Don Mangi
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 2,198
- 852
Kama kawaida yangu ambavyo situlii mahali pamoja nchi hii ya thelathini kwa ukubwa duniani, katika safari zangu za hapa na pale nikatumbukia wilaya ya Ruangwa mkoani Lindi, moja kati ya mikoa mikubwa Tanzania.
Ki ukweli Don Mangi napenda sana watoto, katika pitapita zangu za hapa na pale nikafika mahali nikaona nipumzike kutokana na jua kali la mchana, palikua na mti mdogo halafu chini yake kuna madereva wa bodaboda wamepaki, kwa pembeni hivi kulikua na watoto wadogo wanacheza nikawa nawaangalia huku nikiwachekea na ku-make faces. Kitoto kimoja katika lile kundi kilipenda ule mchezo, ghafla kikatoka kilipokua na marafiki zake na kuja kunikimbilia, kikaja magotini na kuanza kunivuta miguu huku kikicheka kwa furaha, vile nilikua nimesimama nikakiangalia kichwani kilikua na tetekuwanga kama ndo zinaishia kupona hivi, sikutilia maanani, karibu na pale palikua na kaduka, basi huyoo nikaenda kununua maji ya kunywa katoto kakanifwata nikakanunulia pipi basi kakaondoka na mie nikaendelea na kilichonipeleka kule.
Siku kama mbili zimepita toka niende huko na kurudi,Sasa cha kushangaza,jana usiku nilikamatwa na homa moja kali kweli yani mpaka ikanibidi kuamka. Nikajitahidi mpaka kufika asubuhi, nikahisi nina malaria, nikakamatia dawa zangu za malaria nikaendelea kuzunguka mjini, homa ikawa pale pale, doh! Yani usiku haufai, kitanda kinalowa jasho na huku nasikia baridi.
Sasa leo asubuhi naamka naanza kuona vipele vinanitokea sana sana usoni vinawasha na vinajaa maji. Kichwa kinagonga usipime kama vile watu wamefungua crusher ya kuponda mawe. Kuchukua kioo na kujiangalia fasta. . .Salaale! Tetekuwanga zimetambaa uso mzima hata naogopa kujiangalia.Dah! Akili ikacheza fasta nikamkumbuka yule dogo aliyekua anacheza miguuni pangu.
Bahati nzuri ninapokaa si mbali na duka la dawa(maana hospitali huku ni kitendawili, hiyo foleni nmb mara mbili) ndo nikaenda pale akanishauri ninunue calamine lotion na vidonge ninywe pen v., Kiufupi sijawahi kuugua hii kitu toka nimezaliwa. niko ndani tu kama mzazi vile, hamu ya kula sina, ni kusikia baridi na kuvuta shuka.
Jamani kwa anayejua kama hiyo prescription niliyopewa ni sawa au kama kuna maboresho.
Dah. . .dogo lakini kanitenda.
Thanx,
Ki ukweli Don Mangi napenda sana watoto, katika pitapita zangu za hapa na pale nikafika mahali nikaona nipumzike kutokana na jua kali la mchana, palikua na mti mdogo halafu chini yake kuna madereva wa bodaboda wamepaki, kwa pembeni hivi kulikua na watoto wadogo wanacheza nikawa nawaangalia huku nikiwachekea na ku-make faces. Kitoto kimoja katika lile kundi kilipenda ule mchezo, ghafla kikatoka kilipokua na marafiki zake na kuja kunikimbilia, kikaja magotini na kuanza kunivuta miguu huku kikicheka kwa furaha, vile nilikua nimesimama nikakiangalia kichwani kilikua na tetekuwanga kama ndo zinaishia kupona hivi, sikutilia maanani, karibu na pale palikua na kaduka, basi huyoo nikaenda kununua maji ya kunywa katoto kakanifwata nikakanunulia pipi basi kakaondoka na mie nikaendelea na kilichonipeleka kule.
Siku kama mbili zimepita toka niende huko na kurudi,Sasa cha kushangaza,jana usiku nilikamatwa na homa moja kali kweli yani mpaka ikanibidi kuamka. Nikajitahidi mpaka kufika asubuhi, nikahisi nina malaria, nikakamatia dawa zangu za malaria nikaendelea kuzunguka mjini, homa ikawa pale pale, doh! Yani usiku haufai, kitanda kinalowa jasho na huku nasikia baridi.
Sasa leo asubuhi naamka naanza kuona vipele vinanitokea sana sana usoni vinawasha na vinajaa maji. Kichwa kinagonga usipime kama vile watu wamefungua crusher ya kuponda mawe. Kuchukua kioo na kujiangalia fasta. . .Salaale! Tetekuwanga zimetambaa uso mzima hata naogopa kujiangalia.Dah! Akili ikacheza fasta nikamkumbuka yule dogo aliyekua anacheza miguuni pangu.
Bahati nzuri ninapokaa si mbali na duka la dawa(maana hospitali huku ni kitendawili, hiyo foleni nmb mara mbili) ndo nikaenda pale akanishauri ninunue calamine lotion na vidonge ninywe pen v., Kiufupi sijawahi kuugua hii kitu toka nimezaliwa. niko ndani tu kama mzazi vile, hamu ya kula sina, ni kusikia baridi na kuvuta shuka.
Jamani kwa anayejua kama hiyo prescription niliyopewa ni sawa au kama kuna maboresho.
Dah. . .dogo lakini kanitenda.
Thanx,