Mzee Jakaya Kikwete hela za kuwekeza kwenye Elimu alikuwa anazitoa wapi

Ni vipaumbele tu, JPM aliwekeza kwenye miradi mikubwa mfano Stiglers na SGR, JK ndio akawekeza kwenye elimu nakumbuka kuna wakati ikasemekana hata lile wazo la shule za kata aliyelileta alikuwa Lowassa akiwa PM.

Samia licha ya kuwepo madarakani kwa muda mfupi bado haeleweki mipango yake, ila hali ya mambo inavyoonesha, naona wameshaanza kula kwa urefu wa kamba zao.

- Bwawa la Nyerere ni kama limeshawashinda, sioni cha maana wanachofanya zaidi ya kufanya ziara kuangalia maendeleo ya ujenzi wake watuzubaishe lakini baada ya hapo ni kimya. Ile habari ya winchi ya tani 24 iliyoagizwa nayo sijui iliishia wapi.

- Umeme kukatika hovyo bila sababu za msingi, mwanzo walisema chanzo kilikuwa ukame, lakini hata baada ya mvua kuanza kunyesha bado umeme unasumbua, tatizo ni nini? kama ni maintanance kwa nini tatizo bado liwe endelevu? hapa ndipo JPM anapokumbukwa.

- Tozo; walisema zitaenda kujenga madarasa na vituo vya afya matokeo yake wakatumia pesa za Covid kwa ajili ya kazi hiyo, sasa sijui hizi tozo wanazotoza mpaka leo zinatumika kwa kazi gani wala hatuambiwi tena kwa mwezi wamekusanya ngapi na zinaelekezwa wapi? mambo yanajiendea tu.

- Mfumuko wa bei, bidhaa kupanda bei kila siku wakiulizwa wanasema tatizo ni soko la dunia, nashangaa hata nyama ya n'gombe nayo kupanda imesababishwa vipi na soko la dunia wakati Tz tuna n'gombe wengi tu?.

Wengine wanasema "soko huria" kwa hiyo hili soko ndio limeachwa limuumize mlaji kama vile hakuna serikali ya kusimamia mambo? kumbe sasa Tanzania wafanyabiashara wako juu ya serikali.

Hapa tatizo ni usimamizi na ufuatiliaji, kuna uzembe umerudi serikalini.
Ukweli mtupu
 
Kwenye shule za kata JK aliupiga mwingi sana.

Hata leo, Spirit ilitakiwa iendelee ileile ya kutumia wananchi kujenga shule zao zinazohitajika siyo kukopakopa utadhani hskuna kesho!
Kutumia wananchi au kutumia kodi wanazochukua kwa wananchi?
 
Huyu mzee wa Msoga kwenye Elimu alitisha Sana,

Fikilia SSH amejenga madarasa elfu15 kwa pesa ya mkopo kutoka IMF, kwa iyo idadi ni madarasa kidogo Sana kwa nchi Kama Tanzania. Serikali ya JPM iliferi vibaya Sana kwenye Elimu, ata kuajiri walimu alishindwa, aliajiri walimu wachache mno, Tena kwa mbwembwe za press conference.

SSH, yeye amekopa kujenga madarasa, wanafunzi wameanza shule this week lakini walimu hasa wa Sayansi hakuna. Serikali imeshindwa kuajiri walimu wa kufundisha watoto wetu. Shule hazina walimu wa hesabu, physics, chemistry na Biology.

Lakini JK alijenga Madarasa kila kata nchi nzima, hakukopa kujenga madarasa, aliajiri walimu maelfu kwa maelfu.mfano wa idadi ya walimu walioajiri kipindi Cha JK.

2012/2013- walimu 32,764
2013/2014- walimu 40,327
2014/2015- walimu 46,103

Lakini chini ya Magufuli

2015-2016-hakuajiri sababu ya uhakiki

2016-2017-walimu 3184
2017-2018-walimu 4854
2018-2019-walimu 4327
2018-2020-walimu 8543

Chini ya Samia
2021-walimu 6468

JK alipata wapi hela za kuwekeza kwenye Elimu, na JPM na SSH wameshindwa nini, ufaulu wa juzi 64% wamepata division four na zero kwa kidato Cha nne.

Swali, JK alipata wapi pesa kuwekeza kwenye Elimu?
Hakuna raisi aliyekuwa anazunguka duniani kama JK.
 
Tikiti kabisa, eti shule kongwe, kujenga madarasa kila kata nchi nzima sio mchezo, JPM kwenye Elimu aliferi vibaya sana
Hivi unazijua shule zilizokarabatiwa kweli au huna taarifa,utalinganisha unafikiri na kujenga madarasa mawili kila shule hauko serious ama unazungumza kusogeza masaa.
 
Umeshindwa kuprove kwa fact alifeli vipi wakati ndie aliye asisi elimu bure na ndie aliyesajili wanafunzi wengi wa darasa la kwanza kuliko kiongozi yeyote, kama hiyo haitoshi kwenye uongozi wake hatukuwahi sikia wanafunzi wa vyuo vikuu wakigoma kisa kuchelewesha mikopo yao. Kuajiri aliajiri kulingana na mahitaji, sasa hapo utasema alifeli au wewe ndio unafeli humu kuweka ushahidi wako.
eti kusajir wanafunzi wengi Ni Maendeleo, afu ukisha wasajir afu hujaajiri watafundshwa na mizimu
 
Kenge mama yako msenge wewe! Hizo VETA karibia kila mkoa huzioni? Wewe unahangaika na Magufuli ambaye wewe na ukoo wako uchwara hutakaa uwafikie kimaisha kwa kila kitu!
Magufuli kwenye Elimu hamana kitu,alijua kuteka na kuua basi
 
Hivi unazijua shule zilizokarabatiwa kweli au huna taarifa,utalinganisha unafikiri na kujenga madarasa mawili kila shule hauko serious ama unazungumza kusogeza masaa.
Shule kongwe ata 200 hazifiki Tena kukarabati sio kujenga, kwenye Elimu aliferi vibaya Sana
 
eti kusajir wanafunzi wengi Ni Maendeleo, afu ukisha wasajir afu hujaajiri watafundshwa na mizimu
Utakuwa unamatatizo wewe sio bure kama ingekuwa hawafundishwi ilikuaje ufaulu ukaongezeka? Wewe ulitegemea ajira za sadakalawe au? Hao walimu waliokuwa walioajiriwa shule zote ikiwemo za ufundi hukuwaona?
 
Utakuwa unamatatizo wewe sio bure kama ingekuwa hawafundishwi ilikuaje ufaulu ukaongezeka? Wewe ulitegemea ajira za sadakalawe au? Hao walimu waliokuwa walioajiriwa shule zote ikiwemo za ufundi hukuwaona?
Mwaka huu 64% ya wanafunzi Kidato Cha nne wamepata Division four na zero,,,,
 
Lakini JK alijenga Madarasa kila kata nchi nzima, hakukopa kujenga madarasa, aliajiri walimu maelfu kwa maelfu.mfano wa idadi ya walimu walioajiri kipindi Cha JK.

Shule za sekondari za Kayumba[ KATA] zilijengwa kwa akili ya Edward Lowassa; Kikwete alikuja kudandia hizo şifa tu!! Pengine hizo hela alikopa kwa HOME SHOPPING CENTRE [ GSM] na Rostam!!!
 
Back
Top Bottom