Naibu Waziri: Marufuku Runinga za Hospitali kuonyesha tamthilia, michezo na burudani kama ilivyozoeleka

Naibu waziri wa Afya, maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dk Faustine Ndugulile amewataka waganga wakuu wa mikoa yote nchini kuanza kutekeleza maelekezo ya Serikali yanayoagiza runinga zote zilizofungwa kwenye hospitali za umma kurusha matangazo yanayohusu elimu ya afya peke yake.

Dk Ndugulile ametoa agizo hilo wakati alipotembelea na kukagua changamoto zinazowakabili wagonjwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma ambapo amesema lengo la Serikali kuweka runinga hizo ni kutoa elimu ya afya na si tamthilia michezo na burudani kama ilivyozoeleka.View attachment 994197 Chanzo: ITV Channel

Sent using Jamii Forums mobile app

Angesema madhara ya kuangalia izo chanel za burudani kwa wagonjwa ni zipi?
 
Nicheke tu
Mie, waanzishe basi afya tv iwe kwenye vinamuzi vya startimes au
Azam ili zionekane huko mahospitalin. Sasa unapiga marufuku bila suluhisho mbadala? Hosp wana weza
Kuratibu hili
Vipi ilihali wanategemea vingamuzi? Kuna haja haawa mawaziri baadhi kupimwa ubongo wao.
 
Hata tukisema kuwa sawa waangalie vipindi vya Afya tu, ni kituo gani cha luninga kitarusha matangazo ya Afya tuuu masaa 24. Na huyo naibu waziri awaagize watoto wake waangalie hivyo vipindi hapo nyumbani kwake kama hatakuta TV imevunjwa vunjwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siku akilazwa hata kama Miezi miwili hivi ataelewa kwanini wanaonyesha Tamthilia.

Atajua kuwa MunGu sio John
 
Hehhh. Ununifu wa hali ya juu sana. Eti huyu ni daktari wa mitishamba au ni wa PhD. Maana akili PhD holders Tanzania kwa sasa hasa walioajiriwa serikalini ni sawa na watoto wa shule ya Sinza mahitaji maalum
 
Hivi kuna Afya channel Tz?
Maana sidhani kama kuna channels makhsusi kwa kitu kimoja tu kwetu

Ama kweli safari hii kila kiongozi anazidi kumwagia acid kwenye kidonda.



Sent from my SM using Tapatalk
 
Back
Top Bottom