SMU
JF-Expert Member
- Feb 14, 2008
- 9,613
- 7,901
Mkono atoboa siri za Zitto
Posted Jumanne,Januari7 2014 saa 24:0 AM
Zitto, mchana anamtuhumu Mkono kuwa fisadi, jioni anaenda kukodi gari kwake!
>> Hivi tangu 2008 mpaka sasa 2014, huyu "MZALENDO wenu ZITTO" kalipa kodi ya kukodi gari kwa NIMRODI MKONO kiasi gani?
Unganisha na hili ndio picha inakuwa "clear" zaidi:
.Kwa kweli sakata la IPTL kwa muda mrefu limekuwa likitutia kichefu chefu sisi Wafanyakazi wa TANESCO hasa pale tunapomuona Mwanasheria anayeitetea TANESCO katika kesi hii ya IPTL akichota mabilioni ya fedha zetu!.
Mwanasheria wa TANESCO ambaye ni Nimrod Mkono amekuwa akitumia fedha nyingi kila kukicha lakini hadi sasa TANESCO haijawahi kushinda kesi hiyo ambapo tangu mwaka 2008 Mkono alikuwa akitumia sh bilioni kumi kila mwaka na hadi ilipofikia mwaka 2013 alikuwa ametumia fedha sh bilioni 52. Serikali imekwisha mlipa shilingi bilioni 35 na zilizobaki zimelipwa na TANESCO.
Sasa kwenye mgogoro unaoanza ni pale alipokuja Waziri Sospter Muhongo na katibu Mkuu Eliakim Maswi ambao pamoja na kwamba wanatoka Mkoa mmoja wa Mara lakini walimpinga wazi wazi bila kuficha kwamba hawapo tayari kuona akiendea kutafuna fedha za TANESCO namna hiyo na kusisitiza kutompatia kazi hiyo tena ya kuitetea TANESCO na kwamba Wanasheria wa TANESCO na wa Wizara wafanye kazi hizo wenyewe kwani gharama ni kubwa sana. Kama watu wanaweza kufanya tathmini ya haraka haraka au uchunguzi wa kawaida tangu Mwanasheria huyu asimamishwe kufanya kazi na TANESCO mambo mengi yamekuwa yakizushwa pasopo na maana wala msingi wowote mbona Mkono wakati anatafuna fedha za TANESCO suala la IPTL lilikuwa kimya
"Inauma Sana" ...... by mizambwa wa JF