My girl is better than yours

My girl is better than yours

Nilifanya hayo yote tena zaidi ya huyo wa kwako almost 10 years unamvulia mtu kwa kila hali ila siku tu alipopata kazi hakuna rangi niliacha kuisoma...... Muombe tu Mungu huyo awe kweli ni mke wako na wewe ni mume wake.... Pia usidharau wanawake wengine ni vile tu kila mtu hawezi elezea kilchomo moyoni mwake hata huyo wako siku mkiachana kuna wanaume watamuona hafai ingawa sio kweli maisha ni safari ndefu sana zaidi ya unavyodhani
Hajui huyoo wanawake wanabadilishwa na wanaume hata Mimi nilikuwa hivyo tena zaidi ya huyo.
 
Watu kama nyie mwisho wa siku ndo mnakuaga wasaliti kwa wadada kama hao...Cha ajabu kbsa unaweza hata usimuoe., kwa wanaume tulivyo na akili za kupayuka
Mkuu ni kweli lakini, huyu mie lazima nimuoe. Home sijamtambulisha rasmi lakini wazazi wangu wanamjua kuwa ni nani kwangu.
 
Habarini wana MMU,

Leo nimeamua kushare kitu nanyi juu ya mahusiano yangu ambayo nipo proud sana kuwa nayo.

Nipo kwenye mahusiano takribani miaka saba sasa binti niliyenae nimuelewa sana sana, anajua ni nini tafsiri ya maisha kwani kwa miaka hii yote japo sijamuoa lakini amesimama kama mke mtarajiwa kwangu. Msemo wake hataki kupoteza nafasi hii.

Nilimkuta akiwa bikra miaka kadhaa iliyopita niliweza kuwa mwanaume wa kwanza kwake. Hajawahi kuniomba hela hata mara moja ila huwa ananiambia hawezi niomba hela ila nikiona ana tatizo basi nijiongeze kumpa hela. Am proud of her kwani kuna muda chuoni nilikuwa naishi gheto naye akaamia kwangu tulisaidia kwa kila kitu.

Binti alikuwa yupo radhi akae wiki hata mbili bila kusuka ili ile hela akanunue mboga na unga tuweze kula. Kipindi hicho ndicho nilichamini kuwa nimepata mke kabisaa kwani nilifukuzwa chuo. Aliweza nishauri sana kuwa nisirudi nyumbani nikae nae ye akiwa chuo mie nianze kufanya biashara then baada ya muda ndo nirudi chuo tena.

Nilikubaliana nae na boom lake lilipotoka siku moja ghetto usiku tumemaliza kula aliweza nipatia laki tano at that time alikuwa only 22 yearz kweli boom lake alibakiwa na hela ndogo akanisihi niwe nafata mzigo wa nguo za kike then ye atakuwa anaenda nazo chuo kuuza kwa wadada wenzake.

Tuliweza kupata hela ya kula na maisha yaliweza kwenda taratibu, mwaka ukaisha ikanibidi nirudi chuo alisimama nami kwa hali yote akinambia ule mtaji ndio niongeze nkalipie ada. Finally nishamaliza chuo now nipo naangaika na ajira.

Upande wa maisha yangu na yeye tunaishi vizuri hana kiburi, hapendi kujiona yeye ndio yeye japo ni mzuri sana. Ghetoni kwetu kachangia vitu vingi nami pia nimechangia vitu vingi tu hakika ni muelewa wa hali ya juu kwani hana tamaa ya pesa kwani kwao wapo vizuri. Siku zote huwa ananiambia anafanya haya yote sababu ananipenda na hataki kunipoteza na kama siku nikitaka kumwacha bora nimpe mimba ndio nimwache.

Tumesaidiana mambo mengi nikiwa na shida she is alwayz there now nasubiri tu amalize chuo nioe kabisa kabisa.
Mkuu ukimtelekeza binti huyo uteguke kiuno kabisa. Unaongoja nini kurasmisha sasa?
 
Oa huyo mwanamke kabla hata hajamaliza chuo, kabla hujapata hela/maisha mazuri.., usijekateleza ukamwacha au yeye akapitiwa na kile kinachoitwa shetani.
HUTAKAA UWE NA AMANI NA MWANAMKE MWINGINE TENA KAMA UKIMWACHIA HUYO iwe kwa wewe au yeye au kwa makosa yake.

Usijisahau saaana kuja kumsifia tu humu, ukadhani yeye siyo binadamu. jitihadi kuliimarisha penzi, vitu vipya nn, vizawadi nini....

siyo ndo umwache apaukeeeeeee
 
Endelea kujadili halafu kuna mwanaume atamtangazia ndoa hapo sasa ndyo utajua kwanini tunaibiwa Mchanga
 
Back
Top Bottom