St. Paka Mweusi
JF-Expert Member
- Sep 3, 2010
- 7,635
- 4,519
Nimekuwa nikifuatilia kwa ukaribu zoezi la kampeni na mbwembwe zote za wanasiasa.Mwaka huu inaonesha wapinzani kweli wamepiga hatua tofauti na huko nyuma.Swali langu kwa wana JF na wote wanaomsupport DR SLAA ni Je kampeni hizo ni kona zote za nchi au zinaishia makao makuu ya wilaya na mikoa tu. Maana kuna sehemu nyingi tu nchini kwetu wala hawajui kama kuna upinzani nchini na wanajua kuwa chama pekee ni CCM tu.Nasema hivyo kwa sababu binafsi nimekuwa mtumishi wa serikali kwa takriban miaka mitatu na nimeshiriki kusimamia uchaguzi wa 2005 na nilichokiona ni naona uchungu hata kukieleza.Na kama hawa watu hawafikiwi na kuelimishwa basi ushindi kwa wapinzani utachukua karibu miaka 500 kupatikana .NAOMBA KUWAKILISHA.