My Best friend ameoa

Mimi nina best frend wangu sanasana ni mwanaume na mimi ni mwanamke. ni rafiki yangu wa siku nyingi kiasi kwamba ndugu zangu wote wanamjua na mume wangu anamjua na wanapatana sana sometime tunatoka wote out sometimes tunafanya nyama choma kwake au kwangu tunaita rafiki zetu wengine tunakunywa pombe na kufurahi pamoja.

Kwa urafiki huo utakuta kila anachofanya lazima ataniambia, akiwa na mwanamke mpya ataniambia akiwa anataka kununua kiwanja tutaenda wote nimpe ushauri akitaka kubadili gari lazima atanishirikisha hata picha atanitumia nione ili nimshauri kama ni zuri au baya. Ikiwa bday yangu ni yeye atakumbuka na kuniletea zawadi hata kama mume amesahau, na sikukuu zingine pia, akisafiri lazima aje na zawadi yangu pia.

Kwa urafiki wetu ulivyo hata nikipata tatizo labda usiku nimeharibikiwa na gari nitampigia yeye simu aje kunisaidia, nikiwa na matatizo na mume wangu yanayosumulika huwa namwambia anipe ushauri, hata kuna kipindi tuko safarini mtoto aliumwa ni yeye tulimuomba ampeleke hospital. naeleza yote haya ili muelewe ni rafiki wa aina gani ili iwe rahisi kunishauri badae.

Rafiki yangu huyu ni playboy fulani hivi anapenda sana wanawake ,kila mara ana dem mpya nimempigia kelele sana mpaka mwaka juzi nikamuunganisha na msichana mmoja hivi,alikuwa nje kimasomo ni ndugu wa rafiki yangu mwingine, badae mwaka jana wakafunga ndoa. yule dem alikuwa ananipenda sana wakigombana nitawasuluhisha na mambo mengine.

Tatizo lililojitokeza sasa hivi mwanamke ananichukia sana nahisi ni sababu rafiki yangu ananijali sana kiasi hata mimi mwenyewe ningekuwa mke wa rafiki yangu ningesikia kawivu flani hivi. Sasa rafiki yangu kanambia wanagombana sana na mkewe kuhusu mimi kwa nini nilimtafutia mke ambae haelewi uhusiano wetu?Kanambia anampenda sana mkewe ila pia ana value urafiki wetu cause tupo kama ndugu.

Pia Kanambia nimwite nimueleweshe sasa mnafikiri nikimwita atanielewa? na nikimwita nimwambie nini? ni vizuri nimwite nikiwa na mume wangu? Mimi nimemwambia rafiki ndoa yake ni muhimu zaidi kuliko mimi rafiki tuwe tunaonana kwenye mambo ya muhimu kama sherehe msiba na kadhalika mnafikiri huu ushauri ni mzuri? Naomba ushauri wanajamvi am about to loose my very best friend
naomba kuwakilisha
hii story imenishangaza kitu kimoja, hivi huyo mume wako wewe kipindi chote hicho ameruhusu hiyo boundless friendship yako wewe na hilo jibaba? yaani unaletewa vizawadi na mnaonana kila siku? usiku unampigia akuje kukusaidia, khaaaa! nazani hii ndoa yako inahitaji msaada kabla hii ndoa ya rafiki yako.
 
hodii junior member hapaaa....jamani huku si kujipunguzia muda wa kuishi kwa kukosa furaha?..msichukue majukumu ya mungu na malaika ingawa tunatakiwa kutoa ushauri ...kosa lako hukumshauri aende mbele za mungu hata kama ulimshauri yule binti ni mzuri.. sasa naomba kwanza utubu kwamba ulikosea mbaya zaidi unajua jamaa ni mtu wa vidosho...au hujui makaa ya moto uliyemwunganisha na best yako na huenda binti ni dada safi na tatizo kwa best yako .....hapoooooooo ni toba tu.
 
ila huo urafiki wenu umezidi bana... lool

kinachomsumbua huyo dada ni wivu wa kawaida kabisa its just human instincts hata kama huna uhusiano wa hivyo na huyo jamaa ye atapata wivu fulani tu wala sishangai its involuntary

Mimi nina mume wangu na huwa tunakutana wote sasa kwa nini apate wivu na alipokuwa ulaya kila akipga sime akimkosa ananipgia mimi inakuwaje sasa hv kujisikia hvyo
 
hii story imenishangaza kitu kimoja, hivi huyo mume wako wewe kipindi chote hicho ameruhusu hiyo boundless friendship yako wewe na hilo jibaba? yaani unaletewa vizawadi na mnaonana kila siku? usiku unampigia akuje kukusaidia, khaaaa! nazani hii ndoa yako inahitaji msaada kabla hii ndoa ya rafiki yako.

Jambo usilolijua ndugu yangu!!!!!!...... mume wangu hana neno kabisa wala hatujawahi kugombana juu ya hilo anamjua na anaheshimu urafiki wetu. naposema tunakutana haimaanishi kila siku ya mwenyezi mungu ila mawasiliano ni karibu kila siku kama marafiki wa kawaida.
 
