Naibu Spika Zungu anapolalamika kuwa makampuni ya simu na mabenki yanawatoza wateja pesa nyingi, je anajua gharama za uendeshaji wa makampuni hayo?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,162
Tumemsikia Naibu Spika, Mussa Zungu, akielezea kuhusu tozo zilizolalamikiwa Sana na wananchi, hadi Serikali ikasalimu amri na kuahidi kuzipunguza tozo hizo kuanzia tarehe 1 mwezi ujayo.

Katika maelezo yake alidai eti wananchi wanachujua ni kuilalamikia Serikali kuhusu tozo wanazotoza kwenye miamala hiyo ya simu, lakini wanasahau kuwa makampuni hayo ya simu na mabenki ndiyo yanayotoza kiwango kikubwa zaidi!

Akaendelea kudai kuwa eti tozo tunazolalamikiwa na wananchi ni kwa manufaaa yetu, kwa kuwa ndizo zinazojenga madarasa na vituo vya afya!

Hivi huyu Zungu, anatufanya sisi watanzania wote ni wajinga kiasi hicho, ambacho anaweza kutudanganya atakavyo?

Hivi Hawa CCM wanaopenda kutumia hii propaganda ya kuwa hizo tozo ndizo zinazojenga madarasa na vituo vya afya, nipende tu kuwauliza swali moja, hivi hizi pesa za mikopo ya World Bank na IMF, ambayo tulikuwa tunaambiwa kuwa wamekopa Ili kujengea madarasa na vituo vya afya, pesa hizo zimefanya Kazi gani?

Hawa watawala wetu wanaopenda kutuibibia sisi wananchi wao kwa kupitia hizo tozo, Ili wao waishi Katika Maisha ya kifahari ya kupindukia!

Hivi inawezakanaje wawakilishi wetu ambao ni wabunge, watembelee magari ya anasa Sana ya mavi-eite ya shilingi milioni 400, yakiwa yanagharimikiwa kila kitu na walipa kodi wa nchi hii masikini Sana, halafu asingizie kuwa wanajenga madarasa na vituo vya afya?

Hivi huyu Zungu anawezaje kuilinganisha Serikali na hayo makampuni Katika utozaji wa tozo hizo?

Hivi anajua gharama za makampuni ya simu hapa nchini, ikiwemo kujenga minara, ofisi kwa ajili ya uendeshaji na kuwalipa mishahara wafanyakazi wake, pamoja na kuwalipa kodi mbalimbali kea Serikali hiyo hiyo?

Hivi anawezaje kujilinganisha na makampuni hayo na Serikali, wakati inajulikana wazi kuwa hao Serikali, wanachojua ni kuchukua tozo hizo, wakati hawajawekeza chochote?

Kwa hiyo ni dhahiri huo ni ulafi wa kupitiliza unaowakabili viongozi we serikali hii kandamizi ya CCM, ndiyo unaomfanya huyo Naibu Spika Mussa Zungu, atetee kwa nguvu zote hizo tozo, ambazo zimekataliwa kwa nguvu ya Umma wa wananchi wa nchi hii.

Kifupi tu mwisho wa matozo ya nchi hii, ni kuandika Katiba mpya ya wananchi, itakayoyokana na maoni yetu tuliyoyatoa kupitia kwenye Rasibu ya Warioba.

Mungu ibariki Tanzania
 
Yeye Zungu kama mbunge baada ya kugundua bank wanachukua hela nyingi sana kwa wateja amechukua hatua gani kulinda wateja ambao ni wananchi na wapiga kura? Au yeye bungeni ameenda kutetea tumbo lake?
 
Ko anawivu anataka wale sawa selikal na bank, haina shida cha kufanya sasa wao wakate zaid ya mabank
 
Na wewe ni mmoja wao bila shaka ni mpambe wao makampuni hayo ni yawazungu ukweli ndo huo yanakata mitozo kuliko serikali yani wanataka faida mara 8.
 
Hata kama ikiyaonhezea kodi na kupunguza tozo bado tu mzigo huo ataubeba mwananchi.

Kuna maeneo mengi tu ya kuongeza mapato kuliko kupambana na industry moja tu.

Taifa halisongi mbele kutokana na ubinafsi wa wanasiasa wanaopeana madaraka kwa kulindana badala ya kuangalia tija.

Viongozi waliopo madarakani ni almost wale wale for the past 30 years.

Hawana motivation yeyote ya kudrive nchi kufikia maendeleo tunayoyataka.

Akili zao zimegota. Hawana mawazo mapya ya kutukwamua kiuchumi.

They are selfish and lazy.
 
Na

Na wewe ni mmoja wao bila shaka ni mpambe wao makampuni hayo ni yawazungu ukweli ndo huo yanakata mitozo kuliko serikali yani wanataka faida mara 8
Big Eagle
Hivi wewe unayeona kuwa hayo makampuni ni wezi, umeshawahi kujiuliza, hivi Serikali inayochukua tozo kwenye hayo makampuni, imewekeza nini kwenye hayo makampuni?

Au ndiyo kawaida yenu nyinyi maccm katufanyia wizi wa mchana kweupe?
 
Hata kama ikiyaonhezea kodi na kupunguza tozo bado tu mzigo huo ataubeba mwananchi.

Kuna maeneo mengi tu ya kuongeza mapato kuliko kupambana na industry moja tu.

Taifa halisongi mbele kutokana na ubinafsi wa wanasiasa wanaopeana madaraka kwa kulindana badala ya kuangalia tija.

Viongozi waliopo madarakani ni almost wale wale for the past 30 years.

Hawana motivation yeyote ya kudrive nchi kufikia maendeleo tunayoyataka.

