Kweli kabisa Bro, nimefail wala Hakuna ubishi, ndio maan nimekuja kwenu mnisaidie kimawazo
Vizuri sana mwanachama sasa ni hivi
1. Punguza starehe fanya mambo ya maendeleo,kumbuka hicho ni kibarua kinaweza kuota nyasi mda wowote ukaadhirika ukaja kuomba kodi hapa.
2. Kumbuka kufanya ibada kila ijumaa na jumapili,muombe Mungu akupe mke mwema(ila sio wa club tena)
3. Tembelea kwenda maeneo tofauti tofauti,umesema uko Rock city nenda hata hapo rock city mall,nenda movie theatre,kwenye maduka humo ndani huwezi jua utakutana na mkeo,nenda beach huko ziwani,kwenye business meetings,seminars,shopping supermarket huko ndio sehem atleast unaweza kukutana na mtu anaeeleweka ila sio club.
4. Fanya savings mapema sio unatumbua tu,kumbuka unataka mwenyewe kujitia kitanzi cha ndoa,hivyo mzigo wa majukumu lazima utaongezeka,utaanza kulisha mtu mmoja zaidi baadae wataongezeka watakuwa wawili,watatu na kuendelea.
5. Ukipata mwanamke mchunguze vizuri(tumia mbinu za kijasusi kidogo) kama je anafaa kuwa mama watoto wako? Huyo angeachia mtoto housegirl au jirani halafu yeye akaenda club.
6. Nimechoka kuandika,fanya hayo kwanza