Mzaha mzaha hutumbua usaha CCM

Mzaha mzaha hutumbua usaha CCM

H20

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2013
Posts
341
Reaction score
170
Kwa muda wa siku takribani 48 tumejionea kampeni za kisiasa kuwania kiti cha ukuu wa nchi ya JMT. Kuna mambo yamekuwa yakijitokeza ambayo kimsingi ni dharau na ufedhuli unaofanywa na watu wasio na chembe ya huruma kwa wagonjwa.


Hebu tujiulize ni nani hajawahi kuugua? Je mgonjwa kama raia yeyote wa JMT hana haki ya kuchaguliwa kuwa kiongozi? Kwanini CCM na wapambe wake wamekuwa wakiwadhihaki wagonjwa? Hebu fikiria wewe mgonjwa au ndugu yako mgonjwa unasikia watu wanawatukana na kudhihaki na wanadiriki kusema marehemu hatuoni huu ni efedhuli?
Kitendo cha kupiga push ups ni hali ya dharau kabisa kwa wagonjwa.

Yaani unaonesha kuwa wewe una nguuvu na umejaaliwa kuliko huyo unayemdhihaki. Hebu kama unafikiri kupiga push up ni vizuri nenda wodi za wagonjwa kafanye hivyo kama unataka kuwaburudisha uone.

Ikiwa mgombea amefikia hatua hii ya kujitoa utu wake na kuwadhalilisha wagonjwa kwa kupiga push ups, nachukua nafasi hii kuwaomba wale wote wanaoguswa na maumivu, mateso na taabu wanazopata wagonjwa wahakikishe ifikapo tarehe 25 Oktoba 2015 kuwakataa John Magufuli na wote waliowadhihaki wagonjwa aidha kwa maneno au/na matendo yao.

Tumuombe Mungu awaaibishe kwenye boksi la kura washindwe vibaya ila tuwaombee Mungu aendelee kuwapa afya njema.

Kama umekubaliana nami naomba ugonge like ili Mungu atende kwani peooooooooplesssss ni power. Mungu ibariki Tanzania.
 
Wanadhihaki wee matokeo yake siku hadi siku wanaendelea kufa wao na huyo wanaye mwita mgonjwa anazidi kuchanja mbuga!
 
Sasa kama ni kweli tushindwe kusema nyie si mahaba yanawasumbua
 
Kufurahia uzima wako ni shukurani kwa mungu.unaonyesha namna mungu alivyokujaali piga p up 10 hapo ulipo hapa kazi tu
 
Hakuna mzaha hata kidogo. Magufuli yupo barabarani kijiji kwa kijiji. Chopa baadaye.
 
ni dharau kubwa kura yangu hawapati hao fisiem
 
Ambaye hajawahi kuwa mgonjwa na hatarajii kabisa kuwa mgonjwa katika maisha yake kura yake ampe mzee wa push ups.
 
Sasa kama ni kweli tushindwe kusema nyie si mahaba yanawasumbua


Pahah hah haaaaaa! Nendeni tu huko Apollo kwa vificho, lakini twawaona mkirudi mkiwa packed (kufungashwa) kwenye vibox! Kama sato walio tayari kuwa exported. Hayo ni malipo ya dharau na matusi yenu kwa wasiojiweza. Wagonjwa na woooote wenye hali za kimaisha zinazodhihakiwa na watawala magamba na familia zao, kura zoooote kwa UKAWA.
 
Hivi ni nani alikuomba uwapigie kura hao fisiem?

Ni mpumbavu wa Magu (Magu Fool). Tena mpaka analia jukwaani na kuanza kupiga push-ups. Sijui ni push-ups kweli au midadi ya malavidavi, manake nasikia hajawa na mkewe kitambo. So huenda jogoo aliwika, akaona amalize kidizain vile, hah haaaaaa!
 
Hii topic imenigusa sana kwa kweli. Kama kweli kuna mwanadamu ana nguvu zaidi ya mungu basi tutaona mwaka huu. Ni imani mungu hamtupi mja wake.
 
Hapa duniani kila mtu anmtegemea Mungu kuishi uhai na afya tunapewa na Mungu,hivi hamjui kwamba Raisi Lowasa atawazika hao wanao jidai wana afya?
 
Kwa muda wa siku takribani 48 tumejionea kampeni za kisiasa kuwania kiti cha ukuu wa nchi ya JMT. Kuna mambo yamekuwa yakijitokeza ambayo kimsingi ni dharau na ufedhuli unaofanywa na watu wasio na chembe ya huruma kwa wagonjwa.


Hebu tujiulize ni nani hajawahi kuugua? Je mgonjwa kama raia yeyote wa JMT hana haki ya kuchaguliwa kuwa kiongozi? Kwanini CCM na wapambe wake wamekuwa wakiwadhihaki wagonjwa? Hebu fikiria wewe mgonjwa au ndugu yako mgonjwa unasikia watu wanawatukana na kudhihaki na wanadiriki kusema marehemu hatuoni huu ni efedhuli?
Kitendo cha kupiga push ups ni hali ya dharau kabisa kwa wagonjwa.

Yaani unaonesha kuwa wewe una nguuvu na umejaaliwa kuliko huyo unayemdhihaki. Hebu kama unafikiri kupiga push up ni vizuri nenda wodi za wagonjwa kafanye hivyo kama unataka kuwaburudisha uone.

Ikiwa mgombea amefikia hatua hii ya kujitoa utu wake na kuwadhalilisha wagonjwa kwa kupiga push ups, nachukua nafasi hii kuwaomba wale wote wanaoguswa na maumivu, mateso na taabu wanazopata wagonjwa wahakikishe ifikapo tarehe 25 Oktoba 2015 kuwakataa John Magufuli na wote waliowadhihaki wagonjwa aidha kwa maneno au/na matendo yao.

Tumuombe Mungu awaaibishe kwenye boksi la kura washindwe vibaya ila tuwaombee Mungu aendelee kuwapa afya njema.

Kama umekubaliana nami naomba ugonge like ili Mungu atende kwani peooooooooplesssss ni power. Mungu ibariki Tanzania.
Kweli kabisa, hata kwa wagombea wao ni dhihaka kubwa, msione wagombea wanaongea majukwaani, kuna watu wapo majukwaani na kansa, kuna wenye magonjwa ya maini na figo, kuna wenye pumu na magonjwa ya moyo etc lakini wakati mwingine inabidi tu na wao wapige pushup ili wafit kwenye kundi la afya bora. Jipimeni viongozi wa ccm kuna wananchi wagonjwa wanaotesekeka na magonjwa yanayotibika, kwa sababu hospitali hakuna dawa wamejikokota kwa shida kuja mkutanoni halafu mnaanza kuwapigia pushup, dharau kabisa
 
Mbaya zaidi wanapo kwenda Apolo hakuna mtu anaye jua ila Mungu ndo anawaumbua kwaani wanarudi wakiwa kwenye mabox na yule wanae twambia mgonjwa anazidi kuimarika kadri siku zinavyo kwenda
 
Umeandika kitu kikubwa sana Magufuli angekuwa na busara asingefanya aliyofanya kny majukwaa,hafai kamwe kuwa Raisi.
 
Back
Top Bottom