Mzee Mwanakijiji, Tafadhali...


ALSO THE END JUSTIFY THE MEANS. Yaani unaweza kutumikia njia ambazo jamii isikuelewe lakini kutokana na GOOD end results jamii ikakuelewa na means wakazikubali. UPO HAPO. Hao wanaotuumiwa sasa pelekeni mahakamani mnaguna nini. CHADEMA WAMEAMUA that means baada ya kuelewa sasa kusita kwa nn. yawezekana lowasa alionekana fisadi kwa maagizo ya wakuu. sasa kajieleza kaeleweka CHADEMA wamemuona sio fisadi HAPO VIPI. Mlete Chenge nae tutamhoji tukiona chenga tunamtema kwa gear ile ile ya hewani. LOWASA ANASEMA MWAMBA AMWAGE UGALI KWA KWENDA MAHAKAMANI. YEYE ATAMWAGA MBOGA HUKO HUKO. watu chaliii.. kimyaaa
 
Character X, thank you. I couldn't have said it better. Toka mwaka 2008 naandika humu kuwa adui mkubwa wa taifa letu ni CCM...si Kikwete, si Mkapa, si Kinana, si Nape na si Makonda. Hapana, hawa ni watu tu wa kawaida kama sisi wengine, it is CCM that makes them different from us, it is CCM that transforms them into the monsters we see, it is through CCM that otherwise nice and kind people evolve into ruthless beasts, it is CCM that has turned our beloved country into a jungle of hyenas fighting each other for the pieces of her poor torn body!

CCM has to go first, the rest can then follow...
 
Last edited by a moderator:
Character X, na wengine nimewasoma sana tangu ilipopostiwa mada hii na imenisaidia na inaendelea kunisaidia kuelewa vizuri political dynamism iliyoko nchini. Alichosema GalaxyS3 hapo juu kinatosha kuwatafakarisha kidogo. Kuna vitu viwili ambavyo naona vinaongelewa sana bila watu kuvifikiria sana; kwanza ni hii hoja ya kuwa "lengo ni kuiondoa CCM tu" na pilia "kwa njia yoyote ile". Natafuta wasaa niandae jibu langu vizuri ili niweze kujibu hoja hizi mbili vizuri zaidi na kuonesha ni kwa namna gani zina makosa kwenye msingi wake.

Uzuri wa demokrasia hata hivyo ni watu kuweza kudissent; demokrasia haiwezi kustawi kama watu wanatakiwa kupanga mstari na kusema "ndio mzee". Tuliwakatalia watawala wa sasa hili na tutawakatalia watawala wajao pia. Hatuwezi kuwa watu wa kuitikia ati kwa vile viongozi wamesema. Tuna haki ya kuhoji na kuuliza ili tushawishiwe na sisi tuone wanachokiona wao lakini kama haiwezekani tuna haki ya kukataa (dissent) tukiwa tayari kuishi na matokeo ya kukataa huko. Kwa mfano, Lowassa akaenda akashinda Urais kupitia CDM haina maana sisi wengine tutakuwa tumebadili mawazo na kushangilia.

So, nitawajibu kwa kirefu labda mara moja tu halafu niachane na hii mada.
 
Kwanza nimpongeze mtoa mada ,amechangia vizuri sana na kuamsha Ari ya wachangiaji wengine.
Pili niwapongeze wachangiaji wengine wote waliokua wanakubaliana na kutofautiana kuhusiana na suala lolote lililo mbele yetu.
Lakini pia kwenye msafala wa mamba na kenge pia huwa hawakosekani hasa ukichukulia wale wanaochangia kama wako face book,na kwingineko kama vile hawajui mustakabali wa maisha yetu kama Taifa ni wetu sote bila kujali uko upande wa upinzani au Twawala.

Niseme tu kwa kifupi mimi ni miongoni mwa watu waliokua disappointed kwa Lowasa kuingia CDM.lakini pia nilivurugwa kabisa kwa suala la yeye kuteuliwa kuwa mgombea.Nikaona sasa ndio upinzani unakufa.

