Habari zenu wana jukwaa
Poleni na majukumu na pilika pilika za wiki nzima
Nina swala moja linalonisumbua sana kichwa kwa sasa, na nimekuja kwenu kuomba ushauri wa jambo hili.
Mimi ni mwanaume, nina miaka 28 kwa sasa. Nimekuwa kwenye mahusiano ya muda mrefu kidogo wa takribani miaka nane na mpenzi wangu lakini naona mahusiano yenu yanafikia ukingoni.
Namshukuru Mungu nimefanikiwa kupata malezi ya wazazi wote wawili, lakini mwenzangu hajabahatika kupata malezi ya baba, namaanisha mpaka leo amebahatika kulelewa na Mama tu ingawa Baba yake yu mzima mpaka leo na kwa sababu ya kulelewa na Mama tu naona amelishwa sumu ya kumchukia mzazi wake wa kiume.
Mpenzi wangu huyu kwa sasa yupo chuo, ila mimi nipo mtaani nna ajira ambayo ukweli ni kwamba ndo chanzo changu cha kipato kinachonifanya niendelee kuishi hapa Dar es Salaam.
Toka tumeanza mahusiano, nilikua natamani sana nipate wasaa wa kuishi nae kwa muda kidogo kabla sijamuoa ili nipate kumfahamu mwenza wangu kiundani na Alhamdullilah nilipata wasaa wa kuishi nae mwaka jana kwa takribani miezi mitano nyumbani kwangu na nikapata kumfahamu kiundani kidogo.
Ukweli ni kwamba, Wazazi wangu ni watu waliokulia vijijini kabla ya kuja mjini ukubwani kutafuta Maisha na hivyo. Wamenilea katika maadili mazuri ya kiafrika katika nyanja zote za Maisha na namshukuru Mungu kwa malezi yao.
Mwenzangu, Mama yake ni Mcha Mungu sana ila yeye yupo tofauti kidogo na tabia za Mama yake. Akiwa mazingira ya kwao, Mama ndo huwa anamhimiza kwenda Kanisani lakini anapoondoka mazingira ya Nyumbani huwa anaacha kabisa kwenda huko Ibadani na kama akienda ni Mara mojamoja tu. Mwenzangu huyu amekumbatia sana mila za Magharibi kama kuvaa sana suruali za kubana mpaka anakosa nguo za kwenda kanisani, wallpapers zake kwenye simu ni picha za nusu utupu kwa sana, akikaa kwa TV vipindi anavyoangaliaga ni dhahama tupu (Keeping up with Kardashians) mpaka unajiuliza anajifunza nini huku, Hapendi kabisa kusikia mazingira ya vijijini na ukitaka mkosane mwambie unapenda kuishi huko, atakwambia we kaishi huko mm siwezi kama Kuwasiliana WhatsApp ipo. Duuh! Hivi huyu anafaa kuwa mke kweli na anaweza kuishi nadhiri ya kuishi pamoja katika shida na Raha?
Ana hulka ya uvivu, kila kazi atataka mfanye wote akiamini haki sawa ni kazi zote za nyumbani mfanye wote, Ni mtu anayependa sana mikorogo ambayo kimsingi inapoteza rangi yake nzuri nyeusi ya asili, Nimeshajaribu kumkanya sana kuhusu hili na hata kutupa baadhi ya vipodozi vyake bila mafanikio, Marafiki zake wanaomzunguka ni walevi, wadangaji na mabinti wenye tabia chafu nyingi tuu, Na hili pia nimejaribu sana kumkanya ila huishia kusema wale ni marafiki tu na yeye ni mtu mzima anayejua nini anafanya hivyo hawawezi kumbadili tabia kwa namna yoyote ile.
Anapenda sana kula vyakula vya kisasa kama Chipsi na Ice Cream na sio vyakula vya kiafrika. Ugali hapendi kula na akila ugali ni lazima anywe na maziwa mgando la sivyo hataki kusikia ugali. Uvivu wake unanifanyaga nimuulize, " Hivi mama kwa uvivu wako huu, utaweza kuingia Leba, kujifungua kwa njia ya kawaida na kutoka salama kweli", kuamka mapema kwake ni ndoto, kwenye mazingira yake ya chuo huko hata nguo zake binafsi anafuliwa, Sasa huyu ni mke au Slay Queen?
Nimeahidi kumuoa akimaliza chuo, ila kila nikiwaza tabia zake naona hafit kuwa mke na Mama Bora wa familia na kwa maana hiyo nafikiria kumuacha na kuanzisha mahusiano mengine. Je niko sahihi kwenye hilii?
