Japhari Shabani (RIP)
R I P
- Jan 16, 2007
- 721
- 176
Sasa unakaribia mwezi baada ya tume ya bunge kutoa taarifa kuhusu sakata la Jairo na wenzake kukusanya pesa kinyume cha sheria(Ufisadi)Ushahidi uliaanishwa wazi na mapendekezo ya hatua ya kuchukuliwa kwa wahusika.Ni mategemeo ya wengi yalikua kwa wahusika waliotajwa watajiuzulu au kufukuzwa kazi na kufikishwa vyombo vya sheria,lakini mpaka sasa hakuna chochote kilichotokea watu hao wanaendelea na shughuli zao kama kawaida,au na wao wanapashwa kupewa muda wajipime na kuchukua hatua?Au wanahitaji kuudiwa kamati ya kuwalazimisha kujivua nafasi zao?! Hii inatoa picha na funzo lipi kwa jamii?Kwanza ni mfano upi kwa wizara na taasisi za serikali zinazofanya ufisadi?Je pesa iliyotumika kwa kamati iliyoundwa kwa kuchunguza sakata hilo imepotea bure?!Kwani kuunda kamati ambayo maamuzi yake hayatekelezwi ni ufisadi juu ya ufisadi na kuwabebesha walipa kodi gharama zisizo na tija.MUNGU IBARIKI TANZANIA.