Lakini nimeweka mawazo yote mazuri ya pande zote mbili pamoja niweze kujiridhisha.nimemchukua Character X upande mmoja nikamuweka Galaxy S3 upande mwingine.Kila mmoja ana hoja za msingi.Lakini katika kutafakari nikaona niweke mawazo yao kwenye mazingira ambayo nchi imefikia kwa sasa ,naweza kuchagua upande upi.Kukubaliana na uongozi wa CDM ama Kuwaupande wa MM Mwana kijiji.

Ukiangalia nchi yetu ilipofikia utaona kwamba mazingira hayawezeshi upinzani kuchukua Madaraka mwaka huu,wangejitahidi sana ni kuongeza wabunge ambao hata hivyo hatuna uhakika kama wangeweza pata hiyo 51 percent tunayoitaka ama la.Wakati huo huo tuangalie namna rasilimali zetu zinavyogawanywa kwa uharaka uliokithiri kwa wageni,ili hali hatuna hata sera muafaka zinazosimamia uwiano wa haki kati yetu na wawekezaji,tukiondoa mbali rushwa iliyogubikwa kwenye michakato hiyo,na pia ukiangalia namna teknolojia ya kuvuna mali asili zetu inavyokua kwa kasi,Mf.Kuna migodi tuliambiwa ina deposit ya miaka 30,lakini teknolojia imewezesha rasili mali hizo kuvunwa ndani ya miaka isiyozidi 15.Matokeo yake hesabu tulizopigiwa za kupata matrilioni zinabaki kuwa hewa.

Upande wa pili nikabaki nikiwaza ndugu yetu Galaxy S3 anayotushauri mambo ya msingi kabisa.Kuhusiana na kupotoka kwa chama hasa kutosimamia misingi ya uadilifu,kwa kuleta watu wasiofaa,na kuacha kuendelea kujenga misingi ya uadilifu mpaka pale ukombozi wa kweli utakapopatikana.Kwa kweli hii ni njia panda kubwa katika upinzani ambayo ikishindwa itatuchukua miaka mingine mingi ijayo kujenga upinzani imara.

Lakini iwe isiwe tumewekwa kwenye njia panda ya kufanya maamuzi ,kukubaliana ama kukataa.Kwa upande wangu kwa mara ya kwanza nimekubaliana na theory ya "The End jusutifies the Means".sababu kubwa ni mazingira tuliyo nayo kwa sasa.Rasilimali zetu zinaisha kwa sasa.Hata hapo baadae tukijenga kizazi chetu cha waadilifu hakitakuta kitu.Matokeo yake kitaanza tena kutafuta utaratibu mwingine wa kuja kudai mali zetu kwa waliozipora kwa mikataba feki.Tutakuta tena taifa letu likizidi kuwa ombaomba kwa karne nyingine zijazo.Nimeona ni bora tubaki na tatizo moja la kuja kushughulia uadilifu kuliko kuhangaika na yote kwa wakati mmoja.(CCM na UFISADI)

Mtizamo wangu ni "half a thing,is better than nothing" Ni heri kupata kidogo kuliko kukosa kabisa.Tuunganisheni nguvu CCM itoke tu define upya.Hapo CCM nayo itaanza kujisafisha kwa kubaki na wale wenye moyo safii.Upinzani wakifanya tofauti tutawatoa kirahisi kuliko ilivyo kwa CCM sasa,ni ngumu sana.
 
Nimesema na kuandika hapa jf mara nyingi kuwa ilipotufikisha ccm ni vyema kutumia silaha yoyote kuindoa ccm. Nimewai kuandika pia ccm haiko tayari kutoa madaraka ya kidola kwa vyama pinzani....na wametamka hivyo si mara moja au mbili....

Ktk mazingira hayo chadema imesoma harama za nyakati.....rejea aliyoyasema Mh Mbowe akimwambia Lowasa...."huku itakubidi uvumilie maana hata mabomu upigwa kidogo...labd wanaweza kukuheshimu maana kuna vijana wako...;

Kama EL anateuliwa kupeperusha bendera ya ukawa...basi kutakuwa na sababu za kipekee ukilinganisha na wengine akiwemo Dr. Slaa. Ninauhakika Dr. alikuwa mshindi 2010...hakutatangzwa mshindi.....ikitokea EL ni mshindi...kwa vyovyote vile atatangazwa. Kwanza anajua mbinu za wizi wao, pili ana nguvu za kidola (indirectyly).

Nimapema u_ccm kumtoka ila naamini busara za viongozi wa ukawa zitatumika ktk kutengeneza na kusuka upya serikali ijayo. Ushindi wa EL kama akiteuliwa na chadema hautakuja kwa kuwa atatmia pesa nyingi, la hasha! Ni kwa kuwa watanzania wanahitaji mabadiliko. Asahau kabisa uccm....hata ktk uteuzi wa ngazi zote za serikali akubali mpango mzima wa ukawa.
 
Godbless you jemedari
 
You have nailed it.
Ukisikia mtu anajidai eti kulaumu CDM kwa tukio hili, ujue ni CCM sympathizer hata kama hajitambulishi hivyo. Ni wasi wasi tu wa kulamba mchanga.
Decision hiyo imeelezwa vizuri sana na Mbowe na Tundu Lisu.

Mbowe na tundu lissu si malaika au miungu mzee,, wanapoongea huwa unapima na kujilizisha kwanza,, kwa hili binafsi naweza kulipinga popote na bado nikamshinda lissu au mbowe,,, lowassa alikuwa kwenye system ya wezi,,, kwa nini hakuiacha hiyo system hadharani na mchana kweupe kwa kuonyesha uzalendo ila aliendelea kiwepo kwa miaka na karne mpaka system hiyo imnyime nafasi ya kugombea urais ndio atuambie kuwa haifai??? Inamaana yeye alivyokuwepo ni sawa na safi leo hayupo basi ccm hawafai -- moja kwa moja tukionacho ni tamaa na kisasi..
 
Unasema LENGO KUU NI KUINDOA CCM, lakini CCM nao LENGO KUU NI KUIPOTEZA CHADEMA. Pia kumbuka kuwa muwinda huindwa! Pia sio kila fursa ni fursa stahiki zingine ni uzushi.... LOWASSA ni Waziri Mkuu mstaafu ambae kwa mujibu wa sheria ya Tanzania hulindwa na usalama wa wataifa kwa kipindi chao chote cha maisha. Hivyo hii ni binu nanifursa kwa CCM kuipoteza CHADEMA kwa kumtumia LOWASSA ambeye ameenda CHADEMA kimkakati.
 
.
Hayo ni maoni yako na una haki ya kuyatoa. Ila siamini kama uko sahihi, sisi tunaona ni turufu mujarabu kushinda uchaguzi huu. CCM wanahaha kama haina madhara kwanini wanatapatapa. Big up kamanda Mbowe chadema tupo pamoja na wewe
 
Mkuu kila la kheri naungana na wewe kwa asilimia zote
 

My point Is; Use your influence to the right end... Influence those that believe in you positively.

Whether you were right or wrong I don't intend to arbitrate..

But as a leader you need to know your role, in my opinion you are a better leader if you can keep your people together.
 


mkuu vipi mbona povu!! hehehehe
 
Kwa nini mstumie kiswahili lugha yetu, nasema hivyo kwa sababu nashindwa kung'amua maana halisi ya lugha mnayotumia.
 
Thank you!!
 
Huwezi kutisha watu wazima!
 
Huyo Mzee Mwana kijiji, tupa kuleeeeeeeeeeee.... lofa tu, hajui siasa, kazi yake chuki binafsi ndio inamuongoza kwa mtu husika,,hasa kwa Lowassa, Mzee Mwanakijiji ana chuki binafsi na Lowassa..

Huyu Mwanakijiji hafai kabisa CDM... yeye
kumpamba tu Dr. Slaa, cjui shemeji yake...?? Very unethical indeed...hana akili kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…