Dodoma. Naibu Kamishna mstaafu wa Magereza nchini (DCP), Luhusa Chiza (62) amefariki dunia katika mazingira ya utata kwenye hoteli ya Kitemba mjini hapa.
Kwa mujibu wa walioshuhudia tukio hilo, mwili wa Chiza uligunduliwa juzi mchana na mmoja wa wahudumu wa hoteli hiyo alipotaka kufanya usafi.
Taarifa kutoka ndani ya hoteli hiyo iliyopo Barabara ya Sita katikati ya mji wa Dodoma, zilidai Chiza aliingia Novemba 15, usiku na msichana ambaye alitoroka baadaye.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa alisema mwili wa Chiza ulikutwa ukiwa na damu puani na kwamba, aliingia chumbani akiwa na msichana ambaye wanamtafuta.
Kwa mujibu wa walioshuhudia tukio hilo, mwili wa Chiza uligunduliwa juzi mchana na mmoja wa wahudumu wa hoteli hiyo alipotaka kufanya usafi.
Taarifa kutoka ndani ya hoteli hiyo iliyopo Barabara ya Sita katikati ya mji wa Dodoma, zilidai Chiza aliingia Novemba 15, usiku na msichana ambaye alitoroka baadaye.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa alisema mwili wa Chiza ulikutwa ukiwa na damu puani na kwamba, aliingia chumbani akiwa na msichana ambaye wanamtafuta.