Mzumbe: Huu uchakachuaji wa ufaulu (GPA) unaleta kukosekana kwa usawa

Singida ndio home

JF-Expert Member
Feb 23, 2012
3,192
3,353
1580738238803.png


Hakunaga ubaguzi mbaya kama ule wa kujaribu kufanya kitu tofauti kionekane sawa na vingine vilivyofanana. Ni ubaguzi mkubwa kwa kukifanya hiki Chuo cha Mzumbe kionekane sawa na vingine wakati kuhalisia Chuo cha Mzumbe hakijafikia kitaaluma kama vingine.

Hapa sizungumzii maneno matupu naongea kwa ushahidi kabisa, kusomea Chuo cha Mzumbe ni rahisi mno mtu kufaulu ukilinganisha na vyuo vingine.

Wale tuliosoma vyuo tunajua kwamba Degree nyingi zina semester sita, kila semester ina masomo yake na kila semester mtu anapata GPA kulingana na ufaulu wake katika masomo aliyosoma kwenye semester nzima.

Vyuo vingi somo la field training huwa linakuwa limeunganishwa kwenye semester ya nne ya mwaka wa pili, semester hii ya nne inaweza ikawa na masomo ya darasani matano na la sita ndio field work inayofanyika chuo kikifungwa. Hivyo nayo field work inajumuishwa na masomo hayo matano ili kupata GPA.

Cha ajabu wenzetu semester nzima inatumika kufanya hiyo field work pekee, yaani hii semesta haina masomo yoyote zaidi ya field, mtu akipata A ya field basi kachukua marks 5 zote za kwenye GPA ya semester tofauti na vyuo vingine ambavyo hata ukipata A ya field work unaweza kujikuta umeambulia GPA ya 3.7 ikijumuishwa na masomo mengine.

Kupata A ya field work Mzumbe ni sawa na mtu aliesoma UDSM, IFM, IAA Arusha, TIA, n,k kupiga “A” masomo yote matano kwenye semester nzima kitu ambacho ni nadra sana.

Hali hii inachangia mhitimu apate GPA ya juu kuliko wa vyuo vingine na hata kuwa na uhakika zaidi wa kupata Second Upper Class kuliko wa vyuo vingine kama uonavyo hapa chini.

Nadhani suluhisho la kuleta haki ni kukifanya hiki chuo kiwe na semester tano, hio field ijumuishwe na masomo mengine ya semester ya nne, Haiwezekani mtu anakula GPA ya 5 kirahisi rashi yupo field wakati wenzake wanapambania hio GPA darasani.
 
Nimekutana na wahitimu wengi wa mzumbe na hiyo udsm yaani ni sifuri tupu!

Huwa najiuliza, kama hawa ndio "cream of the nation", sijui huko kwingine kuna hali gani!

Daktari mwenyewe ambaye tunaambiwa ni waziri wa elimu na falsafa yake uchwara hawezi angalau kuongea maneno mawili yakaeleweka!

"Cream of the nation".... hahahaaaaaaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Elimu biashara mkuu hasa kwenye hizi nyakati za kupenda sifa kuliko chakula..

Pia hiyo ni fursa waache waendelee na huo utaratibu coz hata huko kwingine wahitimu wao ukiwaweka na wahitimu wa mzumbe watakuwa sawa.

Ila mkuu sijakuelewa ukisema semister ziwe tano kwamba hiyo field ndo waesabie kama semister ya sita au vipi mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vyuo vyote vipo sawa, GPA hazioneshi sana uwezo halisi Wa mtu mfno Mzuri ni maofsn. Kuna watu sana GPA kubwa matokeo madogo, na kuna wenyewe GPA ndogo matokeo makubwa. Cha msingi gamba, ukiwa na la chuo chochote fresh tu
 
Mzumbe sio Chuo kikuu rahisi kama ulivyoandika.
Hiyo field work sio tafsiri ya kwamba Mzumbe ni Chuo rahisi na ukiona mtu kapata GPA kubwa Mzumbe basi fahamu kichwani yupo vizuri.

