sweetlady
JF-Expert Member
- Dec 24, 2010
- 16,947
- 8,409
Habari wana jamii wenzangu. Nimeolewa, kabla sijapatwa na mkasa ninaotaka kuwaeleza nilikuwa namuamini sana mume wangu. Mwaka jana mwezi wa 6 nikagundua kuwa ana mwanamke (mama mtu mzima ) Kuanzia hapo moyo wangu umekuwa mgumu sana kumwamini ingawaje tulishayaongea na alikiri na kuniomba sana msamaha ila kuna wakati kumbukumbu zinanijia na ghafla najikuta namchukia mno. Niasaidieni cha kufanya coz nahisi nimeathiriwa na tukio kwa kiasi kikubwa sana. Imefikia mahali sifurahii tena tendo la ndoa na kuna wakati naweza kumnyima hata mwezi mzima. Kabla ilikuwa tunashirikiana vizuri tu ila kwa sasa nipo nipo tu. Huwa najiuliza je kama niliweza kumtimizia kila kitu kama mume na bado akanisaliti kwa nini niendelee wakati nmeshagundua kuwa hatosheki? Kweli naishi nae basi tu ila moyoni kwangu hayupo kabisa. Nilishamwomba tuachane kwa upendo akakataa eti tutamwathiri mtoto, eti bado ananipenda ni shetani tu alimpitia na hatampitia tena. Anachonikera zaidi ameanzisha tabia ya kunichunga kama mbuzi, hata nikienda saluni siondoki mpaka aje kunichukua, madai yake eti anaogopa nitamlipizia. Nikiwa kazini cm masaa yote na anafika kunichukua dakika 5 kabla ya muda wa kazi kuisha. Nisaidieni wajameni coz kweli sina upendo na huyu mtu. Hilo jimama alishaliacha na viapo tele kuwa hatarudia tena. MOYO MGUMU KUSAMEHE! NIFANYEJE???