Nahitaji kuacha kunywa pombe

Nahitaji kuacha kunywa pombe

Pole sana, ila jitahidi upunguze sio kuacha.
Ukijifariji umeacha, siku ukija kuzimua tutakuzika.

Punguza tu kijana, usiache.

Na uzuri ukipunguza utaanza kuiongoza sio kama sasa inavokuongoza hadi kupata usingizi unaitegemea.
 
Piga chini kampani zote za tungi...
Oa..
Kama unakaa nyumba ya walevi hamaa...
Fikiri malengo mapya, kama huna nyumba anza ujenzi...kama huna watoto zaa...
Usikae na hela ambayo haina kazi...
Anza dose ya kutoa sumu ya pombe mwilini...
mku ushauri mzuri sana tena sana. Dawa ya kutoa sumu ni ipi naomba mwongozo
 
Mimi nilitaka kuacha kwa sababu nilihisi kama inanifilisi,, nilikaa week tu na pesa sijapata kama navyoipata nikinywa.
Kwahyo kilalaheri mkuu
 
Boss ili uache unatakiwa kubadili mazingira na watu unaoishi nao uishi na watu ambao hawapendi kukuona katika hali ya ulevi na pia hauwezi kunywa au kulewa mbele yao , utajikuta siku zinakatika bila kupiga pombe na mwisho wa siku utaacha au utakuwa unakunywa mara moja moja kutokana na events, au kama unaishi mwenyewe tafuta mtu ambaye atakufanya uache pombe ishi naye nyumba moja iwe mtoto au mtu mzima ambaye utakuwa unahofia kulewa mbele zake au atakuwa kama management yako
Acha na uanze kufanya mazoezi
 
Back
Top Bottom