Kwa waliosoma Chuo kikuu Mzumbe wanafahamu Shule ya pale ilivyo ngumu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ugumu uko wapi mkuu, mbona ni chuo cha kawaida kabisa, kwa mfano mdogo tu nikichukulia kozi ya accounting vyuo vingi ni masomo 35 ila mzumbe ni masomo 25 tu

, hio field wanayoifanya november mpaka januari inambeba hata kilaza kwenye gpa, vyuo vingine hii field hata ukigonga "A" bado inajumuishwa na masomo ya ziada matano ili kupata gpa.

mitihani inafanyika wiki 3 mzumbe wakati vyuo vingine ni ndani ya siku 5 ni bampa to bampa mkianza pepa ni kila siku, Nakumbuka wanafunzi wengi wa hiki chuo niliosoma nao CPA walikuwa wanalalamika ratiba ya cpa kufanya masomo mengi ndani ya siku 4 tu.

Ugumu utoke wapi aisee, Labda kama waaolalamika ni vilaza
 
Vyuo vyote vipo sawa, GPA hazioneshi sana uwezo halisi Wa mtu mfno Mzuri ni maofsn. Kuna watu sana GPA kubwa matokeo madogo, na kuna wenyewe GPA ndogo matokeo makubwa. Cha msingi gamba, ukiwa na la chuo chochote fresh tu
Mkuu hivi huujui umuhimu wa gpa au, kuna baadhi ya kazi bila kufikisha gpa ya 3.5 huwezi kuomba, hapa ndipo huu uchakachuaji unapofaidisha wahitimu wengi wa mzumbe,
 
Elimu ya Tanzania ni ya kukariri ili kufaulu mtihani tu. Masuala ya GPA sio kipimo rasmi wa uwezo wa mtu, maamuzi ya kubania GPA ni maprof kuwa roho mbaya ya wivu kuona watoto wa wenzao wakifaulu.
Tanzania toka 1961 mpaka leo hakuna cha msomi, mtaalam, cream, lotion wala TO. Hao wote ni kukariri, inabidi mfumo wa elimu urekebishwe tusome kwa kiswahili ili tuelewe kinachofundishwa.


Ngoja niendelee kukariri vitini hapa.
 
Mzumbe sio Chuo kikuu rahisi kama ulivyoandika.
Hiyo field work sio tafsiri ya kwamba Mzumbe ni Chuo rahisi na ukiona mtu kapata GPA kubwa Mzumbe basi fahamu kichwani yupo vizuri.

Kwa waliosoma Chuo kikuu Mzumbe wanafahamu Shule ya pale ilivyo ngumu.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nani alikwambia kuwa chuo kikiwa "kigumu" ndio elimu bora?

Huu ushamba wa watanganyika ni unbelievable!

Ndio maana tumefuga "maprofesa" yanayokariri vitini vya nyambari nyangwine tu lakini hawawezi kuzalisha chochote!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Natafakari tu,

He? Unatafuta wingi wa masomo ama ubora wa kinacho zalishwa ama vyote viwili?

Inawezekana uko sahihi mahala, lakini nilitamani pia 'utuaminishe kwa kontenti za kozi husika (sambamba na vimeng'enywa) vilivyo ndani ya kila somo.

Zaidi usiandike kwa mihemuko, lazima tujifunze kwa kuheshimu tofauti zetu.

Aidha, ninacho fahamu mimi, Serikali kupitia wizara ya Elimu, hufanya mapitio ya kozi zote vyuoni ili kuona kama zina kidhi soko na mahitaji ya Walaji (waajiri).

Nadhani bado ipo haja ya kutafiti zaidi hats hiyo unayo iita field moja. Inawezekana ni zaidi ya mafunzo kwa vitendo.

Asante.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
View attachment 1345422

Hakunaga ubaguzi mbaya kama ule wa kujaribu kufanya kitu tofauti kionekane sawa na vingine vilivyofanana. Ni ubaguzi mkubwa kwa kukifanya hiki Chuo cha Mzumbe kionekane sawa na vingine wakati kuhalisia Chuo cha Mzumbe hakijafikia kitaaluma kama vingine.

Hapa sizungumzii maneno matupu naongea kwa ushahidi kabisa, kusomea Chuo cha Mzumbe ni rahisi mno mtu kufaulu ukilinganisha na vyuo vingine.