Naombeni ushauri wenu katika hili tafadhali
Poleni na majukumu na pilika pilika za wiki nzima
Nina swala moja linalonisumbua sana kichwa kwa sasa, na nimekuja kwenu kuomba ushauri wa jambo hili.
Mimi ni mwanaume, nina miaka 28 kwa sasa. Nimekuwa kwenye mahusiano ya muda mrefu kidogo wa takribani miaka nane na mpenzi wangu lakini naona mahusiano yenu yanafikia ukingoni.
Namshukuru Mungu nimefanikiwa kupata malezi ya wazazi wote wawili, lakini mwenzangu hajabahatika kupata malezi ya baba, namaanisha mpaka leo amebahatika kulelewa na Mama tu ingawa Baba yake yu mzima mpaka leo na kwa sababu ya kulelewa na Mama tu naona amelishwa sumu ya kumchukia mzazi wake wa kiume.
Mpenzi wangu huyu kwa sasa yupo chuo, ila mimi nipo mtaani nna ajira ambayo ukweli ni kwamba ndo chanzo changu cha kipato kinachonifanya niendelee kuishi hapa Dar es Salaam.
Toka tumeanza mahusiano, nilikua natamani sana nipate wasaa wa kuishi nae kwa muda kidogo kabla sijamuoa ili nipate kumfahamu mwenza wangu kiundani na Alhamdullilah nilipata wasaa wa kuishi nae mwaka jana kwa takribani miezi mitano nyumbani kwangu na nikapata kumfahamu kiundani kidogo.
Ukweli ni kwamba, Wazazi wangu ni watu waliokulia vijijini kabla ya kuja mjini ukubwani kutafuta Maisha na hivyo. Wamenilea katika maadili mazuri ya kiafrika katika nyanja zote za Maisha na namshukuru Mungu kwa malezi yao.
Mwenzangu, Mama yake ni Mcha Mungu sana ila yeye yupo tofauti kidogo na tabia za Mama yake. Akiwa mazingira ya kwao, Mama ndo huwa anamhimiza kwenda Kanisani lakini anapoondoka mazingira ya Nyumbani huwa anaacha kabisa kwenda huko Ibadani na kama akienda ni Mara mojamoja tu. Mwenzangu huyu amekumbatia sana mila za Magharibi kama kuvaa sana suruali za kubana mpaka anakosa nguo za kwenda kanisani, wallpapers zake kwenye simu ni picha za nusu utupu kwa sana, akikaa kwa TV vipindi anavyoangaliaga ni dhahama tupu (Keeping up with Kardashians) mpaka unajiuliza anajifunza nini huku, Hapendi kabisa kusikia mazingira ya vijijini na ukitaka mkosane mwambie unapenda kuishi huko, atakwambia we kaishi huko mm siwezi kama Kuwasiliana WhatsApp ipo. Duuh! Hivi huyu anafaa kuwa mke kweli na anaweza kuishi nadhiri ya kuishi pamoja katika shida na Raha?
Ana hulka ya uvivu, kila kazi atataka mfanye wote akiamini haki sawa ni kazi zote za nyumbani mfanye wote, Ni mtu anayependa sana mikorogo ambayo kimsingi inapoteza rangi yake nzuri nyeusi ya asili, Nimeshajaribu kumkanya sana kuhusu hili na hata kutupa baadhi ya vipodozi vyake bila mafanikio, Marafiki zake wanaomzunguka ni walevi, wadangaji na mabinti wenye tabia chafu nyingi tuu, Na hili pia nimejaribu sana kumkanya ila huishia kusema wale ni marafiki tu na yeye ni mtu mzima anayejua nini anafanya hivyo hawawezi kumbadili tabia kwa namna yoyote ile.
Anapenda sana kula vyakula vya kisasa kama Chipsi na Ice Cream na sio vyakula vya kiafrika. Ugali hapendi kula na akila ugali ni lazima anywe na maziwa mgando la sivyo hataki kusikia ugali. Uvivu wake unanifanyaga nimuulize, " Hivi mama kwa uvivu wako huu, utaweza kuingia Leba, kujifungua kwa njia ya kawaida na kutoka salama kweli", kuamka mapema kwake ni ndoto, kwenye mazingira yake ya chuo huko hata nguo zake binafsi anafuliwa, Sasa huyu ni mke au Slay Queen?
Nimeahidi kumuoa akimaliza chuo, ila kila nikiwaza tabia zake naona hafit kuwa mke na Mama Bora wa familia na kwa maana hiyo nafikiria kumuacha na kuanzisha mahusiano mengine. Je niko sahihi kwenye hilii?
Naombeni ushauri wenu katika hili tafadhali
