Naiona Nchi ikipasuka vipande vipande

Naiona Nchi ikipasuka vipande vipande

Domokaya naona umeanza ngonjera na mapambio ova tupo kwenye kampeni

vyovyote vile, dawa imeingia, hayo ni maumivu ya kutobolewa na sindano tu, kupona lazima, taka usitake, upole unahusu!
 
Mkuu, suala la Machinga kujimwaga K,koo mabarabarani na Kule Mwanza ni suala la kisiasa tu, time will tell. Watu wanataka kuona japo Foundation ya kiwanda kimoja Kati ya vilivyoahidiwa, Siku zinaenda, suala la Madawa na watuhumiwa sioni Faida zake moja kwa moja kwa wananchi. Naona Kama mnawatoa wananchi ktk Mstari, yaani mnahamisha magoli.

We si ndio ufurahi sasa ahadi hazitimizwi ili wananchi wasiwachague wale tena, mbona sasa badala ya kufurahia na kukaa kimya ili uje kuua kirahisi unapigapiga kelele? Au huna hakika na usemalo? Kwni wewe shida yako nini?
 
c
Bro, Hakuna sheria ktk hii Nchi inayomlazimisha mtu kuwa mfuasi wa Vyama, ila Msema kweli ni mpenzi Mungu, hii Nchi ni Mali yetu Sote, sasa Ukijiona ww ni Zaidi yetu lazima tukushushe, huwezi kudharau unaowaongoza halafu ukatarajia kubaki salama!

Utamshusha nani mtu mwenyewe muoga kama mimi. Ikiwa jina lako tu unalificha humu jf wewe utamshusha nani? Utamshusha mtu kwa kutype tu tena ukiwa umejificha hata mtu akikusogelea unaficha unacho andika, acha hizo story za kujidanganya
 
Ofcoz mm ni mwanaCCM damu na wengi mnanijua hapa ndani,but automatically nimejikuta nikimchukia Makonda na Rais wake Maguguri.
Maana kama ameweza kutoa sauti ya kitisho kumuita mh MBOWE na wafanya biashara wakubwa tena wenye brand kubwa vipi kapuku mimi?
Nilimpigia debe kwenye ukuu wa mkoa baada ya kuona kazi nzr kinondoni.
But kwa ubabe huu nikisikia kafa ntapika biliani kisha ntalisha mbwa wangu.
Mh Rais afanye mabadiliko ya haraka ili kuinusuru Dar yetu.
 
Haihitaji akili nyingi sana kujua hili, ni wazi na ni dhahiri kabisa kuwa hali ya Nchi ni mbaya sana kwa sasa, kitendo cha Wabunge wote wa CCM na wa vyama vyote vya upinzani kuunga hoja Mkono kwa asilimia 100 ya kwamba Mh Makonda Aitwe na kwenda kujitetea Ktk kamati ya maadili bungeni wakati huo huo Akiwa anaungwa Mkono na kusifiwa sana na Raisi ni Dhahiri kuwa wabunge wote hawamuungi Mkono Raisi.

Kwa mitaani hali ni mbaya Zaidi, kila mtu anamzungumzia Makonda kwa Ubaya, siyo Maprofesa siyo Madoctor siyo Machinga, Wasanii ndiyo Kabisa usiseme. Hasa ukizingatia ile Amri yake ya kuzuia Shughuli zote za Burundani kuanzia Saa sita usiku. Amri ambayo imewafanya Wasanii wengi kukosa kazi ya kufanya kwa sababu Hakuna ukumbi unaokubali kuwaalika Wasanii kutumbuiza kwa masaa mawili tu hatafu walipwe, kwa hiyo wengi Kama siyo wote hawana kazi ya kufanya na hali zao ni mbaya sana kifedha.

