nahitaji mguu wa kuku

nahitaji mguu wa kuku

yeleuwiii hivi ni nini nimesoma roho ya mauti toka ushindwe na ulegee
 
waheshimiwa nisaidieni jamani nahitaji nami nimiliki mguu wa kuku (bunduki), nimebahatika kukopa ka-starlet sijajua kuendesha vizuri sasa watu waki ni over take huwa naumia sana,mfano juzi daladala ilini over take halafu konda kaniambia tulia wewe, basi nika funga brake za ghafla kisha nikakasirika nilishuka bahati mbaya sina nguvu, kweli nikatamani na miimi ningekuwa na mguu wa kuku yaani hawa maboda boda wanavyoyaendesha kwa fujo ningewamaliza wotee manake huku barabarani kuna watu wanatia kweli hasira, halafu pia kwenye ma bar watu wakijua una mguu wa kuku wanakupa heshima mno una uwezo wa kumchukua mrembo yoyote maadam tu uwe umeiweka sehemu ambayo kila mtu ana uwezo wa kuiona, kingine ni kwamba wapenzi siku hizi wamekuwa siyo waaminifu hivyo nikiwa na mguu wa kuku nakuwa na uwezo wa kumtuliza mwizi wangu wote pamoja na huyo mpenzi kama matukio mengi tunayoyasikia kwa sasa ....kwa sababu tajwa hapo juu nilikuwa naomba ndugu wasomaji mnishauri utaratibu wa kumiliki hii kitu au hata kama kuna mtumishi yoyote asiye mwaminifu aliyepewa dhamana ya hii kitu aweze kuniuzia ya kwake kwani kale kautaratibu ka serikali ni karefu mnoo


asanteni kwa kunielewa

-----.
 
Kwa hayo maelezo ya mdau ataishia kumiliki mguu wa kuku orijino kama huu.
0000117_leg-oil_300.jpeg
 
illegal migrant pita maeneo ya Buguruni au mitaa ya uswazi nyakati za jioni utapata miguu ya kuku za kumwaga: utapata mbichi, zilizochomwa, zilizokaangwa na hata za kuchemsha! Yaani unachagua unayotaka mwenyewe!😡
 
Last edited by a moderator:
Kabla hauja pata huo mguu wa kuku omba mungu akuondolee huyo shetani mbeba maovu aliyekutawala kimawazo kisha akakuogoza kuleta haya maneno ya kutaka mguu wa kuku.
 
Dawa yako ipo jikoni vumilia kidogo
 
Ingekuwa kwa ajili ya kuchalaza maccm.ningekupa ushirikiano wa kutosha.kwa hizop sababu..we endelea kutafuta
 
huyu jamaa sizi yake ni rungu, manati ama sana sana upinde! Hana sifa kabisa za kumiliki cha moto! Na anahitajika mirembe!
 
hii kitu unaweza kujikuta wewe ndo unailinda zaidi ya yenyewe kuilinda...
 
Watie Vitasa wala hautaji mguu wa Kuku labda kama wangekuwa mbwa mwitu
 
Aisee we jamaa umenifurahisha sana!!!!! Kwi kwi kwii kwiiiiiiii....eti Tulia weweee....

Ujue kuna watu duniani waliumbwa kuchekesha wengine tu ilimradi raha tupu. Hii thread naona jamaa alikaa akaona muda wote watu wanasoma thread za kuudhi na kusikitisha; basi yeye kaamua kuwafurahisha kidogo wana JF. Safi bwana illegal immigrant. unawaongezea watu siku za kuishi
 
Mwanangu ukipata mwenye miguu miwili nistue hata mm nahitaji. Naumiaga sana nikinyanyaswa
 
mkuu manati tu inafaa au wakiku overtake nawe kazana mpite af funga brake kwa nguvu ukiwa mbele ake kwa ninavyojua daladala nyingi brake za mashaka lazma atakugonga kwa nyuma hapo unamuuzia kesi anakulipa starlet mpya kutuliza hasira zako
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom