Jc Simba
JF-Expert Member
- Mar 23, 2017
- 300
- 422
[http://dsh7tu7hoh3mx]
Rais wa zamani wa Ufaransa Nicolas Sarkozy aendelea kushikiliwa na polisi
21 Mar 2018, 04:30 pm| By Azam NewsUHALIFU
Rais wa zamani wa Ufaransa Nicolas Sarkozy ameonekana akiwa na Polisi nyumbani kwake leo asubuhi mjini Paris na kisha kuondoka na maafisa hao ambao wanaendelea na uchunguzi wa tuhuma zinazomkabili kiongozi huyo.
Inaelezwa kuwa baada ya ukaguzi uliofanyika kwenye makazi yake, Sarkozy amerejeshwa Polisi kwa mahojiano zaidi ambako amewekwa mahabusu tangu jana ikiwa ni sehemu ya uchunguzi kuhusu kashfa inayomkabili ya kupokea mamilioni ya fedha za kampeni za urais kutoka kwa kiongozi wa zamani wa Libya, marehemu Muammar Gadhafi kinyume cha sheria.
Chanzo kimoja kimelitaarifu shirika la habari la AP kuwa Rais wa zamani wa Ufaransa anashikiliwa katika kituo cha Polisi cha Nanterre mjini Paris.
Polisi wanachunguza uhalali wa fedha alizotumia katika kampeni za kuwania urais mwaka 2007 ambapo mara kadhaa Sarkozy amekuwa akikana shutuma hizo.
Rais wa zamani wa Ufaransa Nicolas Sarkozy aendelea kushikiliwa na polisi
21 Mar 2018, 04:30 pm| By Azam NewsUHALIFU
Rais wa zamani wa Ufaransa Nicolas Sarkozy ameonekana akiwa na Polisi nyumbani kwake leo asubuhi mjini Paris na kisha kuondoka na maafisa hao ambao wanaendelea na uchunguzi wa tuhuma zinazomkabili kiongozi huyo.
Inaelezwa kuwa baada ya ukaguzi uliofanyika kwenye makazi yake, Sarkozy amerejeshwa Polisi kwa mahojiano zaidi ambako amewekwa mahabusu tangu jana ikiwa ni sehemu ya uchunguzi kuhusu kashfa inayomkabili ya kupokea mamilioni ya fedha za kampeni za urais kutoka kwa kiongozi wa zamani wa Libya, marehemu Muammar Gadhafi kinyume cha sheria.
Chanzo kimoja kimelitaarifu shirika la habari la AP kuwa Rais wa zamani wa Ufaransa anashikiliwa katika kituo cha Polisi cha Nanterre mjini Paris.
Polisi wanachunguza uhalali wa fedha alizotumia katika kampeni za kuwania urais mwaka 2007 ambapo mara kadhaa Sarkozy amekuwa akikana shutuma hizo.