Akili zao zimegota. Hawana mawazo mapya ya kutukwamua kiuchumi.

They are selfish and lazy.
Stroke
Tayari umepiga U turn, kada wa kuaminika wa CCM?

Hongera Sana kada kwa kuutambua ukweli🤝
 
Big Eagle
Hivi wewe unayeona kuwa hayo makampuni ni wezi, umeshawahi kujiuliza, hivi Serikali inayochukua tozo kwenye hayo makampuni, imewekeza nini kwenye hayo makampuni?

Au ndiyo kawaida yenu nyinyi maccm katufanyia wizi wa mchana kweupe?
Kwani naibu spika si serikali? Kunguza kuchelewa kufikiri
 
Tumemsikia Naibu Spika, Mussa Zungu, akielezea kuhusu tozo zilizolalamikiwa Sana na wananchi, hadi Serikali ikasalimu amri na kuahidi kuzipunguza tozo hizo kuanzia tarehe 1 mwezi ujayo.

Katika maelezo yake alidai eti wananchi wanachujua ni kuilalamikia Serikali kuhusu tozo wanazotoza kwenye miamala hiyo ya simu, lakini wanasahau kuwa makampuni hayo ya simu na mabenki ndiyo yanayotoza kiwango kikubwa zaidi!

Akaendelea kudai kuwa eti tozo tunazolalamikiwa na wananchi ni kwa manufaaa yetu, kwa kuwa ndizo zinazojenga madarasa na vituo vya afya!

Hivi huyu Zungu, anatufanya sisi watanzania wote ni wajinga kiasi hicho, ambacho anaweza kutudanganya atakavyo?

Hivi Hawa CCM wanaopenda kutumia hii propaganda ya kuwa hizo tozo ndizo zinazojenga madarasa na vituo vya afya, nipende tu kuwauliza swali moja, hivi hizi pesa za mikopo ya World Bank na IMF, ambayo tulikuwa tunaambiwa kuwa wamekopa Ili kujengea madarasa na vituo vya afya, pesa hizo zimefanya Kazi gani?

Hawa watawala wetu wanaopenda kutuibibia sisi wananchi wao kwa kupitia hizo tozo, Ili wao waishi Katika Maisha ya kifahari ya kupindukia!

Hivi inawezakanaje wawakilishi wetu ambao ni wabunge, watembelee magari ya anasa Sana ya mavi-eite ya shilingi milioni 400, yakiwa yanagharimikiwa kila kitu na walipa kodi wa nchi hii masikini Sana, halafu asingizie kuwa wanajenga madarasa na vituo vya afya?

Hivi huyu Zungu anawezaje kuilinganisha Serikali na hayo makampuni Katika utozaji wa tozo hizo?

Hivi anajua gharama za makampuni ya simu hapa nchini, ikiwemo kujenga minara, ofisi kwa ajili ya uendeshaji na kuwalipa mishahara wafanyakazi wake, pamoja na kuwalipa kodi mbalimbali kea Serikali hiyo hiyo?

Hivi anawezaje kujilinganisha na makampuni hayo na Serikali, wakati inajulikana wazi kuwa hao Serikali, wanachojua ni kuchukua tozo hizo, wakati hawajawekeza chochote?

Kwa hiyo ni dhahiri huo ni ulafi wa kupitiliza unaowakabili viongozi we serikali hii kandamizi ya CCM, ndiyo unaomfanya huyo Naibu Spika Mussa Zungu, atetee kwa nguvu zote hizo tozo, ambazo zimekataliwa kwa nguvu ya Umma wa wananchi wa nchi hii.

Kifupi tu mwisho wa matozo ya nchi hii, ni kuandika Katiba mpya ya wananchi, itakayoyokana na maoni yetu tuliyoyatoa kupitia kwenye Rasibu ya Warioba.

Mungu ibariki Tanzania
Gharama za uendeshaji zinatumika kama kisingizio cha upigaji WA hayo makampuni..
 
Gharama za uendeshaji zinatumika kama kisingizio cha upigaji WA hayo makampuni..
Kwani hujui kuwa na Serikali nayo kututoza tozo kuwa ajili ya kujenga madarasa na vituo vya afya, ilihali hayo madarasa na vituo vya afya, wslijenga kutokana na mikopo ya World Bank na IMF, ndiyo tunapigwa zaidi na Serikali?🥺
 
Hayo makampuni ya simu na mabenki huanzishwa ili mtumiaji akatwe gharama za uendeshaji wake? Nonsense! Tumia hiyo ugali kwa kichwa yako mkuu. Kila mtu apambane kuweka huduma nzuri ili awavutie wateja kwa wingi aweze endesha kampuni/benki y/lake. Hakuna kampuni ya simu inayosubiri mtumiaji anunue line ndo kisha aweke mnara.
 
Kwani hujui kuwa na Serikali nayo kututoza tozo kuwa ajili ya kujenga madarasa na vituo vya afya, ilihali hayo madarasa na vituo vya afya, wslijenga kutokana na mikopo ya World Bank na IMF, ndiyo tunapigwa zaidi na Serikali?🥺
Mnaongeaga kama watu wajinga fulani..

Mara kadhaa mumeelezwa kwamba madarasa ya uviko yalikuwa sekondari na shule za msingi serikali ilimalizia maboma ya vyumba zaidi ya 7,000 kwa tozo lakini hamuelewi..

Mwaka huu walioanza kujenga madarasa 8,000 wakati uhitaji ni zaidi ya 18,000 na wanaotumia sio watoto wa kina Mwigulu maana hawasomi huko kwenye Kata so ukiambiwa changia kwa tozo wewe changia sio ulalamishi usio na msingi..
 
Back
Top Bottom