Nahisi kuachwa na niliempenda

Nahisi kuachwa na niliempenda

Nyanya mbichi

JF-Expert Member
Joined
Nov 10, 2011
Posts
3,716
Reaction score
2,220
Nilikua na mdada na mdate kwa miaka kadhaa sasa,ila mwaka juzi Mamake akawa hanitaki kwa kuwa Mimi hohehahe sina kitu,lakini baada ya kuambiwa na watoto[jamaa tu] kuwa Mimi ndio natoka na mwanae.

Waliwahi kuwapeleka kwa Mama wanaume wenye mkwanja akawatolea nje,kipindi nasoma na yeye ni teacher mkoa fulani,mwakajana alipewa na bibi yake dawa ili aachane na Mimi ataitupa,mwakajana mwishoni Mamake bint akawa anaumwa,akamwambia mwanae mbona haolewi,wakati huo ndio nimemaliza college

Nikambembeleza yakaisha,siku moja Mamake binti akampigia simu mfanyibiashara mwenzake amkopeshe pesa,akaenda jamaa mpaka home kwa Mama mkwe wangu akatoa pesa akamkopesha Mama,jamaa akamwambia Mama mtoto yupo hapa,nipe mwanao nimuoe nitakupa zaidi ya hizo.

Jamaa alivyoondoka Mama akawa anamlaumu mwanae kwa kukomaa na hohehahe Mimi na kuwaacha watu wenye pesa,amenisaidia sana mdada mpaka nimemaliza college,mtoto aliridhika na Mimi ila Mama na ndugu hawanitaki kabisa,mwakajana Mamake alilia akiwa mgonjwa na akamwambia afe bila kuona wajukuu sio sawa,

TImbwili likawa kwangu bado kiuchumi sijakaa vizuri hata kidogo,from no where baby wangu akawa akirudi mjini haniambii,akawa anataka nguo zake eti ziko kwangu kitambo hazitumiki,nikawa naingia wasiwasi nikawa namuuliza kama nataka kunitema akawa anakataa,siku moja akaibuka home gafla nilikua na homa kidogo akaja kuchukua nguo zake nilikua na msela sebleni.

Nikaenda nae room nikamuuliza kama kunatatizo akasema hakuna amefuata nguo zake,nikalazimika kumpa shingo upande,simu nikipiga hapokei ontime au hapokei kabisa,texts hajibu au anareply late,akaweka status 'burning the past' sikusema kitu baada ya kuona nadharaulika nikaacha kupiga simu na kutuma texts pia,akaenda Instagram akaweka nyimbo ya christian Bella aliempenda kwa dhati eti amemkimbia.

Sejasema kitu mpaka sasa zaidi ya mwezi na ushekh hatuwasiliani kwa ufupi ,ingawa nilimuomba aniambie mapema kama amepata mtu mwingine,aaah ajabu Baba yangu anampenda sana huyu bint ingawa hajawah kumuona,alikua anampigia simu na kumsalimia na mzazi wangu hajawahi hata siku moja kuwa na mawasiliano na wapenzi wa watoto wake ila kwa huyu bint imekua tofauti

......nahisi sina changu tena.....

Wakuu nimekwama nafanyaje hapa au ungekua wewe ungefanya nini?

serious hii case niko nayo nilikua na malengo nae sana sana huyu mtu.
 
Kuna vitu vikipangwa na Mungu vinakuwa tu, inaonekana huyu hujaandikiwa kama hana msimamo namna hiyo. Inauma lakini mwezi ujao wakati kama huu utakuwa umepata nafuu na kuanza kumsahau kama juhamsahau kabisa. Mwache aende unaweza kukuta kuna mzuri zaidi umeandikiwa na Mungu utakutana nae. Wehenga walisema mlango mmoja ukifunga mwingine unafunguka. Huwezi kuacha mlango wazi ili mwingine ufunguke, hapana.
 
Pole sana kijana huyo kashapata ustaarabu mwingine na wewe usiumize kichwa tafuta pumziko lingine mbona watoto wazuri wapo wengi tu!!
 
Pole ndugu,kama ni wako atarudi tu,no matter what. Ila kama si wako bila shaka utamsahau na kusonga mbele,jipe muda tu
yaani mimi mtu aniache kisa njaa halafu baadaye arudi hakuna hiyo, ningekuwa playboy ningemtia kisha namuacha ila sina michezo hiyo, aende zake tu kwa amani (sijui kwa nini hili limenichoma sana pamoja na mikasa mingi inayowekwa humu)
 
Nina uhakika kwasasa nikiachwa na mwanamke/ mpenzi wangu yeyote sintaumia tena wala kupata stress kama zamani.

Mimi nilishakuwa kikomazi na sugu wa kuachwa.
 
