Nahitaji taarifa kuhusu TAESA Internship Program

Ni hivi interview zao huwezi kufel niamin mimi hata mtu ambaye hajasoma vidato anafaulu
😂😂😂 Tuombe Mungu mambo yawe mazuri na kazi ipatikane kwa haraka, mm nilifanya Interview yao Ijumaa iliyopita.
 
Walinipigia simu niende kwa ajili ya training then nikafanya na interview ofisini kwao
mkuu naomba kujua kwa hao je kama uko mbali na office zao unafanyaje interview na je kupata internship kwa hawaangali maswala ya GPA kama private wanataka second class upper
 
mkuu naomba kujua kwa hao je kama uko mbali na office zao unafanyaje interview na je kupata internship kwa hawaangali maswala ya GPA kama private wanataka second class upper
Kama uko mbali na ofisi zao aisee hapo cjui itakuaje ila nakumbuka kuna raia alitoka Morogoro kuja kufanya Interview labla ww angalia ofisi ya kanda iliyokaribu na ww, kuhusu GPA wao taesa hawahusiki nalo ila kampuni ndo watahusika mana wataangalia mtu wanaomtaka
 
Kama uko mbali na ofisi zao aisee hapo cjui itakuaje ila nakumbuka kuna raia alitoka Morogoro kuja kufanya Interview labla ww angalia ofisi ya kanda iliyokaribu na ww, kuhusu GPA wao taesa hawahusiki nalo ila kampuni ndo watahusika mana wataangalia mtu wanaomtaka
sawa nimeelewa mkuu
 
Walinipigia simu niende kwa ajili ya training then nikafanya na interview ofisini kwao
Sasa wengine wanaombwa kufanya interview kwa simu maswali mawili tu wenyewe wanakuwa wamechoka unachukua max zako za bure pasi yakutokujua uko na nondo pembeni yako unasoma tu
 
Hawa ni agents wa serikali na baadhi ya makampuni binafsi wanotumika kurecruit interns.
Utaenda pale utajisajiri hakikisha umebeba vyeti vyako original.
Baada ya muda utaitwa kwa ajili ya interview kisha baada ya hapo utapatiwa training.
Ikitokea nafasi inayoendana na elimu au skills zako basi utaitwa na kupelekwa ofisi husika ukaanze internship.
Wanalipa posho ya sh 150,000/- tu kwa ajili ya lunch na nauli. Ila ukibahatika ofisi uliyoenda wakawa nao wanakupa chochote basi Mungu mwema.
Wao huwa wanatoa nafasi kwa either miezi sita au mwaka pekee. Baada ya mwaka kuisha wanakua wamemalizana na wewe na endapo ofisi uliyokua ukifanya internship wakakuhitaji basi itawabidi wenyewe ndio wakulipe au waingie makubaliano na wewe.
Hii kitu ndio imepelekea wengi kuajiriwa na taasisi hisika wanakofanya internship hasa kwa wale ambao hawapitii utumishi maana huwa ni kama wanathibitishwa tu hata kama tangazo limetoka na mkaitwa interview na imeongeza kelele za kusema vimemo vinafanya kazi.
Ukumbuke TAESA hawaajiri, kwa hiyo ukipata nafasi usiache kuendelea kutafuta kazi sehemu nyinginezo.
Naomba kuuliza, mfano shirika la kiserikali linahitaji watu wanaanzia huko taesa au kule ajira portal.?
Kuna jamaa yangu alifanya kila kitu hapo taesa alifanya training na interview (hakufanya internship) ikapita kama miezi sita akaona kazi ajira portal inayohitaji mtu kama yeye ali-apply ajira portal na akafanya interview lkn kwa bahati mbaya hakupata kazi.
Sasa ndo nauliza kazi inaanzia wapi taesa au utumishi.?
 
Kwa upande wangu sikujisajili wala kufanya interview nlikua referred sabab kozi yangu watu kuwapata sio rahisi hivyo walinitafuta wenyewe.
Mie mkuu nimejisajili hata week tatu sina wamenpigia kuniuliza ka nshafanya interview sijui kuna mchongo ila wameniambia niende j3,
Kada engineering
 
Sasa wengine wanaombwa kufanya interview kwa simu maswali mawili tu wenyewe wanakuwa wamechoka unachukua max zako za bure pasi yakutokujua uko na nondo pembeni yako unasoma tu
Habari
Samahani Kama una namba zao naomba na website zao Ni zipi nisaidie
 
Back
Top Bottom