Naanza kuona dalili ya serikali ya mseto

Naanza kuona dalili ya serikali ya mseto

Inakatisha tamaa mtu anaongea jambo muhimu tena baada ya kuangalia mbele,watu mnajitokeza kuchangia eti flani hafai,mmeanza kukubali nk silazima kuchangia kila kinachojadiliwa,tuangalie zaidi maslahi ya nchi
 
Serikali ya mseto sawa ila hatutaki kusikia hata harufu ya Ccm
 
Mi binafsi sihitaji serikali ya mseto na haya majuzi ya kijani...yaondoke yatuachie nchi yetu
 
Hatutaki, magufuli anatosha na amesema wazi majizi yaliyoiba ccm na kukimbia na kumtesa Lisa pesa walizoiba imekula kwao,hatutaki yasubili mahakama ya mafisadi,

Hivi wewe ni raia wa wapi?
 
hakuna serikali ya mseto kabisa, ccm haitokuwa rahisi kukubali kufanya kazi na wapinzani. Ccm watakuwa na wabunge wengi pia kutakuwa na uwamuzi wa rais kuunda serikali yake bila kuweka hata kiumbe mmoja wa upinzani.

Ccm wakipata wabunge 50 basi wachinje kuku
 
Ccm ikae pemben,imetuumiza kila idara...wale wez wa escrow ...eti wamepitishwa na chama cha kijani kugombea ubunge....hawakutakiwa kupitishwa kugombea ubunge tena...
 
lengo letu kina january makamba waje kuandamana mitaani ili wajue nini maana ya shida za wananchi.

ukichagua magufuli maana yake umeruhusu kina wema sepetu wawe wabunge wa vitu maalumu. kina makamba, riziwani wawe mawaziri. what a waste!!!
 
Kutokana na vuguvugu la siasa nchini naanza kuona dalili za serikali ya mseto na itakuwa either rais magufuli waziri mkuu mbowe au rais lowassa waziri mkuu magufuli.
Hii naamini inaweza ikawa serikali inayoweza kuwatumikia wananchi kuliko serikali zote zilizopita.
Naomba mungu tusifike hapo kwa vurugu bali kuwepo na mashauliano.

Sababu kubwa ni ccm nguvu yake kubwa imepunguwa kwa wananchi na ukawa nguvu yao imeongezeka kwa wananchi.

Pili, kutokana na ujio wa lowassa ukawa sera zao zitabadilika kutoka sera za ufisadi na watakuja na sera za maendeleo kwa wananchi ambazo zitawajenga kisiasa.

Tatu, magufuli ndio nguzo pekee ambayo ccm wamebaki nayo na anapendwa na wananchi na hata ukawa hawatapenda wampoteze bali watakuwa tayari kushirikiana nae.

Nne, hata ukawa wakishinda sio rahisi ccm wakakubali kirahisi zaidi itabidi waingie kwenye maridhiano.
kwa Hali halisi Nchi yetu imegawanyika sana , na tatizo tumegawanyika Kikanda, sioni jinsi watu wa kaskazini wakaweza kuishi na watu wa kanda ya ziwa, matusi yamezidi, na wakubwa hawakemei kwa kuwa na wasiwasi na misimamo ya vyama, hii ni hatari sana, Bahati Mbaya Hatuna njia ya kuzuia hiyo na sidhani kuna uwezekano wa serkalini ya mseto, Kama CCM ikishinda, lakini Kama ukawa ikishinda hiyo inawezekana, all in all tanzania ya umoja imeishia kwenye utawala wa kikwete
 
Tanzania Bara serikali ya mseto bado sana.
nadhani muhimu ni right conditions, na right conditions ni representation kwenye ubunge, naona kama stategically ukawa tumepotea, nia ilikuwa ni kuungana ili tupate nguvu ya kuweza kusimamisha watu kwenye majimbo yote mmoja mmoja, naona kama hii haikupangwa vizuri kwani kuna majimbo ambayo CCM. wamepata ubunge bila upinzani, this was a serious tactical mistake. pili hata sasa kuna majimbo ambayo ukawa , wana wagombea zaidi ya mmoja, hii ni lack of sight and imaturity, hatuoni mbele, ya tatu ushabiki ilioletwa baada ya lowassa kuja upinzani, hii haija kaa vibaya, ila kutokana na poor resources, tumesahau kuwa representation kwenye bunge ndiyo key pre requisite , kwani hata lowassa akishinda bila kuwa na majority bungeni ni kazi bure, nne mtaji wa akiba, CCM wameuweka zanzibar, wameongeza majimbo with a direct fear ya majimbo watakayo poteza bara, au proportinate na majimbo watakayopoteza bara, kiuhalisia ina maana hata wakishindwa bara, au wakapungukiwa wabunge bara, watajazia zanzibar, i mean simple majority itapatikana ukiunga na wabunge wa zanzibar. hii hatuiooni, kwa sababu ushabiki wa lowassa umetutawala, na wala sioni kama nguvu kwa zanzibar inawekwa kivile, anyway tuone kwani sasa ni too late lakini, chenga twawala
 
Hakuna mseto wala dengu.kwanza katiba hairuhusu na hata ingeruhusu ccm kura zitatosha tu
 
kwa Hali halisi Nchi yetu imegawanyika sana , na tatizo tumegawanyika Kikanda, sioni jinsi watu wa kaskazini wakaweza kuishi na watu wa kanda ya ziwa, matusi yamezidi, na wakubwa hawakemei kwa kuwa na wasiwasi na misimamo ya vyama, hii ni hatari sana, Bahati Mbaya Hatuna njia ya kuzuia hiyo na sidhani kuna uwezekano wa serkalini ya mseto, Kama CCM ikishinda, lakini Kama ukawa ikishinda hiyo inawezekana, all in all tanzania ya umoja imeishia kwenye utawala wa kikwete
Mkuu hebu acha upuuzi wewe, watu wa kaskazini hawawezi kuishi na wa Kanda nyingine?????. Utakuwa hauishi Tanzania wewe, na unamezeshwa propaganda za CCM bila kuangalia uhalisia wewe. Hebu anza na hili swali, ktk selekali inayo maliza muda wake ccm ilikuwa na wabunge wangapi, madiwani wangapi, na selekali za mitaa kutoka kaskazini???......... Ujione ulivyo mpuuzi utakapo baini kuwa ccm ina kubalika kaskazini kuliko chama chochote.
 
Inasikitisha,habari hii,niliandika mimi kwa jina lililo hapo lakini maneno yamebadilishwa sikusema,eti serikali iwe rais magufuli,sikutaja majina,nilichokisema,nilishauri vyma vyote vya siasa vikae na kuangalia mbele ya uchaguzi,yaani waongee kuhusu uwezekano wa kuunda serikali ya mseto,sijui aliebadilisha maneno yangu alilenga nini, nashangaa hata baadhi ya post zangu zinakaa muda mchache na kuondolewa mwisho,nitapoteza uaminifu wangu kwa jf
 
Inakatisha tamaa mtu anaongea jambo muhimu tena baada ya kuangalia mbele,watu mnajitokeza kuchangia eti flani hafai,mmeanza kukubali nk silazima kuchangia kila kinachojadiliwa,tuangalie zaidi maslahi ya nchi

Vipi mbona unarusha ngumi hewani?
 
Back
Top Bottom