Mzee mmoja alipanda kwenye daladala na kubahatika kupata siti, lakini baada ya muda akagundua kuwa simu yake aloiweka mfukoni imeibiwa, basi akaamua kumuomba jirani yake kwenye siti aibipu namba yake akiamini mwizi wake atakuwa hajashuka kwani daladala tangu iondoke alipopanda hakuna aliyeshuka. Kumbe yule jirani yake ndo alikuwa kamchomolea mzee simu yake na kuiweka kwenye kava jingine alilokuwa nalo, hivyo alipoombwa na mzee kuibipu namba yake, jamaa aliamua kumpa simu mzee ili abipu yeye mwenyewe kwa kuwa alijua dili lake lishawini. Basi ikawa kila Mzee alipojaribu kuibipu namba yake alisikia "Namba ya mteja unaempigia, inatumika kwa sasa tafadhali jaribu tena baadae"