Nabaguliwa kisa dini na kabila

Nabaguliwa kisa dini na kabila

wasabato na wayahudi ni mbingu na ardhi. kwanza wayahudi hawaamini kama yesu alikuja duniani. halafu pia sisi wakubwa zetu ni wakatoliki, kwa kua tulitoka katika ukatoliki... tukaitwa waasi na kuwindwa ulaya nzima, wengine kadhaa wakiuliwa kikatili na wengi wakikimbilia amerika ambayo ilikua na misingi ya uhuru wa kuabudu. tatizo hujasoma na kuvichambua hivi vitu, vipo wazi katika biblia na katika vitabu vya historia

Wasabato na Wakatoliki wapi na wapi? Labda unatafuta tu credits kwa kujiambatanisha. Nyinyi ni Wafarisayo na Yesu alipata shida sana na nyinyi. Kama mliamua kuishi kama Walawi, mbona basi nisione mkitoa sadaka za kuteketeza?

Wakatoliki tunakula Kambale na Kitimoto
 
Samahani kwa maoni yangu..il hamna lolote wewe tafuta mijihela.
I mean struggle and get really loaded....
Haayo ubaguzi maneno tuuu,sema umaskini tuu unasumbua..
Waswahili husema..penye udhia,rupia hutiwa njiani.....
Adios man..!
 
Mimi ni kijana wa kikurya afu msabato sijawahi kukataliwa kwa misingi hiyo japo wanauliza eti nyie wakali majibu hapohapo ina maana nyie wachaga wote ni wezi na majambazi? Inamaana kila mzaramo ni kiruka njia? Huo ni mtazamo uliopitwa na wakati ni kweli kulikuwa na tamaduni mbaya za kukeketa sio wakurya tu hata makabila mengine hapa Tanzania hata nchi nyingine za Afrika kusini bado wanakeketa,kupiga wanawake kumepitwa na wakati siku hizi watu wako bize kimaisha zaidi hayo mambo yalikuwa zamani wakurya tuko civilized bana,je mliosoma huko vyuoni mtakubaliana na mimi kuwa wakurya ni vipanga kwenye masomo wako bright,pia wakurya ni viongozi huko mashuleni na vyuoni? Mkurya hapendi mwenzake aonewe yuko radhi kukupigania hata kama hakujui, wakurya ni mashujaa na wachapa kazi,wapi unamwona mkurya mzembe au goi goi,Mkurya amepigania nchi ya Tanzania wakati wa Mvamizi Idd Amini,acheni kupotosha watu nani alifanya kazi Musoma akabaguliwa? Mbona sisi sio wabaguzi!!Nauliza swali,kila kukicha unasikia matukio ya kikatili kila kona Tanzania hayo yote wanafanya wakurya?
Huyu jamaa aliyeleta huu uzi kasema yeye sio mkurya sasa kwanini analeta madhaifu ya kuachwa na wachumba mkurya hayuko hivyo hata kidogo,sifa ya mkurya ni kwamba mwanamke akimkubalia tu kosa hamwachi hata kama ana shida gani,anadhibiti ndoa vilivyo hususani kitandani mwanamke haoni hata haja yaku-cheat kamapenzi wamekuwa kwa kula vyakula vya asili n.k
 
foolish age... wow!

Shida yako hujitambui, na hiyo ndio sifa kubwa ya FOOLISH AGE. Hebu angalia hii statement yako

sina uhakika kama nitakuja kupenda tena, ni ubaguzi ... ubaguzi tu:shut-mouth:


Haya ni maneno ya watoto. Mwanaume haishi kwa ridhaa ya moyo wa mwanamke. Bado hujakua, unausikilizia uchi kiasi kwamba unaamini huwezi kuishi bila huyo mwanamke. Kinachokuathiri ni upweke-moyo wa kitoto na sio mapenzi.

Ungekuwa umekomaa, usingesikitika kwa ndugu wa huyo mwanamke kukubagua, bali ungeshukuru kuwa umepata fursa ya kuwabaini mapema kabla hujaingia kwenye mahusiano.

Cha pili, utoto wako umeshindwa kukupa nafasi ya kubaini kuwa; mwanamke anayekuwa twisted na mawazo ya familia yake hafai kuwa mke.

Sasa we rukaruka na kejeli ukadhani mi umri wako, mi najua madogo huwa wanawaza nini na ndio maana umeanza kusema eti baada ya miezi sita umezama kwa mchaga, nini hiyo kama sio balehe?
 
e

tatizo sio dini, tatizo ni true love

Dini nayo ni swala la muhimu ili kuzuia maumivi ya baadae kwa sababu ya dini . kumbadili mwenzio kutoka dini yake kuja kwenye dini yako mara nyingi huleta migogoro ya kifamilia na tukumbuke ndoa zinazo tambulika kwa mungu ni za kidini na wala sio za selekari bado kuna umuhimu wa kutafuta mwenza wa dini moja ili kuondoa tafaruku za kifamilia
 
Huo ndo ukweli unaokabiliana nao japo ni mchungu na huwezi kulazimisha iwe kama unavyotaka, unajua maishani kuna mambo mengine yanafanywa magumu sana japo sio magumu. Lakini wewe usikate tamaa na ukitaka KUPENDA KWANZA JUA KWA HAKIKA MSIMAMO wa huyo umpendaye kuhusu masula hayo mawili. Inagawa yeye anaweza asiwe na shida lakini akashawishiwa na ndugu zake kama yule wa kwanza. Lakini uskate tamaa utapata wa kwako tu
 
Na wewe kama unampenda siunahama tu kwani Sabato nini bana.Ila kama humpendi baki hapo ulipo
 

@Fidel80
. Katika agano jipya Yesu anasema ktk Mathayo 5:17 Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii la sikuja kutangua bali kuitimiliza. Yesu hajaja kubadilisha chochote,Biblia ni Agano lake + jipya bila hivyo haijaitwa Biblia,wasabato wanasimamia maandiko ya Biblia sio watakavyo wanadamu.

Lakini nyie mmejikita kwenye agano la Kale
 
Pole kaka yangu.
Naomba unitumie private sms then ntakwambia nini cha kufanya.
Thanks.
 
Wasabato na Wakatoliki wapi na wapi? Labda unatafuta tu credits kwa kujiambatanisha. Nyinyi ni Wafarisayo na Yesu alipata shida sana na nyinyi. Kama mliamua kuishi kama Walawi, mbona basi nisione mkitoa sadaka za kuteketeza?

Wakatoliki tunakula Kambale na Kitimoto

@ mwana!
Hujui ulisemalo nakuombea kwa jina la Yesu ufunguke ujue maandiko kama wasabato! Haya maandiko yako agano la kale?

YESU ALIAMURU PEPO WAWAINGIE NGURUWE, KWELI NGURUWE HAWAFAI!
Mathayo 8:28-32, marko 5:1-20, luke 8:26-39 Walipofika pwani ya nchi ya wagerasi inayoelekea Galilaya alikutana mtu mtu mmoja mwenye pepo hakuvaa nguo siku nyingi na hakukaa nyumbani ila makaburini,alipomwona Yesu alipiga kelele akasema kwa sauti kuu nina nini nawe Yesu,mwana wa Mungu aliye juu? Nakusihi usinitese,Yesu akamwuliza jina lako nani? Akasema jina langu Jeshi,wale pepo wakamsihi asiwaamuru watoke kwenda shimoni,wakamsihi awape ruhusa kuwaingia wale nguruwe,basi Yesu akawaamuru pepo wakatoka kwa mtu Yule wakawaingia wale nguruwe,nalo kundi la nguruwe liliteremka gengeni kwa kasi ,wakaingia ziwani wakafa maji.
 
@ mwana!
Hujui ulisemalo nakuombea kwa jina la Yesu ufunguke ujue maandiko kama wasabato! Haya maandiko yako agano la kale?

YESU ALIAMURU PEPO WAWAINGIE NGURUWE, KWELI NGURUWE HAWAFAI!
Mathayo 8:28-32, marko 5:1-20, luke 8:26-39 Walipofika pwani ya nchi ya wagerasi inayoelekea Galilaya alikutana mtu mtu mmoja mwenye pepo hakuvaa nguo siku nyingi na hakukaa nyumbani ila makaburini,alipomwona Yesu alipiga kelele akasema kwa sauti kuu nina nini nawe Yesu,mwana wa Mungu aliye juu? Nakusihi usinitese,Yesu akamwuliza jina lako nani? Akasema jina langu Jeshi,wale pepo wakamsihi asiwaamuru watoke kwenda shimoni,wakamsihi awape ruhusa kuwaingia wale nguruwe,basi Yesu akawaamuru pepo wakatoka kwa mtu Yule wakawaingia wale nguruwe,nalo kundi la nguruwe liliteremka gengeni kwa kasi ,wakaingia ziwani wakafa maji.

