Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,462
- 21,334
Matatani kwa wizi katika nyumba ya kulala wageni | |
Monday, June 20, 2011 4:20 PM KIJANA mmoja aliyefahamika kwa jina la Jackson[ 22] mkaazi wa Manzese, amejikuta akiwa katika wakati mgumu baada ya kufanya wizi kuiba mipira ya kiume kondom boksi tatu aliyoikuta katika moja ya chumba cha nyumba ya kulala wageni iitwayo Moe gest | |
Kijana huyo inadaiwa wiki tatu zilizopita alipata tenda ya kufanya usafi katika nyumba hiyo ikiwa ni ombi lake alilopeleka la kujiingizia kipato cha kila siku ili aweze kunyikwamua kiuchumi Juzi imedaiwa kuwa mmoja wa wahudumu waliokuwa zamu katika nyumba hiyo akiwa katika matayarisho ya kuandaa vyumba alidaiwa kumuuliza mfanya usafi huo kuwa bidhaa hiyo haioni pale sehemu wanapoweka na mfanya usafi huyo alikana kudai hakuona maboksi hayo ya miopira hiyo izuayo maambukizi dhidi ya maradhi ya ukimwi nay ale ya zinaa Hata hivyo kwa kuwa ni utaratibu wa nyumba hiyo kuandaa mipira hiyo katika kila chumba ikiwa ni kuwajali wateja wao, muhudumu huyo alidaiwa kuripoti tukio hilo kwa mkuu wao wa kazi kuwa haoni mipira hiyo ya wateja Hivyo mkuu huyo wa kazi katika nyumba hiyo ilidaiwa kumbana mfanya usafi huyo ili aeleze kama alihamisha mipira hiyo ama la Hata hivyo ilidaiwa awali kijana huyo alikuwa akijiuma uma na kudai hakuhusika na wizi huo na alivyozidi kubanwa na kutishiwa kufukuzwa kazi ilidaiwa kijana huyo alikiri kufanya wizi wa mipira hiyo na kuomba msamaha kwa mkuu wake huyo wa kazi na kudai angeweza kurudisha kwa kuwa alimuuzia muuza duka ambaye alikuwa akimfahamu Hivyo kijana huyo, alikuwa alishawasilisha maboksi mawili ya mipira hiyo kwa kumuuzia kwa bei nafuu na boksi moja alikuwa katika matayarisho ya kulichukua na kumuuzia tena mwenye duka hilo Kutokana na kauli yake hiyo mkuu huyo wa kazi hakuwa na uvumilivu na kuanza kumpa kichapo hali iliyoshangaza watu wapitao njiani na kwa kupiga mayowe ya wizi hali iliyofanya NIFAHAMISHE ibaini kuwa kulikuwa na wizi katika nyumba hiyo NIFAHAMISHE ilishuhudia mkuu huyo kumpa tuhuma kijana huyo kuwa alikuwa akitaka kuharibu biashara katika nyumba hiyo ya kulla wageni kwa kuwa wateja wao walishazoea kukuta mipira hiyo na kujizolea wateja lukuki kutokana na huduma hiyo Unataka nifukuzwe kazi, kwa ujinga wako, lazima nikupeleke kituo cha polisi ili upate adabu alilama msimamizi mkuu wa wahudumu hao Hadi nifahamishe inaondoka ene la tukio iliacha kutopatikana kwa maelewano kati yao na kijana huyo kutakiwa aonyeshe duka alipouza mipira hiyo kwa kuwa imedaiwa mipira hiyo ni ya gharama kidogo tofauti na ili inayouzwa kwa shilingi mia na hiyo kudaiwa inapatikana kwa shilingi elfu 3000 kwa kila pakti moja |