Wild Flower
JF-Expert Member
- Jul 20, 2023
- 844
- 1,604
Nabii Mkuu wa Kanisa la Ngurumo ya Upako Dkt. Geordavie ametoa mchango wa shilingi Milioni 50 za Kitanzania kwa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Arusha kwaajili ya kuwezesha Kampeni za Mgombea Urais wa Tanzania Samia anayetarajiwa kuwa na kampeni za Uchaguzi Mkuu Mkoani Arusha tarehe mbili mwezi Oktoba, 2025.
Geordavie amekabidhi fedha hizo kwa Katibu wa CCM Mkoa wa Arusha, Musa Matoroka kwa niaba ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa kwenye Ofisi za CCM Mkoani Arusha, akimtakia kheri pia Samia kwenye kampeni zake zinazoendelea kwenye Mikoa mbalimbali ya Tanzania pamoja na kukishukuru CCM kwa kumpa fursa ya kuchangia kampeni hizo!
Geordavie amekabidhi fedha hizo kwa Katibu wa CCM Mkoa wa Arusha, Musa Matoroka kwa niaba ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa kwenye Ofisi za CCM Mkoani Arusha, akimtakia kheri pia Samia kwenye kampeni zake zinazoendelea kwenye Mikoa mbalimbali ya Tanzania pamoja na kukishukuru CCM kwa kumpa fursa ya kuchangia kampeni hizo!