Wale tuliosoma vyuo tunajua kwamba Degree nyingi zina semester sita, kila semester ina masomo yake na kila semester mtu anapata GPA kulingana na ufaulu wake katika masomo aliyosoma kwenye semester nzima.

Vyuo vingi somo la field training huwa linakuwa limeunganishwa kwenye semester ya nne ya mwaka wa pili, semester hii ya nne inaweza ikawa na masomo ya darasani matano na la sita ndio field work inayofanyika chuo kikifungwa. Hivyo nayo field work inajumuishwa na masomo hayo matano ili kupata GPA.

Cha ajabu wenzetu semester nzima inatumika kufanya hiyo field work pekee, yaani hii semesta haina masomo yoyote zaidi ya field, mtu akipata A ya field basi kachukua marks 5 zote za kwenye GPA ya semester tofauti na vyuo vingine ambavyo hata ukipata A ya field work unaweza kujikuta umeambulia GPA ya 3.7 ikijumuishwa na masomo mengine.

Kupata A ya field work Mzumbe ni sawa na mtu aliesoma UDSM, IFM, IAA Arusha, TIA, n,k kupiga “A” masomo yote matano kwenye semester nzima kitu ambacho ni nadra sana.

Hali hii inachangia mhitimu apate GPA ya juu kuliko wa vyuo vingine na hata kuwa na uhakika zaidi wa kupata Second Upper Class kuliko wa vyuo vingine kama uonavyo hapa chini.

Nadhani suluhisho la kuleta haki ni kukifanya hiki chuo kiwe na semester tano, hio field ijumuishwe na masomo mengine ya semester ya nne, Haiwezekani mtu anakula GPA ya 5 kirahisi rashi yupo field wakati wenzake wanapambania hio GPA darasani.
Mkuu Machozi ya Simba asante kwa kuleta hili suala. Tuliosoma Mzumbe tunafahamu, hiyo siyo A kama zawadi, ina vipengele vyake vingi sana mpaka kupata A. Wanaofahamu vizuri watakuja kufafanua, ila ngoja nikupe mtonyo kama ifuatavyo:

1.Hiyo field report ni research report ambayo humfanya mwanafunzi awe equipped with research skills (lengo ni kufahamau namna ya ku solve organization problem with evidence (based on research). Na uelewe mwanafunzi aliyesoma bachelor Mzumbe kufanya master dissertation kwake huwa siyo tatizo, ila waliosoma vyuo vingine ndiyo wanaongoza kuandikiwa master dissertation zao, na hilo lina ushahidi.

2. Mwanafunzi anakuwa evaluated katika sehemu kuu tatu (i. Host supervisor wa organization ana mark 20%; ii. Oral Examination inakuwa na panel ya examiners watatu–Major, internal, na chair wa kamati na ina marks zake 35% (sina hakika siku hizi), iii. Field research report ina 45% (sina hakika siku hizi)). Na kumbuka oral examination inamtaka mwanafunzi ailewe kazi yake yote (literature review, problem statement, research questions/objectives etc).

3. Field research report ina kuwa marked na watu watatu (major, internal na external).

Ukiangalia 1-3 unadhani ni rahisi kupata hiyo A?

Pia wanapoenda kwenye organization kufanya hizo field wanatakiwa kuhakikisha wanafuata masharti ya kazi, mfano, confidentiality, kuwahi kazini, na kutoka kulingana na masharti ya kazi, na ni lazima Lecturers wawatembelee kuona mwenendo wa wanafunzi, na ndiyo maana organization nyingi zinawagombania wanafunzi wa Mzumbe kwa sababu wana muongozo ambao unahakikisha organization inakuwa salama. Na kwa sababu ya mchaka mchaka wa shule ni mkubwa basi wanafunzi wa Mzumbe ni wachapa kazi sana, wanafanya kazi kwa sababu wamezoea toka chuo, maana chuoni kuna bata na masomo kwa sana!
 