Wahudumu wa Bar, Kama Watanzania masikini nao pia wana kilio kikali na Wanaongea kila lililo baya kwa Mkuu huyu wa Mkoa, sababu, bar zote zimepunguza wahudumu kwa zaidi ya 80% hii ni kwa sababu wale waliokuwa wakiingia Shift za asubuhi, wote wamepoteza kazi outomatic, na wale wa shift ya usiku wamepunguzwa kwa 50%. Jaribu kuona ni familia ngapi zimeathirika,

Wamiliki wa Mabaa na Maclabu, kila mtu analaani kwa Lugha yake, sababu, masaa ya kufanya kazi ni machache sana, hivyo kufanya Mapato Yao kushuka kwa Zaidi ya 60% bajaji boda boda, na Tax ndiyo balaa, wao walikuwa wakipata abiria kuanzia Asubuhi mpaka usiku saa kumi, sasa hivi wanalazimika kufunga shughuli zao saa sita usiku na kuzifungua saa kumi jioni, Muda mwingi wanautumia kucheza Drafti na kupiga soga zisizo na faida yoyote. Mapato Yao yameshuka kwa zaidi ya 65%

Kutokana na pia Hali za watu za uchumi kuwa mbaya sana, watu wamekuwa na Hasira na Chuki Sana, kuna mpasuko mkubwa sana wa kiuongozi, Wenyeviti wa Serikali za mitaa kila Mmoja analaani kwa Lugha yake.

Je, tutaachana Vipi na hii hali halisi iliyopo ambapo kila Mtu amepoteza Matumaini, Wakati wa Kampeni Wagombea waliahidi kuwa awamu hii itakiwa ni TANZANIA YA VIWANDA. Juzi Waziri wa viwanda amewachana wananchi wazi kuwa, Serikali haina uwezo wa kujenga viwanda ila itaandaa mazingira ya wanachi kujijengea Viwanda. Japo hakufafanua, ila kwa wenye akili timamu tumejua imetoka hiyo!

Wanasiasa wanakamatwa na kufungwa hovyo, yaani ni Chuki kila mahali. Watu wamekosa Furaha kabisa ktk Nchi Yao, ni hofu na mashaka tele., Tujipange Upya, tuone tunapokosea tuparekebishe haraka, vinginevyo siyo Muda mrefu tunaweza kujikuta tukigawana madirisha na mabati wakati nyumba ni Mali yetu wenyewe

Yote haya ni kwa sababu ya uongozi wa hovyo wa jk na genge lake. Hat kama wamekufa, waliomweka madarakani huyu mharabu, lawama zitawafuata kwa yote yaliyotendeka kwa ridhaa yake, na yanaoyfanywa na aliyowapachika kwa nguvu zake hata kama hawafai.
 
Yaani yote niliyoandika umeona neno bar tu!Nakukumbusha tu, Nchi haiendeshwi Kwa Mihemko, na Viburi. Kwani hujui kwamba nchi nyingi zimejikuta ktk Vita baada ya haki Kupuuzwa?. Je ww uchambuzi wako unasemaje!

Wewe umeshawahi uendesha nchi gani ukajua kuwa nchi haiendeshwi kwa kihemuko na viburi? Au umeishi nchigani hiyoambao viongozi wake hawana kiburi, itaje hapa kila mtu aichunguze ili tuhakikishe kama usemalo kweli au wewe tu unaendeshwa na hisia badala ya ukweli. Nchi lazima iendeshwe kwa mihemuko na kiburi, hayo mengine ni story tu za kijiweni.
 
Kwa hiyo unataka kusema uchumi wa Tanzania unategemea madawa ya kulevya?
 
Akili za watu wa chadema zina matatizo.wote humu siku ya kwanza walipotajwa wasanii,mkiongozwa na lissu mkasema anakamata dagaa.Kuitwa mwenyekiti wenu tu tena kwa maongezi,zoezi zima mnasema ni batili na halifai.
Kwa akili ya makonda,hizi thread zote zinamzidishia nguvu na ujasiri,na kesho jumapili Rais anatarajiwa kupigilia msumari wa moto
Kweli ninaanza kuamini kazi ya kichwa ni kufugia nywele
 
Ofcoz mm ni mwanaCCM damu na wengi mnanijua hapa ndani,but automatically nimejikuta nikimchukia Makonda na Rais wake Maguguri.
Maana kama ameweza kutoa sauti ya kitisho kumuita mh MBOWE na wafanya biashara wakubwa tena wenye brand kubwa vipi kapuku mimi?
Nilimpigia debe kwenye ukuu wa mkoa baada ya kuona kazi nzr kinondoni.
But kwa ubabe huu nikisikia kafa ntapika biliani kisha ntalisha mbwa wangu.
Mh Rais afanye mabadiliko ya haraka ili kuinusuru Dar yetu.