Gaga your husband should be your best friend na si ntu mwingine. ukishaingia kwenye ndoa achana na u best na watu wengine, unayumbisha ndoa ya mwenzio kitu ambacho si kizuri
 
Aaaah huo urafiki hapana,coz hakuna mwanamke ambaye anaweza kuvumilia mumewe awe dat's close na mwanamke mwingine hata kama aliwakuta marafiki.Cha kufanya ni kupunguza tu huo urafiki wenu kwani unatakiwa kujua kuwa ameo huyo rafiki yako,na pia ebu wewe jaribu kujiweka position ya huyo mwanamke mwingine uone jinsi anavyoumia huyo mwenzio.
Ni mawazo yangu tu.
 
Gaga your husband should be your best friend na si ntu mwingine. ukishaingia kwenye ndoa achana na u best na watu wengine, unayumbisha ndoa ya mwenzio kitu ambacho si kizuri

:clap2::clap2::clap2::clap2::clap2::clap2::clap2:
 
Gaga sijui kama huyo rafiki yako bado anakufuata kwa ushauri japo
ana mke wake tayari ila kama ndivyo....wa kuongea nae hapo sio
mkewe bali ni huyo rafiki yako!!Kama kweli huna nia ya kuvunja ndoa
yao inabidi umwambie aache kabisa....akitaka ushauri amuombe mke
wake.....mfano tu:sidhani kama inaleta picha nzuri mtu wa pembeni
kuwachagulia vitu ambavyo vinawahusu wao...kwasababu kama mko
karibu kama unavyosemana bado unatoa ushauri lazima huyo rafiki
yako atakua anathamini sana mawazo yako kiasi cha kuyafanyia kazi!
Na hata kama sio jaribuni kupunguza mawasiliano yenu....though huyo
dada atakua na wivu wa ajabu kwasababuwewe ndiye uliyemtambulisha
ila anayo haki ya kua nao!!!Una mume wako...mfanye yeye ndo awe rafiki
yako wa karibu.....mwache mwenzio nae aenjoy ndoa yake na mumewe!!!!!​
 
hii story imenishangaza kitu kimoja, hivi huyo mume wako wewe kipindi chote hicho ameruhusu hiyo boundless friendship yako wewe na hilo jibaba? yaani unaletewa vizawadi na mnaonana kila siku? usiku unampigia akuje kukusaidia, khaaaa! nazani hii ndoa yako inahitaji msaada kabla hii ndoa ya rafiki yako.

ucshangae mume ***** wako wengi mjini hapa
 
No no no no, nimegundua wewe Gaga ni mnyanyasaji, yaani unamnyanyasa mme wako kwa sababu ya katatizo kale ka kushindwa ko-do for about four yrs now, unajua kabisa kuwa hawezi kukujia juu wewe kuwa close na wanaume wengine kwa sababu ya tatizo lake. Naamini kabisa asingekuwa na lile tatizo ulilotuambia kwenye thread fulani asingekubali wewe kuwa na urafiki wa karibu na man mwingine katu.

Unasema sasa amekuwa mpolee, pengeni ni unyonge ya vile unavyofanya. Saidiana na mme wako kulitatua lile tatizo bila kujenga mazingira ya kumsononesha moyo wake(yawezakana ukawa hujui kuwa unamsononesha). Na Mungu awasaidie.
 
No no no no, nimegundua wewe Gaga ni mnyanyasaji, yaani unamnyanyasa mme wako kwa sababu ya katatizo kale ka kushindwa ko-do for about four yrs now, unajua kabisa kuwa hawezi kukujia juu wewe kuwa close na wanaume wengine kwa sababu ya tatizo lake. Naamini kabisa asingekuwa na lile tatizo ulilotuambia kwenye thread fulani asingekubali wewe kuwa na urafiki wa karibu na man mwingine katu.

Unasema sasa amekuwa mpolee, pengeni ni unyonge ya vile unavyofanya. Saidiana na mme wako kulitatua lile tatizo bila kujenga mazingira ya kumsononesha moyo wake(yawezakana ukawa hujui kuwa unamsononesha). Na Mungu awasaidie.

mumewe ana tatizo gani? Mbona nje anachapa kama kawaida!! Ni yeye tu ndo anayeshindwa kumfanya! Ndo maana hii story haijatulia! Huo urafiki wako na huyo mwanaume ulishamharibu kisaikolojia mme wako. Sasa inaenda kumharibia mwenzio. game over...
 
....that is too much on your part! ur friend (she) is right on the other side of the coin.......!
 
No no no no, nimegundua wewe Gaga ni mnyanyasaji, yaani unamnyanyasa mme wako kwa sababu ya katatizo kale ka kushindwa ko-do for about four yrs now, unajua kabisa kuwa hawezi kukujia juu wewe kuwa close na wanaume wengine kwa sababu ya tatizo lake.