NGURUWE NI NAJISI!
Walawi 11:7 Na nguruwe kwasababu yeye ana kwato,ni mwenye miguu iliyopasuka kati,lakini hacheui,yeye ni najisi kwenu,msile nyama yao wala msiguse mizoga yao hao ni NAJISI KWENU.
Torati 14:8 Na nguruwe kwa kuwa amepasuliwa ukwato lakini hacheui huyu ni NAJISI KWENU msile nyama zao wala mizoga yao msiiguse.
Walawi 11:10 Na hao wote wasio na mapezi na magamba waliomo majini ni MACHUKIZO KWENU
Walawi 11:29 kenge mjusi hao ni NAJISI
Walawi 11:13 Kisha ndege hawa watakuwa MACHUKIZO tai,mwewe,kunguru,bundi,korongo.
 
I hate people wa hivyo wote mnaabudu Yesu mnatofautiana madhehebu tu nao ni tatizo.
Am sorry to say this dini/imani haina nafasi kwangu zililetwa na wazungu na waarabu kugawa watu.
Leo hii mimi amu muislam sababu nimezaliwa dar pwani ila ningezaliwa Mbeya au Bukoba ningekuwa mkristo.
Siku zote mahusiano ni uamuzi wa mtu those excuses are just rubbish

Nakaubaliana nawe kimantiki, lakini kijamii na hasa wazazi wetu na jamii inayotuzunguka inakuwa ngumu kukubaliana na wewe kuanzisha familia na mtu wa dini/kabila nyingine, na hii hupelekea hata ukatengwa na familia japo si moja kwa moja.

Nadhani inabidi kulinganisha jamii yako ilivyo na kuona madhara yanayoweza kukupata (kutengwa) kutokana na mitazamo yao, ikiwa wana mitazamo chanya dhidi ya dini/kabila tofauti bas sawa. Kila siku katika maisha mtu hawezi hata kukuwazia ww kuwa rafiki yake kwa kuwa tu mnatoka dini tofauti.
 
Lakini nyie mmejikita kwenye agano la Kale

Taja ni sehemu gani tumejikita katika agano la kale ili nikupe fungu linapoana kwenye agano jipya,narudia Yesu hakuja kutangua torati bali kuitimiliza soma hapa chini uone Yesu ananena kwenye agano jipya maneno yaliyosikika agano la kale.

Mathayo 5:21,Mmesikia watu wa kale walivyoambiwa,Usiue na mtu akiua itampasa hukumu
Mathayo 5:27,mmesikia kwamba imenenwa usizini,lakini mimi naawmbia kila mtu amtazamaye mwanamke kwa kumtamani amekwisha kuzini naye moyoni mwake. Hizo baadhi ya amri kumi kutoka agano la kale,kwa hiyo unamaanisha tuvunje amri kumi kisa ziko agano la kale?
 
Pole sana mkuu, time will heal machungu yako
 
Kusema ukweli Sabato ni Wakristo, lakini kidogo mna mambo magumu , na ndiyo maana mnahisi kubaguliwa.
Mambo kama yafuatayo ni ishu sana:
-Kutokula nyama
z
-Kutokunywa soda

-Kutokula baadhi ya samaki.

-kutokunywa chai na kahawa.

-kutopika wala kugusa chochote jumamoc.

-chakula cha jmosi kupikwa ijumaa.

-jua likizama ijumaa sabato ishaanza.

-mambo ya lesoni, pathfinderz, makambi etc

-hakuna sikukuu zozote za kikristo.

-hakuna vipindi maalum vya kanisa kama vile Majilio, Kwaresma, Ijumaa kuu na Jumatano ya majivu.

-masharti kama kutokutengeneza nywele kwa mwanamke, wakati mnajua MWANAMKE NYWELE.

-Kutumia na kuamini zaidi agano la kale kuliko jipya.

Kweli mdada anahitaji maamuzi magumu kabisa kuamua kuachana na mambo aliyozowea na kuwa msabato.
Dadaangu wa tumbo moja akiamua kuwa msabato nitamkubalia, lakn nitalia sana na machozi yataenda tumboni.
Ha ha ahaa haa mkuu umenifurahisha sana nyama wanakula ila sio zote hasa hasa yule mnaomwita noah .ni najisi!!
 
