Nafunga ndoa natawakali

Sokomoko

JF-Expert Member
Mar 29, 2008
1,915
127
Salaamu zangu natuma, zifike kila mahali,
Tunaziomba rehema, za Mungu zituwasili,
Hapo siku ya Qiyaama, tuwe chini ya kivuli,
Nafunga ndoa natawakali, naoa mke Muumini.

Naoa mke Muumini, nafunga ndoa natawakali,
Mke aloshika dini, na kila siku kuswali,
Hijaab ipo kichwani, afunikae wote mwili,
Nafunga ndoa natawakali, naoa mke Muumini.


Sijatafuta uzuri, au yule mwenye mali,
Nimechagua tabia nzuri, alotulia akili,
Aloleleka vizuri, kidini na kiasili,
Nafunga ndoa natawakali, naoa mke Muumini.

Sikumtafuta kwa haraka, nijionyeshe kamili,
Zinifikie baraka, za Mola wangu Jalali,
Nitulie kwa hakika, tabia mbaya nibadili,
Nafunga ndoa natawakali, naoa mke Muumini.

Fadhila zake ni nyingi, uliza kila pahali,
Huo ndio ni msingi, wa maisha ya halali,
Ni kinga kwa mambo mengi, kwa madhambi mbalimbali,
Nafunga ndoa natawakali, naoa mke Muumini.

Kuoa ni utulivu, tumeshaona dalili,
Huyaondoa maovu, na mambo huwa sahali,
Hukufanya mtulivu, shida ikikukabili,
Nafunga ndoa natawakali, naoa mke Muumini.

Wajibu wangu tatimiza, tutakapokuwa wawili,
Tukikaa kuzungumza, na mambo kuyajadili,
Tutajaribu kueleza, tuelezane ukweli,
Nafunga ndoa natawakali, naoa mke Muumini.

Niwe msimamizi, kwa mali na kila hali,
Ayaonyeshe mapenzi, maneno kama asali,
Katika masimulizi, sitosema kwa ukali,
Nafunga ndoa natawakali, naoa mke Muumini.

Mungu atupe watoto, hao ni rasilmali,
Mke ni mama watoto, awe mwema na mkali,
Awatazame watoto, wasikuwe kijahili,
Nafunga ndoa natawakali, naoa mke Muumini.

Mke ni nguzo nyumbani, kama vile matofali,
Na mume ndio rubani, huona yaliyo mbali,
Kamba ya Mungu tuishike, ibada iwe awali,
Nafunga ndoa natawakali, naoa mke Muumini.

Mungu Watunze vigoli, pamoja na wanawali,
Wawe kama wa awali, kama zama za Rasuli,
Nimemaliza kauli, hapa nafunga kufuli,
Nafunga ndoa natawakali, naoa mke Muumini.
 
sokomoko we pongezi, uamuzi wa busara
umeepuka uzinzi, kigori ukampura
wa dini na siyo mwizi, mzuri tabia sura
Tualike hata wali, nasi tuje sherekea!
 
sokomoko we pongezi, uamuzi wa busara
umeepuka uzinzi, kigori ukampura
wa dini na siyo mwizi, mzuri tabia sura
Tualike hata wali, nasi tuje sherekea!

Pongezi nazipokea ewe wangu mshirika
Uzinzi hauna maana na wengi wameathirika
Harusini wakaribishwa muda utakapofika
Wewe ndugu jamaa na marafiki kadhalika


We ni mkali mazee!

Mimi najaribu wapo malenga walofuzu
Siwezi jifananisha najifananisha na kauzu
Hao beti huzichezea huziona kama mzuzu
Ipo siku nitafuweza umalenga kuufuzu


Du!Leo kazi ipo!

Hana ukali ni dini kutimiza
Ama weye hujui HIV yaumiza?
Bora uoe utulie usijejiviza


Kila la kheri.

Amin nakuitikia ewe wangu sahib
Dua yako iwe nisipate masahib
Ndoa iwe tamu kushinda zabubu
Tuwe wema na wenye kuabudu
 
Salaamu zangu natuma, zifike kila mahali,
Tunaziomba rehema, za Mungu zituwasili,
Hapo siku ya Qiyaama, tuwe chini ya kivuli,
Nafunga ndoa natawakali, naoa mke Muumini.

Naoa mke Muumini, nafunga ndoa natawakali,
Mke aloshika dini, na kila siku kuswali,
Hijaab ipo kichwani, afunikae wote mwili,
Nafunga ndoa natawakali, naoa mke Muumini.


Sijatafuta uzuri, au yule mwenye mali,
Nimechagua tabia nzuri, alotulia akili,
Aloleleka vizuri, kidini na kiasili,
Nafunga ndoa natawakali, naoa mke Muumini.

Sikumtafuta kwa haraka, nijionyeshe kamili,
Zinifikie baraka, za Mola wangu Jalali,
Nitulie kwa hakika, tabia mbaya nibadili,
Nafunga ndoa natawakali, naoa mke Muumini.

