Wakubwa Shkamooni na Wadogo Habari zenu.
Jamani naomba ushauri wenu,mm ni kijana mdogo sana sbb sijafikia miaka 30,kwenye jamii yangu ninayoishi mm ni kijana wa kupigiwa mfano kwa kuwa nimepata maendeleo mapema kuliko vijana wote waliobakia wa rika langu.
Nilianza kumiliki Nyumba ya kisasa nikiwa kijana wa miaka 17 tu,nilipofikia umri wa miaka 18,nilifunga safari za kwenda Dubai na Thailand kufata biashara za electronics,na kwa kuwa n kijana mm tu niliejanjaruka kwa wakati huo,nilipata faida ya haraka sana nikaweza kumiliki gari tatu za abiria,na kama haitoshi nikanunua boti mbili za uvuvi,ikumbukwe kwa wakati huo nilikuwa na umri wa miaka 19 tu.
kwa wakati huu naandika habari hii nina miaka 23,nimeshakuwa na vitega uchumi vingi tu.
Najua utakuwa na hamu na kujiuliza kwa nini nimesema nimerogwa?.napenda kuchukua fursa hii nikuelezeni kwa nini nimesema hivyo,maana huenda msaada wenu utakuwa na manufaa kwangu!.
Mtaani kwetu ninapoishi nilijenga mazoea ya kiurafiki na mama mmoja ambae ni kweli nilimtumia kama mshauri wangu wa kibiashara,basi huyo mama alikuwa amebahatika kupata watoto watoto 3,mmoja akiwa wa kike,na ikumbukwe huyo mama alipenda sana kunifanyia matani muda mwingine akiniita "Mkwe wangu".
nilipokuwa na miaka 22 nilitamani sana kupata msichana ili nifunge nae ndoa,nilimfata yule mama kwa ajili ya kunipa ushauri kuhusu ndoa,basi matatizo yote yalianzia hapo,sbb yule mama alinitaka nimuoe mtoto wake,na pia aliwahi kuniambia kitu kuwa ikiwa sitomuoa mtoto wake basi mm na yeye tusizungumze kwa lolote,na litakalonipata nisije kulia na yeye,niliogopa sana.
Kwa kuwa mm yule binti yake hakunivutia kwa kuwa hakuwa wife material,niliamua kumuoa msichana mwengine,basi alihamaki sana hata siku hizi nikimsalimia haitikii kabisa,na kama haitoshi,tangia nilipofunga ndoa mambo yangu kibiashara yamekuwa ya hovyo sana,mara ya mwisho kwenda dubai ilikuwa mwaka jana,biashara zangu zimeyumba sana,gari zangu 3 nimeshauza tayari,na boti yangu moja ilizama na wale watu wangu waliokuwa wanavulia wamekufa wakati inazama,niliumia sana,kwa sasa nimebaki na boti moja tu,ambalo hata halifanyi kazi vizuri,siku hizi nikifanya biashara napata hasara sipati faida.
Nilijaribu kumuomba radhi yule mama ili tuishi kama zamani,ila amekataa hata kuzungumza na mm,ki ukweli mm siwezi kumuoa mwanae namjua hajatulia,kwa kuwa alishawahi kufanya mapenzi na marafiki zangu wawili ambao tulikuwa tunashirikiana kwenye biashara,siku hadithiwa nilimuona mwenyewe kwa macho yangu alipovunja amri ya sita.
Kiukweli ninaumia sana jinsi nilivokuwa zamani na nilivo sasa.
Naombeni munishauri nifanye nn ili niwe kama zamani.
AHSANTENI.