Mtu anayepika biriani kulisha mbwa huyo walahutakiwi kuuliza kazi yake au biashara yake hivyo ni wazi hawezi kumpenda Makonda wala JPM. Anaweza asiwe anajua alichoandika kwa sababu ya hasira. lakini anaweza kuwa amesema jambo kubwa sana kumuhusu.
 
Haihitaji akili nyingi sana kujua hili, ni wazi na ni dhahiri kabisa kuwa hali ya Nchi ni mbaya sana kwa sasa, kitendo cha Wabunge wote wa CCM na wa vyama vyote vya upinzani kuunga hoja Mkono kwa asilimia 100 ya kwamba Mh Makonda Aitwe na kwenda kujitetea Ktk kamati ya maadili bungeni wakati huo huo Akiwa anaungwa Mkono na kusifiwa sana na Raisi ni Dhahiri kuwa wabunge wote hawamuungi Mkono Raisi.

Kwa mitaani hali ni mbaya Zaidi, kila mtu anamzungumzia Makonda kwa Ubaya, siyo Maprofesa siyo Madoctor siyo Machinga, Wasanii ndiyo Kabisa usiseme. Hasa ukizingatia ile Amri yake ya kuzuia Shughuli zote za Burundani kuanzia Saa sita usiku. Amri ambayo imewafanya Wasanii wengi kukosa kazi ya kufanya kwa sababu Hakuna ukumbi unaokubali kuwaalika Wasanii kutumbuiza kwa masaa mawili tu hatafu walipwe, kwa hiyo wengi Kama siyo wote hawana kazi ya kufanya na hali zao ni mbaya sana kifedha.

Wahudumu wa Bar, Kama Watanzania masikini nao pia wana kilio kikali na Wanaongea kila lililo baya kwa Mkuu huyu wa Mkoa, sababu, bar zote zimepunguza wahudumu kwa zaidi ya 80% hii ni kwa sababu wale waliokuwa wakiingia Shift za asubuhi, wote wamepoteza kazi outomatic, na wale wa shift ya usiku wamepunguzwa kwa 50%. Jaribu kuona ni familia ngapi zimeathirika,

Wamiliki wa Mabaa na Maclabu, kila mtu analaani kwa Lugha yake, sababu, masaa ya kufanya kazi ni machache sana, hivyo kufanya Mapato Yao kushuka kwa Zaidi ya 60% bajaji boda boda, na Tax ndiyo balaa, wao walikuwa wakipata abiria kuanzia Asubuhi mpaka usiku saa kumi, sasa hivi wanalazimika kufunga shughuli zao saa sita usiku na kuzifungua saa kumi jioni, Muda mwingi wanautumia kucheza Drafti na kupiga soga zisizo na faida yoyote. Mapato Yao yameshuka kwa zaidi ya 65%

Kutokana na pia Hali za watu za uchumi kuwa mbaya sana, watu wamekuwa na Hasira na Chuki Sana, kuna mpasuko mkubwa sana wa kiuongozi, Wenyeviti wa Serikali za mitaa kila Mmoja analaani kwa Lugha yake.

Je, tutaachana Vipi na hii hali halisi iliyopo ambapo kila Mtu amepoteza Matumaini, Wakati wa Kampeni Wagombea waliahidi kuwa awamu hii itakiwa ni TANZANIA YA VIWANDA. Juzi Waziri wa viwanda amewachana wananchi wazi kuwa, Serikali haina uwezo wa kujenga viwanda ila itaandaa mazingira ya wanachi kujijengea Viwanda. Japo hakufafanua, ila kwa wenye akili timamu tumejua imetoka hiyo!

