kinyama nje
JF-Expert Member
- Jul 3, 2017
- 1,839
- 2,487
Wasi wasi wako tu Hamna kitu
Perception creates reality... Makutano ya kiroho hutokea kwa watu wanaopatanaje ni mawazi tu au ni mzimu wa marehemu ulimtokea kwa ndoto? tupe nondo mtaalam wa hizo kazi
Yeah mkuu...hapo ni hao roho wa nguvu za giza wakiwa kazini kwa njia ya ndoto...marehemu hayupo hai tena. Na hata huko mbinguni hayupo...Pepo hilo mkuu akija mkemee kwa jina la Yesu halitarudi tena
ufafanuzi please mkuuPerception creates reality... Makutano ya kiroho hutokea kwa watu wanaopatana
Una kitu inaitwa hallucinations na illusion unahutaji counselling period
Mkuuhiyo ni dalili mbaya si muda mrefu Israel anakuja kukuchukua saiz anakamilisha visa yako ya kuzimuWakuu habari za mihangaiko
Leo naomba kama kuna wataalamu wa mambo ya ulimwengu wa roho naomba mnisaidie kunijibu swali langu hili
Nilikua na rafiki yangu wa kike kiukweli nilimpenda vilivyo
Mimi kipindi namaliza yeye alikua mwaka wa pili
Nilikua nataniana nae sana nilipendelea kumuita strong woman
Kwasababu alikua anajihamini sana na alikua mchangamfu sana na alikua mcha Mungu na nilikua naimba nae kwaya moja
Nakumbuka hata siku namaliza chuo Nilienda kumuaga kama mida ya SAA tatu usiku nikimpa taarifa kua kesho yake nasafiri
Lakini alinipigia simu tena kama saa saba usiku akaniambia asubuhi kabla sijasafiri niende anione tena kwa Mara ya mwisho yaani nikamuage tena
Basi me ilipofika asubuhi nikaamka nikaenda kumuaga tena kama alivyonisihi
Tukaagana vizuri tuu nikaondoka kurejea nyumbani
Siku zikapita nikawa naendelea kuwasiliana nae mchana na usiku
Baada kama ya siku kadhaa kupita akaugua ghafla na mauti yakamkuta
Nakumbuka ilikua muda ya SAA sits mchana nikatumiwa ujumbe kwamba amefariki
Kiukweli nilihisi kama utani nikampigia simu marehemu nikiamini hajafa ni utani tu
Simu yake haikupatikana ikabidi nimtumie SMS
Yani kiujumla nilikua kama nimechanganyikiwa kwa muda huo
Nilipata uhakika baada ya kuona picha zake zikianza kusambaa mitandaoni zikiwa na neno R.I.P
Sikua na namna tena nililia kwa sauti kuu nikimlilia
Nilimlaumu sana marehemu kwanini hakuniaga,
Nilitamani aamke ninuulize hats swali moja kisha alale tena
nilifika mpaka hatua nikaanza kumwomba Mungu aniletee huyu Dada kuna kitu nataka nimuulize kisha amchukue tena.
Zilipita kama siku mbili siku ya tatu nikiwa nimelala nikaota ndoto yule msichana akanijia tukapiga story kisha alivitaka kuondoka akaniambia "usilie sana tusipoonana tena duniani tutaonana mbinguni" akaondoka
niliposhtuka usingizini nilihamaki sana nikajiuliza mini maana ya ndoto hii? Je kweli amerudi kumuaga?
Basi asubuhi nikamuandikia rafiki yangu SMS nikamueleza Jana usiku niliota Grace amekuja na akanisihi tutaonana tena,
Rafiki yangu akanijibu kua ninamuwaza sana ndio maana hadi namuota kwaiyo nipunguze mawazo
Basi nikapotezea
Ikapita kama wiki moja nikiwa nimelala nikaota ndoto tena
Grace akaja tulikua chini ya mti tena mazingira tuliyokuwepo ni mazuri sana nikaongea nae mambo kibao kisha akaniambia anawai sana kwani siku hiyo ni siku ambayo mbinguni wako wanajifunza masomo ya biblia kisha akasepa
Nikashtuka tena usingizini kiukweli nilikosa majibu juu ya hii ndoto
Nilibaki nahamaki sana
Mpaka leo Nahisi marehemu alirudi kuniaga
Wadau kwa yoyote anaeweza kuwa anajua ni mini maana ya hizi ndoto?
Je inawezekana ni kweli marehemu alirudi kumuaga au?
Na wengi hudanganyika wakiamini ni kweli wapendwa wao wamerudi ila ni uongo maana wafu hawajui neno lolote wamelala kwenye kimya mpka ya ufufuoYeah mkuu...hapo ni hao roho wa nguvu za giza wakiwa kazini kwa njia ya ndoto...marehemu hayupo hai tena. Na hata huko mbinguni hayupo...
Sasa anakuelezaje kuwa eti mbinguni siku hiyo wanajifunza masomo ya biblia..? Kweli kabisa? Nani anawafundisha hayo masomo? Kuna kifungu kwenye biblia kinathibitisha hayo aliyokueleza ndotoni?
Acha kututisha tutakutoa kwenye ukooInasemekana KUWA "siku 30 kabla ya mtu kufa hufanya mambo ya tofauti au mazuri au mabaya".
Mimi zamani nikiwa Teen nilikuwa nikikuota umefariki ndugu yangu wewe andaa wosia maana unakufa kweli kwa sasa naota watu hawafi
Siku hizi siwezi.Acha kututisha tutakutoa kwenye ukoo
hahahahaha
Mkuu, kwanza huyo mdada alikuwa mcha Mungu na mcha Mungu yoyote aliyezama ndani ya Yesu kabla hajaondoka hapa duniani huwa anaaga. Tazama akina Paulo, Yesu n.
.
.
Mawazo pia yanachangia ila pengine malaika amekuja kupitia sura ya marehemu ili kukwambia ni wapi marehemu alipo baada ya safari yake ya maisha hapa duniani ili kukutia moyo na wewe kukazana ktk imani ili ufikr alipo mtumishi wake aliyetangulia.
.
.
Kumbuka walio ndani ya Kristo hawafi bali wanalala na siku ya mwisho ajapo Kristo wanainuka na Kristo Yesu kwenda kumlaki Bwana mawinguni. Heri wafu wafao sasa ktk Kristo Yesu.
.
.
Tubu mbele za Mungu na uishi ktk uchaji wake, siku ya hukumu imekaribia, tutubu dhambi zetu tuondolewe ktk habari ya dhambi.
Mhubiri 9:5 Wafu hawajui lolote
Zaburi 115:17 Wafu hawawezi kumsifu Bwana
Kumb. 18: 11 Msiombe wafu
2Wakor. 11: 13-15 Shetani na malaika wake (Majini/mapepo) hujigeuza wawe mfano wa waliokufa ili kupotosha neno la Mungu . Kwa kifupi huyo uliyeota sio Grace bali unaongea na pepo kwenye ndoto ambalo huvaa umbo na sura ileile ya mpendwa wako ili uzidi kuamini kuwa kuna maisha yanaendelea baada ya kifo.
Wafu wote watakuwa hai Kristo atakaporudi kuwafufua (Yohana 5:28-29)