Chapa kumbuka nipo about 16 years in marriage na tatizo la mume ni miaka minne tu iliyopita na nipo na rafiki yangu huyo about 20 years yaani wakati nina miaka 14 15 hv huoni kwmba mume alitukuta na akaelewa tena wala hajaona ni ishu kuwa na huyo rafiki kwa hiyo kusema namnyanyasa haiwezekani labda yeye ndio anaeninyanyasa kwa sasa. Pia huyu rafiki yangu na yeye amekuwa kama rafiki na mume wangu mara nyingi huwa wanakuwa pamoja hata kama mimi sipo

Unasema sasa amekuwa mpolee, pengeni ni unyonge ya vile unavyofanya. Saidiana na mme wako kulitatua lile tatizo bila kujenga mazingira ya kumsononesha moyo wake(yawezakana ukawa hujui kuwa unamsononesha). Na Mungu awasaidie.
Chapa kumbuka nipo about 16 years in marriage na tatizo la mume ni miaka minne tu iliyopita na nipo na rafiki yangu huyo about 20 years yaani wakati nina miaka 14 15 hv huoni kwmba mume alitukuta na akaelewa tena wala hajaona ni ishu kuwa na huyo rafiki kwa hiyo kusema namnyanyasa haiwezekani labda yeye ndio anaeninyanyasa kwa sasa. Pia huyu rafiki yangu na yeye amekuwa kama rafiki na mume wangu mara nyingi huwa wanakuwa pamoja hata kama mimi sipo
 
mumewe ana tatizo gani? Mbona nje anachapa kama kawaida!! Ni yeye tu ndo anayeshindwa kumfanya! Ndo maana hii story haijatulia! Huo urafiki wako na huyo mwanaume ulishamharibu kisaikolojia mme wako. Sasa inaenda kumharibia mwenzio. game over...

He never complains about it. miaka yote hiyo unafikiri angeweza kuvumilia? navyomjua mimi mume wangu hawezaki weka kitu moyoni hata na wala haogopi kuniambia kitu. kuna kipindi fulani nilikuwa na rafiki wa kike chuoni alikuwa hampendi kila siku ananiambia huyu sio rafiki mzuri simpendi mie nipo tu bize nae mpaka siku moja tulimfata hotel moja hv mjini nikiwa nae akamwambia rafiki yangu huyo i dont like you near my wife i dont like your company leave my wife alone tena kwa kushout!
You think that kind of husband anaweza vumilia kitu chochote ambacho hapendi?
 
Habari yako Gaga,unaendeleaje kwanza na ile ishu iliyopita????

Nafikiri kulipaswa kuwe na mipaka kati yako na huyo kaka baada ya yeye kuoa.....yes nyie ni ma-best friend lakini,wote tuna wivu na tuwapendao na hatupendi ku-share attention na wanawake wenzetu kwa mwanaume tunayempenda,kumtunza na kumjali sana......

Usiwe kikwazo cha ndoa ya watu kwa ku-value sana u-best friend wenu,have some boundaries,it takes two kuwa katika strong bond kama uliyo nayo wewe na huyo kaka,nakushauri keep a distance,waache wawe na sababu nyingine ya kutofautiana na sio wewe.....kama ni rafiki wa kweli huyo kaka ataheshimu mawazo yako kwakuwa una roho safi na unawatakia mema......

Muite huyo msichana uzungumze nae na si vibaya mumewe na muwe wako wakawepo mkaweka mambo wazi na si kwa staili ya kusutana just kueleweshana......all the best!!:coffee:

I love you Michelle! I love everything about you especially how you advise someone. Please, keep the good work. Love you!
 
Mambo hayoooo!!!!!!!.

Maisha haya kaleta mzungu, sisi waafrika, vijana wa kiume na wakike kuna mipaka kwenye urafiki. Kwanza ukiwa na rafiki wa jinsia nyingine na sio mpenzi, kuna fitna ndugu zanguu!!. Maisha haya ya kibepari, eti msichana na kijana wanashare nyumba lakini hawana uhusiano wo-wote wa kimwili!!, vyawezekana huko ughaibuni lakini AFRICA, mambo kama kama hayo hayawezekani. Mukiji-epusha na ukaribu huo madhara kama haya hamtayapata. USHAURI!!!!!
 
Lady Gaga itabidi upunguze urafiki wako na huyo rafiki yako ili unusuru ndoa ya mwenzio
Kwa vile wewe una kwako na mmeo na maisha yako endelea na family yako
Urafiki wenu uwe wa kawaida kabisa ,vizawadi na mazoea mangine ya karibu punguzeni,
Katika hali ya kawaida yule mwanamke mwingine anashindwa kuamini labda mko karibu saaaaaaaaaaaaana

You are very right Mamaa!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Lakini Mazoea nayo yana Taabu. Kuyaacha ni shughuli pevu.
 
....that is too much on your part! ur friend (she) is right on the other side of the coin.......!

Sio too much kama unamchukulia ni rafiki tu na mmeshazoeana. Jamani ni rafiki yangu wa miaka mingi tu
 
Back
Top Bottom