Wanasiasa wanakamatwa na kufungwa hovyo, yaani ni Chuki kila mahali. Watu wamekosa Furaha kabisa ktk Nchi Yao, ni hofu na mashaka tele., Tujipange Upya, tuone tunapokosea tuparekebishe haraka, vinginevyo siyo Muda mrefu tunaweza kujikuta tukigawana madirisha na mabati wakati nyumba ni Mali yetu wenyewe
Wenye akili zetu hali hii tulionana tangu siku yule babu aliposimama na kutangaza matokeo. Jinsi nchi ilivyozizima tu tukajua hapa ni kulia tu na kusaga meno. Hata hivyo haujachelewa kwa kukiona hilo leo
 
Akili za watu wa chadema zina matatizo.wote humu siku ya kwanza walipotajwa wasanii,mkiongozwa na lissu mkasema anakamata dagaa.Kuitwa mwenyekiti wenu tu tena kwa maongezi,zoezi zima mnasema ni batili na halifai.
Kwa akili ya makonda,hizi thread zote zinamzidishia nguvu na ujasiri,na kesho jumapili Rais anatarajiwa kupigilia msumari wa moto
chezea akili za nyumbu !!
 
Ukiwa kiongozi ni lazima utafakari sana Juu ya amri unazozitoa, nyingine zina impact kubwa sana kwa jamii.
Kweli mkuu,na hilo ndilo analolikosa Makonda,hatafakari amri zake zitakuwa na sukumo gani katika jamii
 
Isha pasuka wachache wajinga hawajui eti
Kitendo cha Wabunge wote wa Ccm kumchukia mteule wa Raisi tena hadharani bila chenga, ni ishara tosha kuwa hawako pamoja na yeye, wakimkosa kosa mkuu wa mkoa wanaweza kulala naye mbele. Yangu macho.
 
Inaonyesha upeo wako wa kufikiri na kuchambua mambo kwa weledi ni mdogo sana!vita ni vita!kila vita inambinu zake!nchi haiwezi kupasuliwa kirahisi hivyo kama ambavyo unataka kutuaminisha!tulia dawa iingie taratibu....tunarejeshwa kwenye mstari
Mkuu tunarejeshwa kwenye mstari kwa kuwahusisha watu na madaya ya kulevya bila kuwa na ushahidi wa uhakika?! Bro shirikisha ubongo wako vizuri
 
Akili za watu wa chadema zina matatizo.wote humu siku ya kwanza walipotajwa wasanii,mkiongozwa na lissu mkasema anakamata dagaa.Kuitwa mwenyekiti wenu tu tena kwa maongezi,zoezi zima mnasema ni batili na halifai.
Kwa akili ya makonda,hizi thread zote zinamzidishia nguvu na ujasiri,na kesho jumapili Rais anatarajiwa kupigilia msumari wa moto
images-1316.jpeg
images-1316.jpeg
 
Makonda kuwa rc dar ni saw a na kumtwisha gunia la Michele mtoto wa miaka 6, lazima aanguke nalo
Yaani ...................
2016-10-12-09-00-53-1415863435.jpeg

Au
images-371.jpeg

images-385.jpeg

Tukiwaambia 'NO' watumie njia sahihi wenyewe wang'ang'ania kusema wa sahihi,wasema tusubirie kuona matokea positive.Dah!!!maskini wanakatisha tamaa.
 
Cheki baadhi ya watanzania walivomashabiki watakuambia "MADEREVA" anatemda kazi kisawa sawa.
Nakwambia sijui tunaumwa ugonjwa gani sie.
Mtukufu mkubwa kabisa alikwenda Bukoba akawatukana matusi ya nguoni na bado wakashangilia kwa nguvu! ninataka kuthibitisha hoja yako ya waTz tuna ugonjwa ambao hakuna mtaalamu anayeweza kueleza ni nini.
 
Back
Top Bottom