Na wewe kama una tabia hii acha

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,462
21,334
Matatani kwa wizi katika nyumba ya kulala wageni

5764722.jpg

Monday, June 20, 2011 4:20 PM
KIJANA mmoja aliyefahamika kwa jina la Jackson[ 22] mkaazi wa Manzese, amejikuta akiwa katika wakati mgumu baada ya kufanya wizi kuiba mipira ya kiume ’kondom’ boksi tatu aliyoikuta katika moja ya chumba cha nyumba ya kulala wageni iitwayo Moe gest
Kijana huyo inadaiwa wiki tatu zilizopita alipata tenda ya kufanya usafi katika nyumba hiyo ikiwa ni ombi lake alilopeleka la kujiingizia kipato cha kila siku ili aweze kunyikwamua kiuchumi

Juzi imedaiwa kuwa mmoja wa wahudumu waliokuwa zamu katika nyumba hiyo akiwa katika matayarisho ya kuandaa vyumba alidaiwa kumuuliza mfanya usafi huo kuwa bidhaa hiyo haioni pale sehemu wanapoweka na mfanya usafi huyo alikana kudai hakuona maboksi hayo ya miopira hiyo izuayo maambukizi dhidi ya maradhi ya ukimwi nay ale ya zinaa

Hata hivyo kwa kuwa ni utaratibu wa nyumba hiyo kuandaa mipira hiyo katika kila chumba ikiwa ni kuwajali wateja wao, muhudumu huyo alidaiwa kuripoti tukio hilo kwa mkuu wao wa kazi kuwa haoni mipira hiyo ya wateja

Hivyo mkuu huyo wa kazi katika nyumba hiyo ilidaiwa kumbana mfanya usafi huyo ili aeleze kama alihamisha mipira hiyo ama la

Hata hivyo ilidaiwa awali kijana huyo alikuwa akijiuma uma na kudai hakuhusika na wizi huo na alivyozidi kubanwa na kutishiwa kufukuzwa kazi ilidaiwa kijana huyo alikiri kufanya wizi wa mipira hiyo na kuomba msamaha kwa mkuu wake huyo wa kazi na kudai angeweza kurudisha kwa kuwa alimuuzia muuza duka ambaye alikuwa akimfahamu

Hivyo kijana huyo, alikuwa alishawasilisha maboksi mawili ya mipira hiyo kwa kumuuzia kwa bei nafuu na boksi moja alikuwa katika matayarisho ya kulichukua na kumuuzia tena mwenye duka hilo

Kutokana na kauli yake hiyo mkuu huyo wa kazi hakuwa na uvumilivu na kuanza kumpa kichapo hali iliyoshangaza watu wapitao njiani na kwa kupiga mayowe ya wizi hali iliyofanya NIFAHAMISHE ibaini kuwa kulikuwa na wizi katika nyumba hiyo
NIFAHAMISHE ilishuhudia mkuu huyo kumpa tuhuma kijana huyo kuwa alikuwa akitaka kuharibu biashara katika nyumba hiyo ya kulla wageni kwa kuwa wateja wao walishazoea kukuta mipira hiyo na kujizolea wateja lukuki kutokana na huduma hiyo

“Unataka nifukuzwe kazi, kwa ujinga wako, lazima nikupeleke kituo cha polisi ili upate adabu” alilama msimamizi mkuu wa wahudumu hao

Hadi nifahamishe inaondoka ene la tukio iliacha kutopatikana kwa maelewano kati yao na kijana huyo kutakiwa aonyeshe duka alipouza mipira hiyo kwa kuwa imedaiwa mipira hiyo ni ya gharama kidogo tofauti na ili inayouzwa kwa shilingi mia na hiyo kudaiwa inapatikana kwa shilingi elfu 3000 kwa kila pakti moja

 
Kuna wale wakienda mahotelini hasa nje ya nchi ama humu humu ndani wanafungasha ma taulo meupe ya watu pair nzima naamini mwaelewa na wewe kama una tabia hiyo acha ukiona hela yako aijatosha chukua mataulo yale futia viatu vyako vyeusi lakini si kuchukua wizi ausaiddii tabia hii iko kwa mabosi wengi sana nahisi taulo nyeupe kwao shida sijui
 
na waache kabisa!
Nimependa hyo ya kufuta viatu vyeusi kwa taulo jeupe ili hela iishe!..hahaha... Mkuu hapa u made my day...
 
Inawezekana hata breakfast ambayo hutolewa na baadhi ya hoteli huwa zinachakachuliwa na watu wenye vijitabia vya wizi kama huyu mwehu!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom