Tanu Youthleague
Member
- Jun 18, 2012
- 14
- 3
Wanabodi kwa mara ya kwanza tangu CDM ianze kuwa na wabunge imekuwa ikishiriki vizuri katika vikao vya bunge na hasa uchambuzi wa bajeti. lakini mwaka huu imekuwa tofauti na imeonekana kuchuja sana na kati ya vigezo ni hivi
1. Makosa ya wazi katika hotuba ya maoni ya kambi ya upinzani ambayo imekuwa ikinadiwa kuwa ni bajeti mbadala. Makosa haya yalifichuliwa na mchumi daraja la kwanza Mwigulu Nchemba.
2.Katika kuonyesha kuzidiwa Tundu Lissu wakati wa kujadili bajeti aliinuka na kutaka kutoa taarifa. Taarifa yake ikaonyesha kukana zile propaganda zilizokuwa zimefanikiwa kuwa huwa wanatoa bajeti mbadala. Lissu akasema ni makosa kuita maoni ya upinzani bajeti mbadala. Spika alikubali lakini swali je hii maana yake nini? Ukipekua hansard wabunge wengi wa chadema wakiwamo viongozi wametamka mara nyingi neno bajeti mbadala-umakini uko wapi? Kumbe wakizidiwa wanatafuta ukweli halisi.
3. Hicho kinachoitwa mabadiliko ya baraza kivuli la mawaziri ni kituko (ni baraza dhaifu). Tafakari eti hii ndiyo timu ya serikali mbadala; Peter Msigwa (mropokaji) vs Hamis Kagasheki (Ambassador, Senior Diplomat); Said Arfi (mwanasiasa asiye na utalaamu wowote) vs Harrison Mwakyembe (Mwanasiasa na mwanataaluma mahiri na mzalendo); Wenje (mtengeneza fitina wa Mbowe-Nyamagana dhidi ya Chagulani) vs BM (Bernard Membe- gwiji wa diplomasia, mzalendo na mwanadekorasia aliyewalisha ugali Chadema (Lema, Millya) walipokwenda jimboni kwake Mtama. Mnyika (zero knowledge katika rasilimali za nishati (gesi) Vs Sospeter Muhongo (Profesa, mwanajiolojia-Lissu anamjua vizuri). Ni kwa ufupi tu. Pointi hapa ni kwamba kwa sababu Chadema ina watu dhaifu katika BARAZA KIVULI basi wangechukua wabunge wengine wa upinzani-ubinafsi umewaponza. Waziri kivuli ninaye mkubali ni Lissu (Katiba na Sheria).
4. Katika Bunge hili imedhihirika Chadema hakuna wanachokisimamia kwa dhati bali ni usanii. Hii inathibitishwa na mwenyekiti wao Mbowe kupinga matumizi ya magari yakifahari (V8) yanayogharimiwa na fedha za umma lakini sasa amelichukua gari alilokataa. Hawa hawa ndiyo wanaojidai kupinga matumizi makubwa yasiyo ya lazima lakini nyongeza ya mishahara ya wabunge maana yake ni nyongeza ya matumizi (ya kibajeti), je, hoja yao ya fedha nyingi zitengwe kwenye miradi ya maendeleo ina ukweli?
5. Wamepinga bajeti ya serikali ambayo ndani yake Waziri wa Fedha ameahidi kusaidia wakulima wa pamba kwa kuvipa unafuu wa kodi viwanda vya nchini vinavyozalisha kwa kutumia pamba ya ndani. Hii maana yake soko la pamba ya ndani litakuwa na uhakika bila kuyumbishwa na soko la dunia. Siasa za kanda ya ziwa ni zao la pamba, serikali itapendekeza kusaidia wakulima wa pamba, wao wanapinga bajeti. Hapa wamechemsha, na mchesho itakuwa umeiva vizuri na kunukia pale pamba itapokuwa na soko la uhakika la ndani kama waziri alivyoahidi. Watasikia kanda ya ziwa muda si mrefu.