Mkuu sina la kuongea sana, karibu na ww upate A ya bure (kuongea bila kuchunguza ni kushindwa kutumia elimu yako vzr)


Kwa taarifa ndogo uku ukipata sup moja ya core subject na ukashindwa kuchomoa ata kama una gpa 4.8 una disco
 
Kwa mwaka mzima unalisoma somo hilo natamani ata ningekuwa nipo udsm nakula kiyoyozi au apo ulipo soma ww najuta why niliomba chuo hiki
 
Mkuu Machozi ya Simba asante kwa kuleta hili suala. Tuliosoma Mzumbe tunafahamu, hiyo siyo A kama zawadi, ina vipengele vyake vingi sana mpaka kupata A. Wanaofahamu vizuri watakuja kufafanua, ila ngoja nikupe mtonyo kama ifuatavyo:
Mkuu nina marafiki wengi wa chuo hiki tawi la Mbeya kila mwaka tunafahamiana nawasaidiaga accounting maana mimi nna cpa1 wengi hunionesha matokeo yao wakiwa na "A", kuna moja kipindi cha field ye alikuwa analima nyanya alipata "A". hiki kipindi wao kinakuwaga kama holiday maana hata napofanyia kazi walipokaguliwa tu januari katikati wakaondoka, wapo nyumbani saizi maana hapa napofanyia kazi hakuna posho, Ila huenda wewe labda kilaza ukaishia kupata B+ yawezekana ulikua unajiuma uma kwenye panel.
Hiyo field report ni research report ambayo humfanya mwanafunzi awe equipped with research skills (lengo ni kufahamau namna ya ku solve organization problem with evidence (based on research). Na uelewe mwanafunzi aliyesoma bachelor Mzumbe kufanya master dissertation kwake huwa siyo tatizo, ila waliosoma vyuo vingine ndiyo wanaongoza kuandikiwa master dissertation zao, na hilo lina ushahidi.
Dissertion hapo ndio kabisa, kila moja aliekuja hapa ofisini kufanya training kanunua kwa elf 40 kwa vijana wasio na ajira waliomaliza masters wanasubiria tu panel huko kutikisa taya, nakumbuka hata sista wangu alisoma mzumbe alinunua kwa laki 1 kama wenzake wengi
Mwanafunzi anakuwa evaluated katika sehemu kuu tatu (i. Host supervisor wa organization ana mark 20%; ii. Oral Examination inakuwa na panel ya examiners watatu–Major, internal, na chair wa kamati na ina marks zake 35% (sina hakika siku hizi), iii. Field research report ina 45% (sina hakika siku hizi)). Na kumbuka oral examination inamtaka mwanafunzi ailewe kazi yake yote (literature review, problem statement, research questions/objectives etc).
Hio host super visor wanafuzi tunawapaga marks zote na zile form zao sijui za tabia nzuri, kuwahi, n.k karibu ofisi zote tunawaambiaga wanafunzi wajijazie, labda bosi awe kauzu, Oral examination hapo ni mdomo wako tu kushindilia points kama mnavypulizwa maswali kwenye group maana nina rafiki yangu ni lecturer ana masters ya open alinialika siku moja chuo niliiona ile panel ya kawaida tu, field research report ni kuedit tu
Field research report ina kuwa marked na watu watatu (major, internal na external).
Bla bla bla ndo yale yale ya mtihani kutungwa lecturer kusahishiwa na watu wengine
Ukiangalia 1-3 unadhani ni rahisi kupata hiyo A?
Ndio ujiulize sasa kwanini wenzako wengi wanapaa A, Labda wewe ulikuwa kilaza mkuu ukapewa b+
Pia wanapoenda kwenye organization kufanya hizo field wanatakiwa kuhakikisha wanafuata masharti ya kazi, mfano, confidentiality, kuwahi kazini, na kutoka kulingana na masharti ya kazi, na ni lazima Lecturers wawatembelee kuona mwenendo wa wanafunzi,
Hivi kuna chuo kipi ambacho hakifanyi haya, kila chuo hapa ofisini wanafunzi wao wanakujaga na form tunazowajazia tabia, kuheshimu mda, n.k na kila mwanafunzi lazima aje akaguliwe
Na kwa sababu ya mchaka mchaka wa shule ni mkubwa basi wanafunzi wa Mzumbe ni wachapa kazi sana, wanafanya kazi kwa sababu wamezoea toka chuo, maana chuoni kuna bata na masomo kwa sana!
Mchaka mchaka upi wewe, Nadhani kwa sababu ulikuwa ni kilaza ukaona ni mchakamchaka, masomo 5 kwa semesta unasema mchackamchaka??? semista nzima watu wapo field huu ndio mchakamchaka?? hapa kazini kulikuwa na wanafunzi wa field wa cbe wa diploma na hawa wa mzumbe kiukweli sikuona utofauti kwasababu kazi hizi ukizoea kwa wiki 1 tu kwisha habari
na ndiyo maana organization nyingi zinawagombania wanafunzi wa Mzumbe kwa sababu wana muongozo ambao unahakikisha organization inakuwa salama.
Dah aisee, naona umeyanywa maji ya bendera sasa, Nadhani bado upo chuoni au umemaliza bado hujaajiriwa, Tafuta kazi uajiriwe alafu uone utavyojicheka ulichokiandika hapa, Binafsi nilisoma chuo cha uhasibu Arusha niliwagaragaza wenzangu wa vyuo vyote maana nilikuwa na distinct advantage ya computer, Aisee kazi ya masaa 10 nilikuwa naipiga kwa saa tu napewa attention yote, Ofisi nayofanyia kazi ni ya serikali na sijawahi kusikia upuuzi huu ila kwa mbali sana UDSM..
 
