Nataka kutumia mantiki mpaka mwisho wa hoja kabisa. Kwa hivyo nitatumia muktadha ambao si halisi au wa kufikirika ili kufika hoja mujarabu. Lengo letu ni kuing'oa sisiemu. Je, endapo watu wote walio sisiemu wakisema leo hii sisi si sisiemu bali ni sisiemu, itakuwaje? tutawakubalia? I admit this is an extreme scenario. Kilichotokea ni wachache wa wale tunaojua kwamba wameharibu nchi ndiyo wamekwenda ukawa au CDM. Hapo ndipo ninapoiona hoja ya Mzee Mwanakijiji.
Ngoja nirejee tena kwa masisiemu yanafanyaje mambo yao. Yanatumia nafasi zao, yanatumia pesa, yanatumia dola kujinufaisha yenyewe bila kujali hali ya nchi. Hapo basi EL amefanyaje kuingia CDM? Ametumia nafasi yake katika CCM, ametumai pesa zake alizojipatika katika CCM kuingina ukawa. Hapo ndipo ninapokosa imani na EL na wimbi zima la nyinyiemu kuingia ukawa. Itakuwaje tuwape dhamana watu walewale waliotuleta hapa? I'm sorry, this makes absolutely no sense to me. Kwa kweli, kwa sasa sitapiga kura. Majambazi yamegombana nasi tunagombana kuyapigia kura?????