balimar
JF-Expert Member
- Sep 18, 2015
- 7,882
- 13,936
Mimi naitwa Anania Titus Mbuta
Mimi ni Mwalimu mwenye Shahada ya Pili katika Elimu (MAEd, Udsm -2017).
Baada ya kumaliza Shahada ya kwanza (BAEd, Stemuco - 2012).
Hata hivyo mafunzo ya Ualimu niliyapata Chuo cha Ualimu Ilonga, 2003.
Kuhusiana na uzoefu kweny mambo ya utawala mimi ni Afisa Elimu Kata na ni mwezeshaji wa Taifa Tasaf
maswala ya Uwekaji wa Akiba na Uundaji wa Vikundi.
Nia hasa ya kugombea nafasi hii, nataka kutengeneza mazingira rafiki kati ya mwalimu na chama.
Walimu wanaweza kufanya makubwa sana ndani ya mwamvuli wa chama kwa kuboresha vitega uchumi na
kuongeza usimamizi wa Miradi iliyopo na kuongeza tija kwa walimu
Mwisho, kuna haja ya kurekebisha katiba ya chama kwa kuyapitia upya maoni yaliyokusanywa ili katiba ya chama
iendane na mahitaji na mabadiliko yanahitajika kuboresha utoaji na upatikanaji wa Elimu nchini. Hili linawezekana
endapo tutapata viongozi makini na wenye uthubutu kama Anania Titus Mbuta
Tafadhari mniunge mkono na nitangaze kwenye magroup ya walimu waniunge
Naambatanisha poster yangu