Mkuu sina la kuongea sana, karibu na ww upate A ya bure (kuongea bila kuchunguza ni kushindwa kutumia elimu yako vzr)


Kwa taarifa ndogo uku ukipata sup moja ya core subject na ukashindwa kuchomoa ata kama una gpa 4.8 una disco
Nimesoma accounting na kuna kipindi nilikua nakaa maeneo ya mzumbe vijana wengi sana wa BAF nimewasaidia kusolve problems, nilikuwa sioni jipya maana ni vitu vya kawaida tu kuanzia capm, abc costing, stepping stones, ratios, n.k

Yaani upate sup, ucarry somo alafu ufeli tena, aisee!! hapo umeenda shulenu au, ila uzuri wa mzumbe huwezi kudisco hata upate supp 5 kwenye masomo 7 ushahidi huu hapa kwenye by laws.

1581272548178.png
 
Elimu ya Tanzania ni ya kukariri ili kufaulu mtihani tu. Masuala ya GPA sio kipimo rasmi wa uwezo wa mtu, maamuzi ya kubania GPA ni maprof kuwa roho mbaya ya wivu kuona watoto wa wenzao wakifaulu.
Tanzania toka 1961 mpaka leo hakuna cha msomi, mtaalam, cream, lotion wala TO. Hao wote ni kukariri, inabidi mfumo wa elimu urekebishwe tusome kwa kiswahili ili tuelewe kinachofundishwa.


Ngoja niendelee kukariri vitini hapa.







SIZAN KAMA UPO SAHIHI,UNAPOZUNGUMZIA MFUMO UNAKOSEA TATIZO NI ZERO INOVATION AND CREATIVITY B'COZ THEORIES NIMUHIMU SANA...MFANO MADAKTARI, MAE ENGINEERS, AND OTHER RELATED SCIENCE FIELD WANAONGOZO NAIZO THEORIES (ambazo unadai wanakariri) MFANO DOCTORS LAZIMA WA KARIRI LITERATURE , THAT WHY UNAENDA UNAMWELEZA MATATIZO ANA CORRELATE NA ALICHOSOMA ILI AJUE TATIZO..,,, SO TZ ATUJATOFAUTIANA NA WENZETU WA ULAYA KAMA THEORIES WANASOMA SO THE DIFFERENT IS CREATIVITY AND INNOVATION ....PIA KUNAWENGI WANASEMA OO TZ TUNAFUNDISHWA THEORIES SANA BILA KUPRACTIZ ,,, USHAJIULIZAGA HOW COME TUNAJUA KUTUMIA SIMU ILA ATUJUI JINSI INAVYO TENGENEZWA? ... MAANA YAKE NIKWAMBA ATUNA KNOWLEDGE (THEORIES) ON HOW TO MAKE IT....SO THE IMPORTANT THING IS KNOWLEDGE PRACTICAL INAFUATAAA............................
 
Back
Top Bottom