habari zenu,
mimi binafsi nilianza project hiyo mwaka jana,nlifika pale kituoni kwao mikocheni ,nilitoa order ya miche ya awali kama 1000 hivi,nikaambiwa nisubiri miezi sita itakuwa tayari,nikajipanga na pesa ambapo walisema mche mmoja ni Tshs 3000...nilikuwa nafanya ufuatiliaji wa hapa na pale kwa njia ya simu,baada ya miezi 3 nilienda kuona wamefikia wapi nikaambiwa ile miche iliuzwa(iliuzwaje uzwaje wakati nilitoa order na wakakubali,hawakunipa maelezo yakujitosheleza)...nikaambiwa nisubiri miezi mitatu mingine nikasubiri ,nikapewa miche 125 tu ambayo ilikuwa aina mchanganyiko(mimi nilitaka mzuzu tupu) lakini waliniahidi katika zile aina hakuna bokoboko...nikaichukua nikaipanda,(nilipanda january 2013)...sasa imeshazaaa,imestawi vizuri ila katika miche 125 ,75 ilikuwa bokoboko....na imestawi vizuri,je bokoboko hapa mjini dar namuuzia nani?inatia hasira saaana(nimeifyeka machipukizi yake yote na nikivuna nang'oa hayo mashina yote,sitaki kuiskia bokoboko,hata mimi binafsi tu sili ile ndizi)
Sikuishia hapo,mwaka huo 2013 nilifika sua,nikaongea na professor Msogoya,alinishauri vizuri yule baba...na akaniambia sua hamna tissue culture ila kuna njia fulani wanatumia pale,wanatreat vile viazi(kama kiini flani cha mgomba) wanaua wadudu halafu wanazalishia miche,nikatoa order yangu,nayo ilichukua miezi sita kupata miche 500 tu,(ila safari hii nilipata na yote ilikuwa mzuzu)...nimetoa nyingine ya 500...nachukua ndani ya miezi 3...bei ni ile ile 3000tsh kwa mche!
natarajia kuwa nahamisha machipukizi kutoka yale mashina ya mwanzo mpaka nijaze ekari zangu 10.
kitu kingine nilichojifunza,machipukizi yanakuwa haraka sana kuliko tissue culture plants na hii miche mingine ya kuotesha nayonunua.
Kingine cha kuongeza sua kuna foleni ya miche,toa order yako mapema,na miche inapatikana kwa wingi wakati wa kiangazi,kama una irrigation system nakushauri uchukue wakati huo...wakati kilimo ukianza ni purukushani unaweza usikute mche hata mmoja.
Kuna mtu alinidokeza kuna mtu ana lab Arusha,yeye alimuona kwenye maonesho fulani ya kilimo,huyo mtu anafanya large scale production ya tissue culture plants,hata miche 3000 unapata in one go,lakini hakuwa na namba ya huyo mtu,nimeulizia sana kuhusu huyo mtu mwenye lab sijampata(labda hayupo lol)...ila nimeshachoka kumtafuta,ntaendelea kusubiri sua.
other than that,kila la kheri!