Nina uhakika kwasasa nikiachwa na mwanamke/ mpenzi wangu yeyote sintaumia tena wala kupata stress kama zamani.

Mimi nilishakuwa kikomazi na sugu wa kuachwa.
Wewe hata yule wa bottom of the heart, yule ambae hata jina lake likitajwa hasira zinayeyuka ghafla?
 
Wewe hata yule wa bottom of the heart, yule ambae hata jina lake likitajwa hasira zinayeyuka ghafla?
Sio siri mimi yupo ambaye nilimpenda sana na kumuwekea malengo kabisa akawa ananiacha acha bila sababu za msingi kumbe alikuwa ananicompare na mwingine especcially kwenye suala la kiuchumi, kwa kumpenda nikamwomba msamaha mimi japo kanikosea yeye.

Tukarudisha closeness kwa muda flani akaniacha tena...ikafikia mahali nikachoka na kugive up na sikuwahi kumcheat before.

From there nikaamua kuachana naye rasmi ingawa sasa anataka turudiane ila nimebaki na msimamo huohuo na itabaki hivyo.
 
Kuna vitu vikipangwa na Mungu vinakuwa tu, inaonekana huyu hujaandikiwa kama hana msimamo namna hiyo. Inauma lakini mwezi ujao wakati kama huu utakuwa umepata nafuu na kuanza kumsahau kama juhamsahau kabisa. Mwache aende unaweza kukuta kuna mzuri zaidi umeandikiwa na Mungu utakutana nae. Wehenga walisema mlango mmoja ukifunga mwingine unafunguka. Huwezi kuacha mlango wazi ili mwingine ufunguke, hapana.
Ameen
 
Pole sana kijana huyo kashapata ustaarabu mwingine na wewe usiumize kichwa tafuta pumziko lingine mbona watoto wazuri wapo wengi tu!!
Dr wa ukweli bado navuta subra kujua hatima yake,kutafuta mwingine harakaharaka sio sawa nisijefanya wrong choice nikajilaumu

Asante kwa ushauri
 
Pole sana, kwanza nakusifu kwa ujasiri wa kutokuendelea kujiumiza kwa kumpigia magoti na kumkumbusha mlipotoka. Usijutie wala usijilaumu kwa hali iliosababisha wewe kutokuanae, huwezi kujua Mungu amekuepushia nini, mwanaume kamili ni yule anaewaza kuachana na ampendae kwa busara pasi na kinyongo moyoni, yaani kiroho safi kbs hata mkikutana salam km kawaida. Nafasi, muda na kila ulichokuwa umekitenga akilini kwa ajili yake viwekeze ktk kutafuta maisha hakika utafanikiwa.
 
Ndio mapenzi hayo mdogo wangu.. Punguza slope, unaweza kufa kwa presha
 
Pole ndugu,kama ni wako atarudi tu,no matter what. Ila kama si wako bila shaka utamsahau na kusonga mbele,jipe muda tu
Unamshauri akirudi ampokee? Yani aingie apendapo na atoke ajisikiapo kama bafuni?
 
yaani mimi mtu aniache kisa njaa halafu baadaye arudi hakuna hiyo, ningekuwa playboy ningemtia kisha namuacha ila sina michezo hiyo, aende zake tu kwa amani (sijui kwa nini hili limenichoma sana pamoja na mikasa mingi inayowekwa humu)
Asante bro inauma sana kwa kweli,kiasi hata ujio wa gafla home labda angenikuta na demu angepata sababu ,alinikuta sebleni na rafiki yangu alietoka mkoa kuja kujiuguza tunapiga story tu

Inauma sana
 
Sio siri mimi yupo ambaye nilimpenda sana na kumuwekea malengo kabisa akawa ananiacha acha bila sababu za msingi kumbe alikuwa ananicompare na mwingine especcially kwenye suala la kiuchumi, kwa kumpenda nikamwomba msamaha mimi japo kanikosea yeye.

Tukarudisha closeness kwa muda flani akaniacha tena...ikafikia mahali nikachoka na kugive up na sikuwahi kumcheat before.

From there nikaamua kuachana naye rasmi ingawa sasa anataka turudiane ila nimebaki na msimamo huohuo na itabaki hivyo.
Mimi niliumia nilimsubiri kama miaka mitano na mawasiliano mazuri tu, sijui kilibadilika nini, siku moja akaniambia mimi na yeye hatuna future tena nimwache aendelee na maisha yake. Ile siku ndiyo nilijua watu wakisema moyo unauma, physically niliyahisi maumivu ya moyo. Alifunga ndoa lakini baada ya miaka mitatu kwenye ndoa vilibuma huko, akaanza kunitafuta, mimi tena? No thank you.
 
Back
Top Bottom