo ya washirika wake?? .., hakuna kitu kinafilisi uchumi kama vita!
Una hoja nzuri.

Wengi wanaona US akiingia vitani na washirika wanahisi US ni weak. Wanashindwa kutambua jamaa anatazama unafuu wa kupambana ktk vita.

Ni mjinga pekee anayedhani Uchumi wa Russia bado uko imara kutokana na vikwazo alivyowekewa. Kila siku nasemaga humu ndani, laiti vyombo vya habari huko Russia vingefunguliwa na kuwa huru kama Ulaya, basi tungesikia mengi zaidi huko Urusi.
 
Huu mzozo urusi kauvagaa kwa pupa na kudhania mambo mepesi tu. Tena bora urusi ana resource za muhim ambazo wengine hawana hivo inakuwa ngumu kumpiga sanction akaisha. Chinq akilogwa auvagae huu muziki atapigwa sanction mpaka achakae na soko lake kubwa lipo US na Uerope bidhaa anauza za viwandani ambazo zinakuwa na mbadala muda wowote.
 
Nipunga sesemoja lililojijaza likajaa nakujihis lenyewe kitu chamaana.

Tuendelee kutumia condom vijana, mitoto kma hii nihasara kwa nchi
Hivi moderators inakuaje mnaruhusu jukwaa huru kama hili linalosomwa na watu mbali mbali wenye akili timamu, elimu ya kutosha na hata viongozi mbali mbali wa nchi linavamiwa na wendaazimu kama huyu alieleta matusi kwenye uzi huu?
Najua lengo lake mimi nimjibu ili niuchafue uzi wangu na hatimae nipewe ban ya lazima. So pliz moderators fanyeni kazi yenu, huyu hafai kuendelea humu JF.
 
Kuna watu wana mahaba Niue humu,wanajifariji kwamba urusi haiathiriki chochote kutokana na hii anayoiita special epereshen,hawajiulizi hata swali la kawaida tu kwamba marekani pamoja na nguvu zake zote alizonanazo, uchumi imara, silaha kibao, mbona hajawai kuingia vitani peke yake mpaka aombe kolabo ya washirika wake?? .., hakuna kitu kinafilisi uchumi kama vita!
Russia ishaathirika kwa kiwango kikubwa sana, ila ndo hivyo katika mbinu za kivita hauwezi kuelezea hasara unayopata kupitia kichapo cha adui.
 
Kwa upande wa Russia

1. Alivyomega Crimea sio mabeberu walifurahia, waliruhusu aimege kisha wakalaani kinafki, media zikafunguliwa kumsifia Putin ni mbabe. Asichokijua ni kwamba, walikuwa wanamjaza ili baadae aingie na Ukraine. Hatimae kajaa kweli Ukraine, anatamani kutoka ila akitazama anaona ni aibu nzito kwake.

2. Leo watu wanasifia Russia kuchukua majimbo, wanasahau kuwa mwezi wa 3 au wa 4 nchi za Magharibi zimepanga kutoa bajeti ya vita hii kwa muda wa miaka 5.

3. US akasema kuwa nia yake kule Ukraine ni kutaka Russia atumie muda mwingi ktk hii Vita. Tumesahau hii kauli ya Biden?

HITIMISHO

Russia atachukua miji na vijiji lakini baada ya muda Ukraine itavikomboa tena. Rejea Ukraine alivyoikomboa Kharkiv, Snake Island na sasa Kherson inakaribia kukombolewa.

Hii yote ni kumchosha Russia. Hata hizi kelele Ulaya wanazopiga mfumuko wa bei, kwao wanajua ni kipindi cha muda tu, tayari walishajipanga kukabiliana na Russia.

CHINA V TAIWAN.

Moja ya vitu nisivyovifikiria ni China kuingia Vitani, China ana majirani ambao akiingia Taiwan na akadhoofika kwa namna yoyote ile, basi muda huohuo India na Japan wanaweza nao wakawasha moto hapo China.

India na Japan hawa wana uwezo kabisa wa kuikalisha serikali ya China totally. Hizi nchi mbili teknolojia zao ktk silaha zao za kivita ni nzuri kuliko mchina.

Mziki wa India na Japan sio wa kitoto.
Rassia inapata hasara kubwa sana kijeshi, hapo hatujazungumzia vikwazo vya kiuchumi.

Baada ya miaka mitatu ya mbele Russia itakuwa nyuma hata ya Saudia Arabia kijeshi na kiuchumi.
 
Back
Top Bottom