...kaka likuepukalo lina kheri na wewe...kuwa na subira, Inshaallah Mungu atakujaalia mke aliyepanga yeye na wepesi utatawala katika mambo yenu. Usiwe na wasiwasi.
salaam wanajamvi,
Leo nimeamua kuandika kuelezea umma namna udini na ukabila ulivyojengeka nchini, hususani katika mapenzi. Mimi ni mhandisi mhitimu wa chuo kikuu nina miaka 28. Mara ya kwanza kujihusisha na mahusiano ilikua mwaka 2006, wakati huo nikiwa form 6. Nakumbuka ilikua Dodoma, nilipokutana na mpenzi wangu huyo wa kwanza katika maisha yangu. Tulipendana sana, na tuliwekeana malengo na mipango mingi ambayo kwa asilimia kubwa tuliweza kkuitimiza.
Matatizo yalianza kuzuka mwaka 2007 huyu binti alipoenda chuo kusoma na mimi nikachagua kufanya kazi kwanza, kampuni flani hivi ya madini. Vikaanza visa kila kukicha , japo nilijaribu kumtimizia kila alichohitaji.....hatimaye aliamua nimwaga rasmi mwaka 2009
Nakumbuka nilimwaga machozi na kuchanganyikiwa. wakati huo nilikua nimejiunga na chuo , niko mwaka wa kwanza.... tulikua katika mitihani...nilifeli karibu nusu ya mitihani yote. ilinichukua miaka miwili kusahau kidogo kilichotokea.
Binafsi, sikuweza kuanzisha mahusiano na binti yoyote kwa kua katika nafsi yangu nilikua nampenda x wangu tu. wapo waliojaribu kunitega, relationships zingine zilivunjika ndani ya usiku mmoja.
Wakati nakaribia kumaliza mwaka wangu wa mwisho chuoni, mpenzi wangu wa zamani alirudisha mawasiliano na akanieleza sababu zilizosababisha aniache. akaniamabia ni kwa kua mimi ni mtu wa musoma , kwao sikubaliki. ati kuna dada yake aliwahi kupata mchumba mtu wa msoma akamsumbua sana, tangu siku hiyo ikawa nongwa kwao. sababu ingine akaniambia pia kwa kua mimi ni msabato.... ati kwao wasabato wanawachukulia kama walokole na wenye imani kali. akaniambia yuko tayari kurudiana na mimi iwapo tu nitaamua kubadili dini na kua mkatoliki kama yeye... ishu ya kabila atanitetea kwa mama yake na dada zake wawili (tena wote wahandisi, wasomi) ambao kila kukicha wamekua wakimpa semina za kutafuta mwanaume ambae ni mkatoliki na asiwe mtu wa musoma
Iliniuma sana, zaidi hata ya aliponipa kibuti mara ya kwanza. kwa kweli japo nampenda sana .. ishu ya kubadili dini nilimkatalia na ndio ikawa nimemkosa milele.
Baada ya miezi kadhaa, nilikutana tena na binti wa kichaga... mwanachuo, mhandisi wa fani sawa na yangu. katika urafiki wetu uliodumu kama miezi 6 , nikajikuta nimezama katika penzi lake na hapo ikabidi nimwambie ukweli mwanzoni mwa mwezi huu nia yangu kwake. yes , nilijua kuna kupata na kukosa.. na ni kweli, alikataa...akadai anafurahia sana urafiki wetu wa kawaida ..na nilipojaribu kumdadisi kama kuna kinachomzuia...story ikawa ile ile...kabila langu na dini yangu kwao havikubaliki....
uchungu niliopata siku hiyo siwezi simulia...nakumbuka nilienda slip way nikasimama na kushangaa bahari huku machozi yananitoka kwa zaidi ya masaa 6...
dini yangu, kabila langu imekua jinamizi kwangu.....nakereka zaidi na kauli kua nisubiri wangu anakuja.
nawashauri wote ambao mnabagua kwa udini na ukabila muache hizo mambo.. mnaumiza sana wengine. mpenzi wa kweli na mwenza wa maisha anapimwa kwa tabia na sio vigezo hivyo.
sina uhakika kama nitakuja kupenda tena, ni ubaguzi ... ubaguzi tu:shut-mouth:
 
Pole sana ndugu yangu ndo yale ninayosemaga kila siku mwanaume msomi wako ni yule asiesoma,kama killa aliesoma ataoa alyesoma mwenzake sasa wasiosoma wataolewa na nani?? wachana nao hao waliosoma oa haraka asiesoma wala hataangalia upuuzi huo,na hakika watakukumbuka milele mana hakuna atakae waoa wala hawatampata yule mwenye sifa wanazozitaka wao,kumpata mwanaume wa kuoa siku hizi ni kazi maisha magumu subiri kidgo tu watakukumbuka sana wakina wanakaribia kuzeeka na hakuna aliehata chumbia.
 
acha kuficha ukweli na unafiki...mimi mwenyewe ni mjaluo tena mkatoliki katika familia yetu kunawasabato wengi sana ila nataka niihakikishie jf wasabato ni wasumbufu sana na wabaguzi tena wakishajua wewe ni mvaticani watatumia hiyo nafasi kukudhoofisha na kukudhihaki....nawaunga mkono hao madada coz najua huyo jamaa kwa usabato wake alikuwa anawadhihaki ndio maana imekuwa raisi kwao kukimbia..nawajua kwasababu ni ndugu zangu.
 
Back
Top Bottom