6.Wameshindwa kutekeleza kwa vitendo, kwa mwaka wa pili mfululizo kuonyesha uchambuzi wa kibajeti kuwa wanaweza kutoa elimu bure (shule ya msingi hadi form 6) kama alivyoahidi Slaa kwenye ilani yao, lakini pia wameshindwa kuainisha namna uchambuzi wao wa kibajeti unavyoweza kushusha bei ya saruji ili iuzwe kwa elfu tano kama alivyoahidi Slaa au angalau pungufu ya elfu 10.
itaendelea
1. Makosa ya wazi katika hotuba ya maoni ya kambi ya upinzani ambayo imekuwa ikinadiwa kuwa ni bajeti mbadala. Makosa haya yalifichuliwa na mchumi daraja la kwanza Mwigulu Nchemba.
2.Katika kuonyesha kuzidiwa Tundu Lissu wakati wa kujadili bajeti aliinuka na kutaka kutoa taarifa. Taarifa yake ikaonyesha kukana zile propaganda zilizokuwa zimefanikiwa kuwa huwa wanatoa bajeti mbadala. Lissu akasema ni makosa kuita maoni ya upinzani bajeti mbadala. Spika alikubali lakini swali je hii maana yake nini? Ukipekua hansard wabunge wengi wa chadema wakiwamo viongozi wametamka mara nyingi neno bajeti mbadala-umakini uko wapi? Kumbe wakizidiwa wanatafuta ukweli halisi.
3. Hicho kinachoitwa mabadiliko ya baraza kivuli la mawaziri ni kituko (ni baraza dhaifu). Tafakari eti hii ndiyo timu ya serikali mbadala; Peter Msigwa (mropokaji) vs Hamis Kagasheki (Ambassador, Senior Diplomat); Said Arfi (mwanasiasa asiye na utalaamu wowote) vs Harrison Mwakyembe (Mwanasiasa na mwanataaluma mahiri na mzalendo); Wenje (mtengeneza fitina wa Mbowe-Nyamagana dhidi ya Chagulani) vs BM (Bernard Membe- gwiji wa diplomasia, mzalendo na mwanadekorasia aliyewalisha ugali Chadema (Lema, Millya) walipokwenda jimboni kwake Mtama. Mnyika (zero knowledge katika rasilimali za nishati (gesi) Vs Sospeter Muhongo (Profesa, mwanajiolojia-Lissu anamjua vizuri). Ni kwa ufupi tu. Pointi hapa ni kwamba kwa sababu Chadema ina watu dhaifu katika BARAZA KIVULI basi wangechukua wabunge wengine wa upinzani-ubinafsi umewaponza. Waziri kivuli ninaye mkubali ni Lissu (Katiba na Sheria).
4. Katika Bunge hili imedhihirika Chadema hakuna wanachokisimamia kwa dhati bali ni usanii. Hii inathibitishwa na mwenyekiti wao Mbowe kupinga matumizi ya magari yakifahari (V8) yanayogharimiwa na fedha za umma lakini sasa amelichukua gari alilokataa. Hawa hawa ndiyo wanaojidai kupinga matumizi makubwa yasiyo ya lazima lakini nyongeza ya mishahara ya wabunge maana yake ni nyongeza ya matumizi (ya kibajeti), je, hoja yao ya fedha nyingi zitengwe kwenye miradi ya maendeleo ina ukweli?
5. Wamepinga bajeti ya serikali ambayo ndani yake Waziri wa Fedha ameahidi kusaidia wakulima wa pamba kwa kuvipa unafuu wa kodi viwanda vya nchini vinavyozalisha kwa kutumia pamba ya ndani. Hii maana yake soko la pamba ya ndani litakuwa na uhakika bila kuyumbishwa na soko la dunia. Siasa za kanda ya ziwa ni zao la pamba, serikali itapendekeza kusaidia wakulima wa pamba, wao wanapinga bajeti. Hapa wamechemsha, na mchesho itakuwa umeiva vizuri na kunukia pale pamba itapokuwa na soko la uhakika la ndani kama waziri alivyoahidi. Watasikia kanda ya ziwa muda si mrefu.
6.Wameshindwa kutekeleza kwa vitendo, kwa mwaka wa pili mfululizo kuonyesha uchambuzi wa kibajeti kuwa wanaweza kutoa elimu bure (shule ya msingi hadi form 6) kama alivyoahidi Slaa kwenye ilani yao, lakini pia wameshindwa kuainisha namna uchambuzi wao wa kibajeti unavyoweza kushusha bei ya saruji ili iuzwe kwa elfu tano kama alivyoahidi Slaa au angalau pungufu ya elfu 10.
itaendelea