Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,632
- 697,796
Tafsiri ya jangwa iko wazi... Ni mahali pasipomea... Sehemu kame kabisa... Jua kali pamoja na joto kali mchana... Usiku baridi kali na wakati mwingine upepo pia.. Jina la sehemu yenye jangwa huitwa Jangwani
Mfano wa majangwa ni Karahali na Sahara... Lakini je unafahamu kwamba majina huathiri na hulka na hata kuleta uhalisia?
Siandiki sasa kwakuwa timu ya Yanga inafanya vibaya kwenye medani ya soka... Pamoja na ukweli kwamba imekuwa na rekodi na matukio ya hovyo kwa ujumla wake kwa muda mrefu sana.... Kwa majumuisho ya jumla Yanga imeachwa mbali na Simba... Yanga inajulikana kama wazee wa Jangwani
Siandiki haya kwakuwa shule ya upili ya wasichana ya Jangwani imefanya vibaya sana kwenye mitihani kitaifa... Imekuwa shule ya 351 kati ya shule 353? Jangwani sekondari
Ni kipi kilishawahi kufanikiwa eneo hilo la Jangwani? Pale ni eneo oevu na tepetevu... N eneo la kidau na lina majimaji majira yote ya Mwaka... Ilikuwaje paitwe jangwani? Mbona jina haliakisi uhalisia? Kiroho kuna tafsiri pana sana
Pale sio jangwa la kimwili... Pale ni jangwa la kiroho.... Ni mapito na makazi ya wenyewe.... Ni mapito ya maji wakati wa mvua lakini pia pana muunganiko na bahari pale.. Ni kipumzikio cha watu pale.... PAACHWE kama palivyo
Hivi unaweza kuamini kuwa STRABAG walishindwaje kujenga barabara ya juu toka magomeni mpaka fire?
Hivi unawezaje kuamini kuwa kuna wakandarasi na elimu na akili zao walishauri kijengwe kituo cha UDART pale? Matokeo mmeyaona? Wanapakimbia
Mpaka leo hii serikali haiwezi kukwambia ukweli eneo lile la jangwa limekula mabilioni mangapi kila mwaka kujaribu kudhibiti mafuriko ya pale.
Ongea uliza watu walioishi pale maisha yao yalikuwaje baada ya kuhama... Wengi wanakiri walikuwa wamefungwa...
Zamani palikuwa na ahueni kwasababu ya makafara... Watu wameuliwa sana pale.... Jangwani ndio ilikuwa mabwepande ya WANA... jangwani palikuwa panatisha na kuogopeka.. Matambiko na kafara vilifanyika sana pale.... Si kila maiti iliyookotwa pale ilikuwa ni kutokana na risasi moja kisogoni
Matambiko na makafara yale vilisaidia kwa kiasi kikubwa kupoza mambo.... Siku hizi pana mataa ya kizungu usiku mzima.
Jangwani sekondari ina historia yake chafu sana... wazee wa mujini wanafahamika vema wallichoifanyia ile shule... Lakini kila jambo lina asili yake... Ya Yanga tusiyaongelee leo..... I inatosha tu kusema MZIMU WA JANGWANI UMEFUFUKA..,
Good morning Africa!
Mfano wa majangwa ni Karahali na Sahara... Lakini je unafahamu kwamba majina huathiri na hulka na hata kuleta uhalisia?
Siandiki sasa kwakuwa timu ya Yanga inafanya vibaya kwenye medani ya soka... Pamoja na ukweli kwamba imekuwa na rekodi na matukio ya hovyo kwa ujumla wake kwa muda mrefu sana.... Kwa majumuisho ya jumla Yanga imeachwa mbali na Simba... Yanga inajulikana kama wazee wa Jangwani
Siandiki haya kwakuwa shule ya upili ya wasichana ya Jangwani imefanya vibaya sana kwenye mitihani kitaifa... Imekuwa shule ya 351 kati ya shule 353? Jangwani sekondari
Ni kipi kilishawahi kufanikiwa eneo hilo la Jangwani? Pale ni eneo oevu na tepetevu... N eneo la kidau na lina majimaji majira yote ya Mwaka... Ilikuwaje paitwe jangwani? Mbona jina haliakisi uhalisia? Kiroho kuna tafsiri pana sana
Pale sio jangwa la kimwili... Pale ni jangwa la kiroho.... Ni mapito na makazi ya wenyewe.... Ni mapito ya maji wakati wa mvua lakini pia pana muunganiko na bahari pale.. Ni kipumzikio cha watu pale.... PAACHWE kama palivyo
Hivi unaweza kuamini kuwa STRABAG walishindwaje kujenga barabara ya juu toka magomeni mpaka fire?
Hivi unawezaje kuamini kuwa kuna wakandarasi na elimu na akili zao walishauri kijengwe kituo cha UDART pale? Matokeo mmeyaona? Wanapakimbia
Mpaka leo hii serikali haiwezi kukwambia ukweli eneo lile la jangwa limekula mabilioni mangapi kila mwaka kujaribu kudhibiti mafuriko ya pale.
Ongea uliza watu walioishi pale maisha yao yalikuwaje baada ya kuhama... Wengi wanakiri walikuwa wamefungwa...
Zamani palikuwa na ahueni kwasababu ya makafara... Watu wameuliwa sana pale.... Jangwani ndio ilikuwa mabwepande ya WANA... jangwani palikuwa panatisha na kuogopeka.. Matambiko na kafara vilifanyika sana pale.... Si kila maiti iliyookotwa pale ilikuwa ni kutokana na risasi moja kisogoni
Matambiko na makafara yale vilisaidia kwa kiasi kikubwa kupoza mambo.... Siku hizi pana mataa ya kizungu usiku mzima.
Jangwani sekondari ina historia yake chafu sana... wazee wa mujini wanafahamika vema wallichoifanyia ile shule... Lakini kila jambo lina asili yake... Ya Yanga tusiyaongelee leo..... I inatosha tu kusema MZIMU WA JANGWANI UMEFUFUKA..,
Good morning Africa!