Habari za kwenu humu
Nina mwaka wa 12 sasa nakunywa pombe, nahitaji kuacha lakini nashindwa. Kila nikijaribu kuacha napata wakati mgumu sana hasa nimeshazoea nikinywa napata usingizi mapema usiku. Wiki hii nimejaribu kuacha kunywa siku moja, lakini usiku sikupata usingiz kabisa... Nimehisi mauzauza usiku mzima, nimekaa macho mpaka asubuhi.
Je hali hii ndo huwatokea wanywaji wote au ni kwangu tu? Jana kuna rafiki yangu ambae hatukuonana kitambo sana, ameisha sana kwa sababu ya pombe. Hii imenifanya nifikirie kuacha hii kitu, mana ninakoelekea si pazuri.
Nifanyeje ili niweze kuacha bila kupata hayo mauzauza ya kukosa usingizi?
🇹🇿Kwanza hongera sana kwa kuweza kulitambua tatizo na kuanza juhudi za kupambana na tatizo mwenyewe. Hapo umeshafanikiwa kupona ugonjwa huo kwa asilimia 80
🇹🇿 Ni kweli pombe na ulevi mwingine vimewaharibia watu maisha yao sana. Kuna watu walikuwa na akili nyingi sana kazini ila wamefukuzwa kazi kwa sababu ya ulevi uliopindukia, kuna watu wamefariki dunia mapemba kwa.kuharibu viungo vyao vya ndani kwa sababu ya pombe kali, kuna watu wamevunja ndoa zao kwa sababu ya ulevi, kuna watu.wameuawa kwa kuhisiwa ni wezi usiku wakitoka kwenye ulevi
🇹🇿 Mlevi ni mbinafsi na huitesa familia yake, asilimia kubwa ya mapato huitumia kunjwa na wanaoitwa marafiki na nyumbani asilimia ndogo tuu ya mapato hutumika
🇹🇿 Ukiona kitu fulani kinafurahisha sana mwili wako ujue kinakutafuna ndani kwa ndani, maumivu yake utayasikia baadaye. Huwezi kuwa myumwa wa mwili na.ukiona kitu kimepingwa sana na mila , na dini usikijaribu maana ukikijaribu utavutiwa na kukiacha utashindwa ndiko shetani alikojificha
🇹🇿 Usidanganyike na watu wanaokunjwa lakini mambo yao yapo safi, Miili yetu imeumbwa kwa udongo tofauti. Kuna wachache wenye uwezo wa kuhimili vilevi ila wengi ulevi huwa ndio vyanzo vya matatizo yao ya ndoa, ukoo , dini , kazi na familia
🇹🇿 Ukiacha ulevi unapoteza kundi kubwa la marafiki ambao unadhani walikuwa ni washauri wako na wengine wanakupa mchango/ ramani ya kazi lakini amini usiamini ukiacha ulevi unapata marafiki wapya wema na wazuri, utaanza kuaminika kazini, nyumbani na vikao vya watu wa busara
🇹🇿 Kuna watu kama mimi niliamka tu siku moja nikasema kuanzia leo pombe basi. Nina miaka zaidi ya 20 sasa tangu niache, niliteseka kwa muda ila iliisha nikahamia kuwa adicted wa soda mwakahuu ulipoanza nikasema bas na hadi leo nimeacha soda
🇹🇿 Nadhani naamini kuna baadhi ya koo wana laana ya kutokunywa pombe na ukijaribu kunywa inainhia kichwani na kukuletea uchizi, wapo watu walitegemewa sana na familia zao ila pombe ndio hivyo imeharibu mfumo mzima wa maisha yao
🇹🇿🇹🇿 Sina ushahidi nimewahi kusikia kuna ushirikina wa kulogewa pombe ambapo utakuwa mlevi hadi pombe zikuue na nasikia kuna dawa za kienyeji unaweza kuchanganjiwa kwenye pombe ukatapika vitu vya ajabu na kuanzia hapo utakuwa umeacha pombe kabisa na ule uchizi wa pombe unaisha na kurudia akili zako