Fadhila zake ni nyingi, uliza kila pahali,
Huo ndio ni msingi, wa maisha ya halali,
Ni kinga kwa mambo mengi, kwa madhambi mbalimbali,
Nafunga ndoa natawakali, naoa mke Muumini.

Kuoa ni utulivu, tumeshaona dalili,
Huyaondoa maovu, na mambo huwa sahali,
Hukufanya mtulivu, shida ikikukabili,
Nafunga ndoa natawakali, naoa mke Muumini.

Wajibu wangu tatimiza, tutakapokuwa wawili,
Tukikaa kuzungumza, na mambo kuyajadili,
Tutajaribu kueleza, tuelezane ukweli,
Nafunga ndoa natawakali, naoa mke Muumini.

Niwe msimamizi, kwa mali na kila hali,
Ayaonyeshe mapenzi, maneno kama asali,
Katika masimulizi, sitosema kwa ukali,
Nafunga ndoa natawakali, naoa mke Muumini.

Mungu atupe watoto, hao ni rasilmali,
Mke ni mama watoto, awe mwema na mkali,
Awatazame watoto, wasikuwe kijahili,
Nafunga ndoa natawakali, naoa mke Muumini.

Mke ni nguzo nyumbani, kama vile matofali,
Na mume ndio rubani, huona yaliyo mbali,
Kamba ya Mungu tuishike, ibada iwe awali,
Nafunga ndoa natawakali, naoa mke Muumini.

Mungu Watunze vigoli, pamoja na wanawali,
Wawe kama wa awali, kama zama za Rasuli,
Nimemaliza kauli, hapa nafunga kufuli,
Nafunga ndoa natawakali, naoa mke Muumini.

Kwanza nikupe pongezi, bibi huyo kumpata
Kwa wako huu utenzi, yaonyesha umekita
Upunguze matembezi, kwani chema ushapata
Ukishaifunga ndoa, zipuyo siache wazi!

Sokomoko uziache, 'kishaingia ndoani
Na ukware uuache, hata 'kiwa mkoani
Bibie usimuache, hasa kama muumini
Ukishaifunga ndoa, bibiye umuheshimu

Watoto mkijaliwa, muwalee kwa imani
Ununue na maziwa, shibe ilete amani
Elimu kizawadiwa, wawe ka' Kofi Anani
Ukishaifunga ndoa, majukumu sikimbie.

Tena ninakuhusia, talaka usiipende
Hata kama ni wosia, haichanui mtende
Kwa zake hizo ghasia, wanao usiwatende
Ukishaifunga ndoa, wa pembeni siwaone.

Mwenzio bado mseja, sijafanya uamuzi
Sasa naiona haja, nisomapo hu' utenzi
Nitalipa na mkaja, kishafanya uamuzi
Nami najipanga pia, kutafuta muamini.

 
Kwanza nikupe pongezi, bibi huyo kumpata
Kwa wako huu utenzi, yaonyesha umekita
Upunguze matembezi, kwani chema ushapata
Ukishaifunga ndoa, zipuyo siache wazi!

Sokomoko uziache, 'kishaingia ndoani
Na ukware uuache, hata 'kiwa mkoani
Bibie usimuache, hasa kama muumini
Ukishaifunga ndoa, bibiye umuheshimu

Watoto mkijaliwa, muwalee kwa imani
Ununue na maziwa, shibe ilete amani
Elimu kizawadiwa, wawe ka' Kofi Anani
Ukishaifunga ndoa, majukumu sikimbie.

Tena ninakuhusia, talaka usiipende
Hata kama ni wosia, haichanui mtende
Kwa zake hizo ghasia, wanao usiwatende
Ukishaifunga ndoa, wa pembeni siwaone.

Mwenzio bado mseja, sijafanya uamuzi
Sasa naiona haja, nisomapo hu' utenzi
Nitalipa na mkaja, kishafanya uamuzi
Nami najipanga pia, kutafuta muamini.


Shukrani zipokee ewe wangu sahib
Nasiha zako nzuri tena za kishababi
Insha'Allah tazingatia namuomba Yarabi
Mungu atuhitimishe kama babu na bibi

Sokomoko taziacha mapenzi kuongeza
Mungu atujalie pacha familia kuongeza
Nitainamisha macho wala sitakonyeza
Nimeamua kuoa uhuni kuutokomeza

Majukumu tayashika bila shaka na wasi
Watoto nitawalisha hata kama si mkwasi
Na elimu tawapatia iliyo bora kuliko sisi
Namomba Rahman anipe pumzi na nafasi

Nakuombea yalo mema usiku na mchana
Zikuepuke fitina kwa watu wenye khiyana
Akujaalie mke mwema kwa nia yako njema
Akuepushe lawama binaadamu si wema

Tafuta mke haraka ukijiona kamili
Utulie kwa haraka tabia mbaya ubadili
Ikufike baraka ya Mola wako Jalali
Funga ndoa tawakali oa mke muumini.

Usitafute uzuri, au yule mwenye mali,
Chagua tabia nzuri, alotulia akili,
Aloleleka vizuri, kidini na kiasili,
Funga ndoa tawakali, oa mke Muumini.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom