Nafikiri NIDA wanapaswa kuwajibika kwa uzembe na ndio pekee walipaswa kupewa ukomo wa muda sio wananchi

gimmy's

JF-Expert Member
Sep 22, 2011
3,283
3,274
Licha ya mazuri mengi yanayofanywa na Serikali yetu ya awamu ya tano lakini yapo mambo lazima Raisi wetu mpendwa anahitaji apate taarifa vizuri kupitia vyanzo vyake vinginevyo hawa wanaoitwa wanyonge watakuwa wananyongwa.

Hivi wananchi wakaidi kusajili namba za simu ili iweje? Nani yuko tayari simu yake ifungwe kwa sababu yakutosajili line ya simu? Kwanini wananchi hawahawa ambao leo wanaonekana wakaidi hapo awali waliitikia vizuri usajili wa line zao wakati wakutumia kitambulisho cha mpiga kura?

Wapeni wananchi namba za NIDA ndipo muwafungie waliokaidi kujisajili.Namba za NIDA hamtoi ili watu wajisajili halafu mnawapa muda wananchi mliowanyima namba za NIDA wasipojisajili mnawafungia line zao,hivi mnasubiri mpaka muambiwe kwamba mnachowafanyia wananchi mnawaonea?

NIDA wamesababisha usumbufu mkubwa sana kwenye utoaji wa vitambulisho.

Ni vema serikali ikatambua kwamba wananchi waliitikia wito kwenye uandikishaji wa vitambulisho vya uraia mwanzoni kabisa wakati zoezi hili lilipoasisiwa lakini vitambulisho vya waliowengi NIDA hawajawaletea,wapo wananchi waliorudia zoezi hili zaidi ya mara mbili pasipo mafanikio yoyote.
Hivi kwa haya nani ni mzembe?

Zoezi hili limesababisha watanzania wanadamka alfajiri saa nane kuwahi foleni za namba za NIDA na baada ya zoezi wanafuatilia hizi namba kwenye ofisi za vijiji wengine wanafanikiwa na wengine wanafeli.Hivi bado huyu raia aliyehangaika alfajiri anafungiwa line yake?

Wapo wananchi wengi ambao wamefuatilia namba za NIDA lakini wamepewa namba ambazo sio zao.

Serikali itambue kwamba kutokana na uzembe wa NIDA wananchi wengi wanasajiliwa namba zao za simu kwa msaada wa ndugu na jamaa zao jambo ambalo linapoteza maana halisi ya zoezi hili kwani kinachofuata ni watu kutumia line ambazo si zao.

Tunamuomba Mh Raisi afuatilie tena mwenendo wa zoezi hili kwani limegeuka adhabu kwa watanzania kwa uzembe wa NIDA.

Watanzania waadhibiwe kwa uzembe wao lakini kuadhibiwa kwa uzembe wa NIDA sio sawa.
 
Magufuli kanoresha utendaji serikalini na kurudisha nidhamu ya kazi sasa unataka NIDA wapewe muda wa nini? Acha uzembe unataka wakufate home kwako?
 
Yaani sisi wachunga ng'ombe tunajua sana fomula hiyo anaechelewesha mwendo anakua mbele anayeadhibiwa ni wa nyuma nida ni tatizo kubwa mnaandikisha na kupiga picha wew na mkeo mmoja kinakuja mwingine unarudia had unakata tamaa mwenyew waliotakiwa kupewa muda was mwisho ni nida sio raia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Magufuli kanoresha utendaji serikalini na kurudisha nidhamu ya kazi sasa unataka NIDA wapewe muda wa nini? Acha uzembe unataka wakufate home kwako?
Nina wasiwasi kama umesoma maelezo ya mtoa mada. Au la we bonge la mkurupakaji kisa una bando. Umeambiwa watu wamejiandikisha NIDA. Namba hawajapewa licha ya kufuatilia kila siku. Na bado adhab ya kufunga line inawalalia. Jaman, kuna ugum wowote hapo kuelewa au ndo wale kulishwa sana ugali tang utoton!. Hata hivyo serkali itapoteza zaid mapato, itaathiri mifumo ya miamala, uchumi itauua kwa mikono yake yenyewe. Mwananchi atapata njia mbadala serkal itashangaa.
 
Nina wasiwasi kama umesoma maelezo ya mtoa mada. Au la we bonge la mkurupakaji kisa una bando. Umeambiwa watu wamejiandikisha NIDA. Namba hawajapewa licha ya kufuatilia kila siku. Na bado adhab ya kufunga line inawalalia. Jaman, kuna ugum wowote hapo kuelewa au ndo wale kulishwa sana ugali tang utoton!. Hata hivyo serkali itapoteza zaid mapato, itaathiri mifumo ya miamala, uchumi itauua kwa mikono yake yenyewe. Mwananchi atapata njia mbadala serkal itashangaa.
Hawajapataje namba wakati utendaji serikalini umeboreshwa? au NiDA si sehemu ya serikali? nadhani wewe ndo umekurupuka
 
Magufuli kanoresha utendaji serikalini na kurudisha nidhamu ya kazi sasa unataka NIDA wapewe muda wa nini? Acha uzembe unataka wakufate home kwako?
Ngoja nikusamehe tu kwani kwa uandishi huu tatizo ni eidha uzembe wa wazazi hawakuwajibika kukupeleka shule, walikupeleka lakini kichwani hakuna kitu ama uzembe wa walimu wako.
Ukipata muda rudia kusoma nilichoandika vizuri.
 
Wananchi wengi hawana vigezo vya kupewa Kadi ya utambulisho wa Uraia.

Wengi hawana vyeti vya kuzaliwa wala karatasi za kuonesha majina au miaka yao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acha ubishi jomba, serikali kupitia NIDA imelifanya zoezi la usajili wa line za simu kuwa la adhabu kwa wananchi bila sababu za msingi.
Hapo mwanzo, nadhani mwaka 2014 NIDA walichukua raarifa za wananchi kwa kuwapitia majumbani.
Kipi kilichopelekea wajifungie kwenye kiofisi kidogo wakisubiri maalfu ya watanzania?
USHAURI. Serikali isitishe deadline ya usajili wa line za simu, kisha iwape deadline NIDA kumaliza zoezi la vitambulisho ili kuepusha usumbufu
Hawajapataje namba wakati utendaji serikalini umeboreshwa? au NiDA si sehemu ya serikali? nadhani wewe ndo umekurupuka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acha ubishi jomba, serikali kupitia NIDA imelifanya zoezi la usajili wa line za simu kuwa la adhabu kwa wananchi bila sababu za msingi.
Hapo mwanzo, nadhani mwaka 2014 NIDA walichukua raarifa za wananchi kwa kuwapitia majumbani.
Kipi kilichopelekea wajifungie kwenye kiofisi kidogo wakisubiri maalfu ya watanzania?
USHAURI. Serikali isitishe deadline ya usajili wa line za simu, kisha iwape deadline NIDA kumaliza zoezi la vitambulisho ili kuepusha usumbufu

Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe utakuwa wakala wa beberu na umetumwa kuchafua serikali yetu tukufu inayopiga kazi haijawahi kutokea si Tanzania wala duniani kote
 
Magufuli kanoresha utendaji serikalini na kurudisha nidhamu ya kazi sasa unataka NIDA wapewe muda wa nini? Acha uzembe unataka wakufate home kwako?

Mjinga mmoja wewe , yani nipange foleni since saa nane usiku nifatilie namba mwezi mzima then ufunge lain yangu kosa ni langu au la NIDA?
Katika watu 5 wapumbavu awakosekan na wewe ni mmoja wao


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Back
Top Bottom